< Jérémie 41 >

1 Dans le septième mois, Ismaël, fils de Netania, fils d’Elichama, qui était de race royale et un des hauts dignitaires du roi, arriva, accompagné de dix hommes, auprès de Ghedalia, fils d’Ahikam, à Miçpa; et là, à Miçpa, ils prirent part ensemble à un festin.
Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
2 Puis Ismaël, fils de Netania, et les dix hommes qui étaient avec lui se levèrent, frappèrent par le glaive Ghedalia, fils d’Ahikam, fils de Chafan, et le firent périr, lui que le roi de Babylone avait nommé gouverneur du pays.
Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
3 De même tous les Judéens qui entouraient Ghedalia à Miçpa, ainsi que les Chaldéens qui s’y trouvaientles gens de guerre, Ismaël les massacra.
Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
4 Le second jour, après le meurtre de Ghedalia, que personne encore ne connaissait,
Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
5 des hommes arrivèrent de Sichem, de Silo et de Samarie, au nombre de quatre-vingts, ayant la barbe rasée, les vêtements déchirés et le corps tailladé, portant dans leurs mains des offrandes et de l’encens qu’ils destinaient au temple de l’Eternel.
watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
6 lsmaël, fils de Netania, sortit de Miçpa pour aller à leur rencontre, en pleurant tout le long de la marche, et quand il fut auprès d’eux, il leur dit: "Venez trouver Ghedalia, fils d’Ahikam."
Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
7 Mais dès qu’ils eurent pénétré dans l’intérieur de la ville, Ismaël, aidé des hommes qui étaient avec lui, les égorga et les jeta dans une citerne.
Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
8 Parmi eux se trouvaient dix hommes qui dirent à Ismaël: "Ne nous fais pas mourir, car nous possédons des provisions cachées dans les champs, du froment, de l’orge, de l’huile et du miel." Il les épargna et ne les tua point comme leurs frères.
Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
9 Or, la citerne où Ismaël avait jeté les corps de tous les hommes qu’il avait frappés en même temps que Ghedalia, était celle que le roi Asa avait construite pour se défendre contre Baasa, roi d’Israël; c’est cette citerne qu’Ismaël, fils de Netania, remplit de cadavres.
Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
10 Et Ismaël fit main basse sur tout le reste de la population qui était à Miçpa, sur les princesses royales et l’ensemble des gens qui demeuraient a Miçpa et que Nebouzaradan, chef des gardes, avait placés sous l’autorité de Ghedalia, fils d’Ahikam. Ismaël, fils de Netania, les emmena tous comme prisonniers, et partit pour se rendre chez les Ammonites.
Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
11 Mais Johanan, fils de Karéah, et tous les commandants de troupes qui l’accompagnaient, ayant appris tout le mal fait par Ismaël, fils de Netania,
Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
12 ramassèrent tous leurs hommes, se mirent en route pour attaquer Ismaël, fils de Netania, et l’atteignirent près des grands étangs de Gabaon.
waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
13 Quand tout le peuple qui se trouvait avec Ismaël aperçut Johanan, fils de Karéah, et tous les commandants de troupes qui l’accompagnaient, il fut dans la joie.
Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
14 Et tous les gens qu’Ismaël avait emmenés comme prisonniers de Miçpa firent volte face et, ayant changé de direction, se rallièrent à Johanan, fils de Karéah.
Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
15 Quant à Ismaël, fils de Netania, il se sauva avec huit hommes devant Johanan et se rendit auprès des Ammonites.
Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
16 Puis Johanan, fils de Karéah, et tous les chefs de troupes qui l’accompagnaient prirent tout le restant de la population qu’Ismaël, fils de Netania, avait enlevée de, Miçpa, après avoir assassiné Ghedalia, fils d’Ahikam: les adultes combattants, les femmes, les enfants et les eunuques qu’ils avaient ramenés de Gabaon.
Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
17 Ils se mirent en route et firent halte dans le cantonnement de Kimham, près de Bethléem, dans l’intention de partir de là et de se rendre en Egypte,
Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
18 à cause des Chaldéens, dont ils avaient peur, parce qu’Ismaël, fils de Netania, avait mis à mort Ghedalia, fils d’Ahikam, établi comme gouverneur du pays par le roi de Babylone.
ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.

< Jérémie 41 >