< Isaïe 34 >
1 Approchez, peuples, pour entendre, nations, soyez attentives; que la terre écoute, elle et tout ce qui la remplit, le globe avec toutes ses créatures!
Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
2 Car l’Eternel est irrité contre tous les peuples et en colère contre toutes leurs légions: il les a frappés d’anathème, voués au carnage.
Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
3 Leurs morts jonchent le sol, leurs cadavres répandent une odeur putride, leur sang fait fondre les montagnes.
Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
4 Toute la milice céleste se dissout, les cieux sont roulés comme un livre, et tous leurs astres tombent comme tombent la feuille de la vigne et le fruit desséché du figuier.
Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
5 Déjà mon glaive est ivre de sang au ciel; le voici qui s’abat sur Edom, sur le peuple que j’ai frappé d’anathème, pour faire justice.
Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
6 Le glaive du Seigneur dégoutte de sang, est luisant de graisse: c’est le sang des agneaux et des boucs, la graisse des reins des béliers; car un festin se prépare pour le Seigneur, à Boçra, de grandes hécatombes dans le pays d’Edom.
Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
7 Des buffles tombent en même temps, des taureaux et des bœufs; leur pays est inondé de sang, et la poussière de leur sol saturée de graisse.
Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
8 C’Est un jour de vengeance pour l’Eternel, une année de représailles pour la cause de Sion.
Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
9 Les rivières d’Edom se changeront en poix, sa poussière en soufre; ainsi son pays sera comme de la poix en feu,
Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
10 qui ne s’éteindra ni la nuit ni le jour, et d’où s’échapperont sans cesse des colonnes de fumée. Il demeurera en ruines de génération en génération, et, en aucun temps, nul n’y passera plus.
Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
11 C’Est le pélican et le hibou qui en prendront possession; la chouette et le corbeau en feront leur demeure. On étendra sur ce pays le cordeau de la destruction et le niveau de la ruine.
Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
12 Ses nobles il n’y en aura plus pour proclamer la royauté, et tous ses grands seront réduits à néant.
Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
13 Ses palais seront envahis par les broussailles, ses forteresses par les orties et les chardons; ils deviendront la demeure des chacals, le séjour des autruches.
Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
14 Là se rencontreront chats sauvages et chiens sauvages, là les satyres se donneront rendez-vous, là Lilit elle-même établira son gîte et trouvera une retraite tranquille.
Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
15 Là aussi nichera la vipère; elle y déposera ses œufs, les fera éclore et rassemblera les petits sous son ombre; là enfin se réuniront en troupe les vautours.
Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
16 Interrogez le livre de Dieu et lisez: nulle de ces bêtes ne fait défaut, l’absence d’aucune n’est signalée. C’Est que la bouche de l’Eternel les a convoquées, c’est ton souffle qui les a groupées.
Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
17 Lui-même a jeté le sort pour elles, et sa main leur a mesuré une part au cordeau: elles en conserveront éternellement la possession et y séjourneront de génération en génération.
Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.