< Josué 11 >

1 A cette nouvelle, Jabin, roi de Haçor, envoya un message à Jobab, roi de Madôn, au roi de Chimrôn, et au roi d’Akchaf,
Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
2 ainsi qu’aux rois qui demeuraient dans le nord, sur la montagne et dans la plaine, au midi de Génésareth et dans la vallée et dans la région de Dor à l’occident,
na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
3 aux Cananéens de l’orient et de l’occident, aux Amorréens, Héthéens, Phérézéens, Jébuséens de la montagne, Hévéens établis au pied du Hermon, dans le pays de Mispa.
kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
4 Et ils sortirent avec toutes leurs armées, multitude nombreuse comme les sables du rivage de la mer, avec un nombre immense de chevaux et de chars.
Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
5 Tous ces rois, s’étant donné rendez-vous, vinrent camper ensemble près des eaux de Mérom pour livrer bataille à Israël.
Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
6 Cependant l’Eternel dit à Josué: "Ne les crains point, car demain, à pareille heure, je les ferai succomber tous devant Israël; et tu couperas les jarrets de leurs chevaux, et tu livreras leurs chars aux flammes."
Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
7 Josué, avec tous les gens de guerre, les atteignit à l’improviste près des eaux de Mérom et tomba sur eux;
Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
8 et l’Eternel les livra au pouvoir des Israélites, qui les battirent et les poursuivirent jusqu’à Sidon la Grande, jusqu’à Misrefot-Maïm et, vers l’orient, jusqu’à la vallée de Mispa; ils les taillèrent en pièces jusqu’au dernier.
naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
9 Et Josué, se conformant aux ordres de l’Eternel, coupa les jarrets de leurs chevaux et brûla leurs chars.
Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
10 Alors, rebroussant chemin, Josué prit Haçor et passa son roi au fil de l’épée (Haçor était, à cette époque, la tête de tous ces royaumes).
Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
11 Et l’on extermina sans merci, par l’épée, toute sa population, sans épargner une seule vie, et l’on réduisit Haçor en cendres;
Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
12 et toutes les villes des autres rois et ces rois eux-mêmes, Josué les prit et les extermina par l’épée, comme l’avait ordonné Moïse, serviteur de l’Eternel.
Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
13 Toutefois, aucune des villes établies sur les hauteurs ne fut brûlée par Israël, à l’exception de Haçor seule, que Josué livra au feu.
Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
14 Tout le butin de ces villes ainsi que le bétail, les Israélites s’en emparèrent; mais les personnes furent toutes passées au fil de l’épée, on les extermina sans en épargner une seule.
Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
15 Comme l’Eternel l’avait ordonné à son serviteur Moïse, ainsi Moïse avait ordonné à Josué; et ainsi fit Josué, n’omettant aucun point de ce que l’Eternel avait prescrit à Moïse.
Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
16 Josué conquit donc tout ce pays: la Montagne avec tout le midi et tout le pays de Gochén, la vallée et la plaine, et toute la montagne d’Israël et ses vallées;
Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
17 depuis la montagne Pelée qui s’élève vers Séir, jusqu’à Baal-Gad, dans la vallée du Liban, au pied du mont Hermon; et il vainquit tous leurs rois et les mit à mort.
kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
18 Pendant de longs jours, Josué guerroya avec tous ces rois.
Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
19 Pas une ville, à l’exception des Hévéens habitants de Gabaon, ne se soumit pacifiquement aux enfants d’Israël; ils durent les conquérir toutes par les armes.
Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
20 Dieu avait permis qu’ils acceptassent résolument la lutte avec Israël afin qu’on les exterminât sans merci; car il fallait qu’ils fussent anéantis, comme l’Eternel l’avait prescrit à Moïse.
Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
21 En ce même temps, Josué marcha contre les Anakéens, qu’il fit disparaître de la montagne, de Hébron, de Debir, d’Anab, de toute la chaîne de Juda et de toute celle d’Israël; tous, Josué les détruisit ainsi que leurs villes.
Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
22 II ne resta plus d’Anakéens dans le pays des enfants d’Israël; il n’en demeura que dans Gaza, dans Gath et dans Asdod.
Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
23 Josué, ayant conquis tout le pays, selon ce que l’Eternel avait dit à Moïse, le donna aux Israélites comme possession héréditaire, en le répartissant selon leurs tribus; et le pays se reposa de la guerre.
Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.

< Josué 11 >