< Job 40 >

1 L’Eternel, répondant à Job, dit:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Le censeur du Tout-Puissant persistera-t-il à récriminer contre lui? Le critique de Dieu répondra-t-il à tout cela?
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Job répondit à l’Eternel et dit:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Hé quoi! Je suis trop peu de chose: que te répliquerai-je? Je mets ma main sur ma bouche.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 J’Ai parlé une fois… je ne prendrai plus la parole; deux fois… je ne dirai plus rien.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Alors l’Eternel répondit à Job du sein de la tempête et dit:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Ceins tes reins comme un homme: je vais t’interroger et tu m’instruiras.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Prétends-tu vraiment prendre en défaut ma justice, ‘me condamner pour te justifier?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 As-tu donc un bras comme celui de Dieu? Fais-tu retentir comme lui la voix du tonnerre?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Alors pare-toi de majesté et de grandeur, revêts-toi de splendeur et de magnificence.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Lance de toutes parts les éclats de ta colère et, d’un regard, abaisse tout orgueilleux.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 D’Un regard, humilie tout orgueilleux, et écrase les méchants sur place.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Enfouis-les tous ensemble dans la poussière, confine leur face dans la nuit du tombeau.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Alors moi-même je te louerai de ce que ta droite t’aura donné la victoire.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Vois donc le Béhémoth que j’ai créé comme toi: il se nourrit d’herbe comme le bœuf.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Admire la force qui est dans ses reins, la vigueur qui réside dans les muscles de son ventre.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 Sa queue se dresse comme un cèdre, les nerfs de ses cuisses sont entrelacés.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 Ses os sont des tuyaux d’airain, ses vertèbres des barres de fer.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Il est une des œuvres capitales de Dieu: Celui qui l’a fait l’a gratifié d’un glaive.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Les montagnes produisent du fourrage pour lui, et là toutes les bêtes des champs prennent leurs ébats.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Il se couche sous les lotus, sous le couvert des roseaux et des marais,
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Les lotus le protègent de leur ombre, les saules du torrent l’enveloppent.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Voici que le fleuve se gonfle et il ne s’en émeut point; il demeurerait plein d’assurance si le Jourdain lui montait à la gueule.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Peut-on s’en emparer quand il a les yeux ouverts, lui percer le nez avec des harpons?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >