< Jérémie 39 >
1 Dans la neuvième année du règne de Sédécias, roi de Juda, le dixième mois, Nabuchodonosor, roi de Babylone, marcha avec toute son armée contre Jérusalem, et ils en firent le siège.
Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
2 Dans la onzième année du règne de Sédécias, le quatrième mois et le neuf du mois, la ville fut ouverte par une brèche.
Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
3 Tous les officiers du roi de Babylone y pénétrèrent et s’installèrent à la porte centrale: Nergal-Sarécér, Samgar-Nebou, Sarsekhim, chef des eunuques, Nergal-Sarécér, chef des mages, et tous les autres officiers du roi de Babylone.
Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
4 Dès que Sédécias, roi de Juda, et tous ses gens de guerre les aperçurent, ils prirent la fuite, sortant nuitamment de la ville, à travers le parc du roi, par la porte du double rempart, et s’échappant dans la direction de la plaine.
Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
5 L’Armée chaldéenne se mit à leur poursuite; elle atteignit Sédécias dans la plaine de Jéricho, s’empara de lui et l’amena auprès de Nabuchodonosor, roi de Babylone, à Ribla, dans le district de Hamat; et celui-ci prononça sa sentence.
Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
6 Le roi de Babylone fit égorger les enfants de Sédécias, sous ses yeux, à Ribla; il fit aussi égorger tous les notables de Juda.
Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
7 Puis il fit crever les yeux à Sédécias et le chargea de chaînes pour le transporter à Babylone.
Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
8 Les Chaldéens livrèrent aux flammes le palais du roi et les maisons du peuple et démolirent les remparts de Jérusalem.
Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
9 Et le reste de la population qui était demeurée dans la ville, les transfuges qui avaient passé de son côté et le surplus de la multitude, Nebouzaradan, chef des gardes, les envoya en exil à Babylone.
Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
10 Le chef des gardes, Nebouzaradan, ne laissa dans le pays de Juda que les plus pauvres d’entre le peuple, qui étaient dénués de tout. Il leur distribua, à ce moment, des vignes et des champs.
Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
11 Or, Nabuchodonosor, roi de Babylone, avait recommandé Jérémie aux soins de Nebouzaradan, chef des gardes, dans les termes suivants:
Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
12 "Prends-le avec toi, veille sur sa personne, et ne lui fais aucun mal. Au contraire, accorde-lui tout ce qu’il te demandera."
“Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
13 Nebouzaradan, chef des gardes, Nebouchazban, chef des eunuques, Nergal-Sarécér, chef des mages, et tous les autres dignitaires du roi de Babylone envoyèrent en conséquence.
Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
14 Ils envoyèrent retirer Jérémie de la cour de la geôle et le confièrent à Ghedalia, fils d’Ahikam, fils de Chafan, pour le ramener à la maison. Il demeura ainsi parmi le peuple.
wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
15 Or, tandis que Jérémie était prisonnier dans la cour de la geôle, la parole de l’Eternel lui avait été adressée en ces termes:
Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
16 "Va dire à Ebed-Mélec, l’Ethiopien, ce qui suit: Ainsi parle l’Eternel-Cebaot, Dieu d’Israël: Je vais accomplir mes desseins sur cette ville pour son malheur et non pour son bien. Ils se réaliseront sous tes yeux, au jour dit.
“Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
17 Mais toi, je te sauverai, dit l’Eternel, ce jour-là; et tu ne seras pas livré au pouvoir des hommes que tu redoutes.
Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
18 Car je te tirerai du danger, et tu ne tomberas pas sous le glaive: ton existence sera ta part de butin, puisque tu as eu confiance en moi, dit l’Eternel."
Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”