< Job 37 >

1 C’Est aussi ce qui jette la frayeur dans mon cœur et le fait vivement tressauter.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Ecoutez attentivement le grondement de sa voix et le roulement qui sort de sa bouche.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Il le prolonge sous toute la voûte des cieux, et ses éclairs brillent jusqu’aux extrémités de la terre.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 A leur suite, c’est un bruit qui rugit: il tonne de sa voix majestueuse, et quand cette voix se fait entendre, il ne les retient plus.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Dieu fait retentir merveilleusement la voix de son tonnerre; il accomplit de grandes choses qui dépassent notre connaissance.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Car il dit à la neige: "Apparais sur la terre!" II envoie la pluie abondante, ses puissantes averses.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Alors il paralyse les bras de tous les hommes, afin que ces hommes, son œuvre à lui, apprennent à le connaître.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Et les fauves rentrent dans leur tanière et se terrent dans leur gîte.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 L’Ouragan surgit de ses retraites, le froid est amené par les vents d’aquilon.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Au souffle de Dieu se forme la glace et se contractent les nappes d’eau.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Il charge aussi la nue de vapeurs humides, dissémine ses nuages que traversent les éclairs.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Et ces nuages se déplacent en tourbillonnant sous son impulsion, en vue de leur besogne, pour exécuter ses ordres sur la surface du globe terrestre.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Il les suscite tantôt comme un fléau pour la terre, tantôt comme une source de bienfaits.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Ecoute, Job, tout ceci; lève-toi et considère les merveilles de Dieu.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Comprends-tu les lois qu’il leur impose et comment il fait briller ses nuages lumineux?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Comprends-tu les déploiements de la nuée, les prodiges de Celui qui possède la science parfaite?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Toi, dont les vêtements deviennent trop chauds, dès que la terre recouvre le calme sous l’influence du midi,
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 pourrais-tu lui aider à étendre les cieux, solides comme un miroir de métal?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Apprends-moi ce que nous pourrions lui dire: dans les ténèbres où nous sommes, nous manquons d’arguments.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Devra-t-on lui rendre compte quand je parle? Jamais homme a-t-il demandé à être anéanti?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Or donc, personne ne peut regarder le soleil qui brille radieux dans le ciel, lorsque le vent qui passe l’a nettoyé.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Si l’or vient du septentrion, Dieu, lui, demeure couvert d’une redoutable majesté.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Le Tout-Puissant, nous ne pouvons l’atteindre, lui qui est grand par la force; mais le droit et la parfaite justice, il ne les écrase point!
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 C’Est pourquoi les hommes le révèrent; quant à lui, il n’abaisse ses regards sur aucun des prétendus sages.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >