< Aggée 1 >
1 Dans la deuxième année du roi Darius, le sixième mois, le premier jour du mois, la parole de l’Eternel fut adressée par l’organe du prophète Haggaï à Zorobabel, fils de Chaltiël, gouverneur de Judée, et à Josué, fils de Joçadak, le grand-prêtre, en ces termes:
Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
2 "Ainsi parle l’Eternel-Cebaot, à savoir: Ce peuple dit: Le temps n’est pas venu encore de rebâtir le temple du Seigneur!"
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
3 La parole de l’Eternel arriva par l’organe du prophète Haggaï en ces termes:
Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
4 "Le temps est-il donc venu pour vous d’habiter vos maisons lambrissées, alors que ce temple est en ruines!
“Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
5 Or, maintenant, ainsi parle l’Eternel-Cebaot: Appliquez votre attention à votre manière d’agir!
Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
6 Vous avez semé beaucoup pour récolter peu, vous mangez sans être rassasiés, vous buvez sans avoir tout votre saoûl, vous mettez des vêtements, mais ils ne vous donnent pas de chaleur, et celui qui se loue pour un salaire gagne le salaire pour une bourse trouée."
Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
7 Ainsi parle l’Eternel-Cebaot: "Appliquez votre attention à votre manière d’agir!
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
8 Montez sur la montagne, rapportez-en du bois et bâtissez le temple: j’y prendrai plaisir et je m’en trouverai honoré, dit le Seigneur.
Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
9 Vous comptiez sur une moisson abondante, et elle s’est réduite à peu de chose; quand vous l’avez rentrée dans votre maison, j’ai soufflé dessus. Pourquoi cela? dit l’Eternel-Cebaot. C’Est à cause de ma maison qui est en ruines, tandis que vous courez tous dans votre maison à vous.
“Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
10 C’Est pourquoi les cieux ont retenu leur rosée à vos dépens, et la terre a refusé ses produits.
Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
11 J’Ai appelé la sécheresse sur les champs et sur les montagnes, sur le froment, le moût et l’huile, sur tout ce que fait pousser le sol; de même sur les hommes et les bêtes, sur tous les produits du travail de vos mains."
Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
12 Zorobabel, fils de Chaltiël, Josué, fils de Joçadak, le grand-prêtre, et tout le reste du peuple écoutèrent la voix de l’Eternel, leur Dieu, et les paroles du prophète Haggaï, dont l’avait chargé l’Eternel, leur Dieu, et le peuple témoigna sa vénération au Seigneur.
Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
13 Or, Haggaï, envoyé de l’Eternel, en vertu de sa mission divine, parla au peuple en ces termes: "Je serai avec vous" dit l’Eternel.
Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
14 Et l’Eternel excita le zèle de Zorobabel, fils de Chaltiël, gouverneur de Judée, le zèle de Josué, fils de Joçadak, le grand-prêtre, et le zèle de tout le reste du peuple. Ils vinrent et se mirent à l’œuvre dans la maison de l’Eternel-Cebaot, leur Dieu.
Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
15 C’Était le vingt-quatrième jour du sixième mois, dans la deuxième année du roi Darius.
katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.