< Jérémie 52 >

1 Sédécias avait vingt-et-un ans lors de son avènement, et il règna onze ans à Jérusalem; le nom de sa mère était Hamoutal, fille de Jérémie de Libna.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
2 Il fit ce qui est mal aux yeux de l’Eternel, tout comme avait agi Joïakim.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
3 C’Est ainsi que la colère de Dieu se manifesta contre Jérusalem et Juda, jusqu’à ce qu’il les eût rejetés de devant sa face. Or. Sédécias entra en révolte contre le roi de Babylone.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
4 Alors, dans la neuvième année de son règne, le dixième mois et le dixième jour du mois, Nabuchodonosor, roi de Babylone, marcha avec toute son armée contre Jérusalem; ils campèrent sous ses murs et élevèrent des retranchements sur toute son enceinte.
Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
5 La ville subit le siège jusqu’à la onzième année du règne de Sédécias.
Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
6 Le quatrième mois, le neuvième jour du mois, la famine sévit dans la ville et les gens du peuple manquèrent de pain.
Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
7 Alors la ville fut ouverte par une brèche. Aussitôt tous les gens de guerre s’enfuirent en quittant la ville nuitamment par la porte du double rempart, attenante au parc du roi, tandis que les Chaldéens cernaient la ville, et ils prirent la direction de la Plaine.
Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
8 L’Armée chaldéenne se mit à la poursuite du roi, et elle atteignit Sédécias dans la plaine de Jéricho, alors que sa propre armée s’était débandée en l’abandonnant.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
9 On fit le roi prisonnier et on l’amena au roi de Babylone à Ribla dans le district de Hamat, et celui-ci prononça sa sentence.
naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
10 Le roi de Babylone fit égorger les fils de Sédécias sous ses yeux; il fit aussi égorger tous les notables de Juda à Ribla.
Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda.
11 Puis il fit crever les yeux à Sédécias et le chargea de chaînes. Enfin le roi de Babylone le déporta à Babylone, où il l’enferma dans la maison de détention jusqu’au jour de sa mort.
Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.
12 Le dixième jour du cinquième mois, qui correspond à la dix-neuvième année du règne de Nabuchodonosor, roi de Babylone, Nebouzaradan, chef des gardes, serviteur du roi de Babylone, entra dans Jérusalem.
Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
13 Il mit le feu au temple du Seigneur et au palais du roi; de même il livra aux flammes toutes les maisons de Jérusalem, à savoir toute maison d’un personnage important.
Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
14 Et tous les remparts qui entouraient Jérusalem furent démolis par l’armée chaldéenne, placée sous les ordres du chef des gardes.
Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu.
15 Une partie de la basse classe et le reste de la population qui était demeurée dans la ville, les transfuges qui s’étaient rendus au roi de Babylone et le surplus de la multitude furent envoyés en exil par Nebouzaradan, chef des gardes.
Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
16 Le chef des gardes, Nebouzaradan, ne laissa dans le pays que des gens de la classe inférieure comme vignerons et laboureurs.
Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
17 Les colonnes d’airain qui se trouvaient dans la maison de Dieu, les supports et la Mer d’airain du temple, les Chaldéens les mirent en pièces et en emportèrent l’airain à Babylone.
Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli.
18 Ils prirent aussi les cendriers, les pelles, les couteaux, les bassins, les cuillers et tous les ustensiles d’airain qui servaient au culte.
Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
19 Le chef des gardes s’empara encore des marmites, des brasiers; des bassins, des poêles, des chandeliers, des écuelles et des tasses tant en or qu’en argent.
Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
20 Quant aux deux colonnes, à la Mer unique, aux douze boeufs en airain placés sous les supports que le roi Salomon avait faits pour le temple du Seigneur, le poids de l’airain de tous ces objets ne peut être évalué.
Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
21 Chacune des colonnes avait dix-huit coudées de haut, un fil de douze coudées en mesurait le tour, et ses parois avaient une épaisseur de quatre doigts; l’intérieur était creux.
Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani.
22 Elle était surmontée d’un chapiteau d’airain; chaque chapiteau était haut de cinq coudées. Un treillage et des grenades entouraient le chapiteau, le tout fait d’airain. Il en était de même de la seconde colonne, également garnie de grenades.
Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza.
23 Les grenades qui apparaissaient sur le côté étaient au nombre de quatre-vingt seize; en réalité, le total des grenades qui entouraient le treillage s’élevait à cent.
Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.
24 Le chef des gardes s’assura de la personne de Seraïa, le grand-prêtre, de Cefania, le grand-prêtre suppléant, et des trois gardiens du seuil.
Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
25 Parmi les habitants de la ville, il arrêta un officier, préposé aux gens de guerre, sept des conseillers intimes du roi qui furent surpris dans la ville, le secrétaire, chef du recrutement, chargé d’enrôler la population du pays, ainsi que soixante hommes de cette population, qui se trouvaient dans la ville.
Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
26 Nebouzaradan, chef des gardes, emmena tous ces prisonniers et les conduisit au roi de Babylone à Ribla.
Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
27 Le roi de Babylone les fit frapper et mettre à mort à Ribla. dans le district de Hamat, C’Est ainsi que Juda fut exilé de son territoire.
Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
28 Voici le chiffre de la population que Nabuchodonosor emmena en exil dans la septième année de son règne trois mille vingt-trois Judéens;
Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni: katika mwaka wa saba, Wayahudi 3,023;
29 dans la dix-huitième année du règne de Nabuchodonosor, il emmena de Jérusalem huit cent trente-deux personnes;
katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza, watu 832 kutoka Yerusalemu;
30 dans la vingt-troisième année du règne de Nabuchodonosor, Nebouzaradan, chef des gardes, envoya en captivité sept cent quarante cinq Judéens: ce qui donne un total de quatre mille six cents hommes.
katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake, Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme. Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.
31 La trente-septième année de l’exil de Joïachin, roi de Juda, le douzième mois et le vingt-cinquième jour du mois, Evil-Merodac, roi de Babylone, gracia Joïachin, roi de Juda, et le fit sortir de la maison de détention.
Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.
32 Il lui parla avec bonté, et lui donna un siège placé au-dessus du siège des rois qui étaient avec lui à Babylone.
Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
33 Il lui fit changer ses vêtements de détention et l’admit constamment à sa table, toute sa vie durant.
Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
34 Son entretien, entretien permanent, lui fut assuré tant qu’il vécut de la part du roi de Babylone, suivant les besoins de chaque jour, jusqu’au moment de sa mort.
Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.

< Jérémie 52 >