< Isaïe 49 >
1 Iles, écoutez-moi, et vous, peuples des contrées lointaines, soyez attentifs! L’Eternel m’a désigné dès le berceau; il a énoncé mon nom dès le sein de ma mère.
Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
2 Il a rendu ma bouche semblable à un glaive tranchant et m’a abrité à l’ombre de sa main; il a fait de moi une flèche reluisante et m’a serré dans son carquois.
Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
3 Et il m’a dit: "Tu es mon serviteur; Israël, c’est par toi que je me couvre de gloire."
Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
4 Cependant moi je pensais: "En vain je me suis fatigué, c’est pour le vide et le néant que j’ai dépensé ma force." Mais non, mon droit est auprès de l’Eternel, et ma récompense auprès de mon Dieu.
Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
5 Et maintenant, s’adressant à moi, l’Eternel qui m’a créé pour être son serviteur, pour lui ramener Jacob et grouper Israël autour de lui car grand est mon prix aux yeux de l’Eternel et mon Dieu est ma force,
Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
6 l’Eternel me dit: "C’Est trop peu que tu sois mon serviteur, pour relever les tribus de Jacob et rétablir les ruines d’Israël; je veux faire de toi la lumière des nations, mon instrument de salut jusqu’aux confins de la terre."
yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
7 Ainsi parle l’Eternel, le libérateur d’Israël, son Saint, à celui qui est un objet de mépris pour les hommes, de répulsion pour les peuples, à l’esclave des puissants: "Des rois, en le voyant, se lèveront, des princes se prosterneront, par égard pour l’Eternel, qui est fidèle à ses promesses, du Saint d’Israël qui t’a élu."
Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
8 Ainsi parle l’Eternel: "À l’heure de la clémence, je t’exauce; au jour du salut, je viens à ton secours. Je veille sur toi, je fais de toi un gage d’alliance parmi les nations, pour restaurer la terre et restituer les patrimoines en ruines,
Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
9 pour dire aux prisonniers: Sortez! à ceux qui sont retenus dans les ténèbres: Paraissez au grand jour! Ils se nourriront sur les routes et trouveront une pâture sur toutes les hauteurs dénudées.
kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
10 Ils n’éprouveront ni faim ni soif; ni sécheresse ni soleil brûlant ne les feront souffrir, car Celui qui les a pris en pitié les dirigera et les mènera près des sources d’eau.
Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
11 Je transformerai toutes mes montagnes en chemins faciles, et mes routes seront rehaussées.
Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
12 Voici venir les uns de pays éloignés, voici venir les autres du Septentrion et du Couchant, d’autres arrivent du pays de Sinnîm.
Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
13 Cieux, jubilez, terre, sois dans l’allégresse, et vous, montagnes, entonnez des chants joyeux! Car Dieu console son peuple, il prend en pitié ses humbles."
Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
14 Sion avait dit: "L’Eternel m’a délaissée, le Seigneur m’a oubliée."
Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
15 Est-ce qu’une femme peut oublier son nourrisson, ne plus aimer le fruit de ses entrailles? Fût-elle capable d’oublier, moi je ne t’oublie point!
“Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
16 Oui, j’ai gravé ton nom sur la paume de mes mains, tes remparts sont constamment devant mes yeux.
Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
17 Tes enfants s’empressent d’accourir; tes destructeurs et les auteurs de ta ruine s’éloignent de toi.
Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
18 Porte tes regards à l’entour et vois: tous en masse ils te reviennent! Vrai comme je suis vivant, dit l’Eternel, tu les revêtiras tous comme une parure, tu te ceindras d’eux comme une fiancée.
Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
19 Oui, tes ruines, tes solitudes, cette terre couverte de tes décombres, elles seront trop étroites pour leurs habitants; mais tes exploiteurs auront fui loin de toi.
“Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
20 Un jour, ces enfants que tu croyais perdus, tu les entendras dire: "Je suis à l’étroit en ces lieux, fais-moi place pour que je m’établisse."
Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
21 Et tu diras en ton cœur: "Qui me les a enfantés, tous ceux-là, à moi qui étais privée d’enfants et solitaire? J’Étais proscrite et délaissée, ceux-là, qui les a élevés? J’Étais demeurée seule, ceux-là, où étaient-ils?"
Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
22 Ainsi parle le Seigneur-Eternel: "Voici, j’étendrai ma main sur les nations, et du côté des peuples je dresserai ma bannière; et ils apporteront tes fils dans leur giron, et ils chargeront tes filles sur leurs épaules.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
23 Des rois seront tes nourriciers, et leurs princesses tes nourrices; leur front jusqu’à terre se courbera devant toi, et ils baiseront la poussière de tes pieds. Et tu reconnaîtras que je suis l’Eternel, qui ne trompe jamais l’attente de ceux qui espèrent en moi."
Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
24 Quoi! Arrachera-t-on au fort son butin? La capture faite aux dépens du juste sera-t-elle reprise?
Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
25 Or, ainsi parle l’Eternel: "Oui, le butin du fort lui sera arraché; oui, la capture du tyran lui échappera! Car moi-même je serai ton champion contre tes adversaires, et je porterai secours à tes enfants.
Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
26 Et je ferai dévorer à tes persécuteurs leur propre chair, et ils s’enivreront de leur sang comme d’un vin exquis; et toute créature saura que c’est moi, l’Eternel, qui te protège, que ton libérateur est le Puissant de Jacob."
Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”