< Job 38 >
1 L’Eternel répondit à Job du sein de la tempête et dit:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Quel est celui qui dénigre les desseins de Dieu par des discours dépourvus de sens?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Ceins donc tes reins comme un homme: je vais t’interroger et tu m’instruiras.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Où étais-tu lorsque je fondais la terre? Dis-le, si tu en as quelque connaissance.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Qui a fixé ses dimensions, si tu le sais, ou qui a tendu sur elle le cordeau?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Sur quoi sont assis ses piliers, ou qui a lancé sa pierre angulaire,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 tandis que les étoiles du matin chantaient en chœur, et que tous les fils de Dieu poussaient des cris de joie?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Qui a fermé la mer avec des portes, quand elle sortit jaillissante du sein maternel,
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 quand je lui donnai la nuée pour vêtement et une brume épaisse pour langes;
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 quand je brisai son élan par mes barrières et lui posai des verrous et des portes,
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 et que je lui dis: "Jusqu’ici tu viendras et non au-delà: ici s’arrêtera l’orgueil de tes flots?"
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 As-tu jamais de ta vie donné des ordres au matin, assigné sa place à l’aurore,
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 pour qu’elle saisisse les bords de la terre et en rejette les méchants en une secousse?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Quand elle paraît, la terre se transforme comme l’argile sous le sceau, et les choses se présentent comme un riche vêtement.
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Les méchants sont privés de leur lumière à eux, et leur bras déjà levé est brisé.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 As-tu pénétré jusqu’aux sources de la mer, as-tu circulé au fonds de l’abîme?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Les portes de la mort se sont-elles dévoilées devant toi? As-tu vu l’entrée du royaume des ombres?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 As-tu mesuré l’immense étendue de la terre? Dis-le, si tu sais tout cela.
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Quel chemin mène à la demeure de la lumière, et où est l’habitation des ténèbres,
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 pour que tu les conduises dans leur domaine et reconnaisses les avenues de leur maison?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Tu le sais sans doute! Car tu étais né dès lors, et grand est le nombre de tes jours!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Es-tu entré dans les trésors de la neige, as-tu aperçu les dépôts de la grêle,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 que je tiens en réserve pour les temps de détresse, pour le jour du combat et de la guerre?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Quelle est la voie par où se disperse la lumière, par où le vent d’Est se répand sur la terre?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Qui a creusé des rigoles à l’averse, une route à l’éclair sonore,
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 pour arroser des régions inhabitées, le désert où il n’y a pas d’hommes,
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 pour abreuver les terres incultes et sauvages et faire pousser l’herbe nouvelle des prairies?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 La pluie a-t-elle un père? Qui engendre les gouttes de la rosée?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 De quel sein sort la glace, et le givre du ciel, qui l’a enfanté?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Les eaux se condensent comme la pierre et la surface des eaux se contracte.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Est-ce toi qui noues les bandeaux des Pléiades ou qui relâches les liens de l’Orion?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Est-ce toi qui fais paraître les planètes en leur temps et qui diriges la Grande-Ourse avec ses petits?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Connais-tu les lois du ciel? Est-ce toi qui règles sa force d’action sur la terre?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Te suffit-il d’élever ta voix vers la nuée, pour qu’elle t’envoie des masses d’eau?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Est-ce toi qui commandes aux éclairs de partir? Te disent-ils: "Nous voici?"
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Qui a mis de la sagesse, dans la brume sombre, ou qui a donné au météore l’intelligence?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Qui pourrait dénombrer les nuages avec sagacité, et qui incline les amphores du ciel,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 de manière à agréger la poussière en une masse compacte et à coller ensemble les glèbes de la terre?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Est-ce toi qui poursuis la proie pour le lion, qui assouvis la voracité des lionceaux,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 lorsqu’ils sont tapis dans leurs tanières ou se tiennent aux aguets dans les fourrés?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Qui prépare au corbeau sa pâture, quand ses petits crient vers Dieu et errent çà et là faute de nourriture?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?