< Genèse 11 >

1 Toute la terre avait une même langue et des paroles semblables.
Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
2 Or, en émigrant de l’Orient, les hommes avaient trouvé une vallée dans le pays de Sennaar, et s’y étaient arrêtés.
Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
3 Ils se dirent l’un à l’autre: "Çà, préparons des briques et cuisons-les au feu." Et la brique leur tint lieu de pierre, et le bitume de mortier.
Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
4 Ils dirent: "Allons, bâtissons-nous une ville, et une tour dont le sommet atteigne le ciel; faisons-nous un établissement durable, pour ne pas nous disperser sur toute la face de la terre."
Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
5 Le Seigneur descendit sur la terre, pour voir la ville et la tour que bâtissaient les fils de l’homme;
Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
6 et il dit: "Voici un peuple uni, tous ayant une même langue. C’Est ainsi qu’ils ont pu commencer leur entreprise et dès lors tout ce qu’ils ont projeté leur réussirait également.
Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
7 Or çà, paraissons! Et, ici même, confondons leur langage, de sorte que l’un n’entende pas le langage de l’autre."
Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
8 Le Seigneur les dispersa donc de ce lieu sur toute la face de la terre, les hommes ayant renoncé à bâtir la ville.
Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
9 C’Est pourquoi on la nomma Babel, parce que là le Seigneur confondit le langage de tous les hommes et de là l’Éternel les dispersa sur toute la face de la terre.
Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
10 Voici les générations de Sem. Sem était âgé de cent ans lorsqu’il engendra Arphaxad, deux ans après le Déluge.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
11 Sem vécut, après avoir engendré Arphaxàd, cinq cents ans; il engendra des fils et des filles.
Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
12 Arphaxad avait vécu trente cinq ans lorsqu’il engendra Chélah.
Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
13 Arphaxad vécut, après la naissance de Chélah, quatre cent trois ans; il engendra des fils et des filles.
Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
14 Chélah, à l’âge de trente ans, engendra Héber.
Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Chélah vécut, après avoir engendré Héber, quatre cent trois ans; il engendra des fils et des filles.
Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
16 Héber, ayant vécu trente quatre ans, engendra Péleg.
Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 Après avoir engendré Péleg, Héber vécut quatre cent trente ans; il engendra dès fils et des filles.
Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
18 Péleg, âgé de trente ans, engendra Reou.
Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 Après avoir engendré Reou, Péleg vécut deux cent neuf ans; il engendra des fils et des filles.
Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
20 Reou, ayant vécu trente-deux ans, engendra Seroug.
Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
21 Après la naissance de Seroug, Reou vécut deux cent sept ans; il engendra des fils et des filles.
Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
22 Seroug, ayant vécu trente ans, engendra Nacor.
Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 Après la naissance de Nacor, Seroug vécut deux cents ans; il engendra des fils et des filles.
Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
24 Nacor, âgé de vingt-neuf ans, engendra Tharé.
Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 Nacor vécut, après avoir engendré Tharé, cent dix-neuf ans; il engendra des fils et des filles.
Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
26 Tharé, ayant vécu soixante-dix ans, engendra Abramé Nacor et Harân.
Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
27 Voici les générations de Tharé: Tharé engendra Abram, Nacor et Harân; Harân engendra Loth,
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
28 Harân mourut du vivant de Tharé son père, dans son pays natal, à Our-Kasdim.
Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
29 Abram et Nacor se marièrent. La femme d’Abram avait nom Sarai, et celle de Nacor, Milka, fille de Harân, le père de Milka et de Yiska.
Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
30 Saraï était stérile, elle n’avait point d’enfant.
Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
31 Tharé emmena Abram son fils, Loth fils de Harân son petit fils, et Saraï sa bru, épouse d’Abram son fils; ils sortirent ensemble d’OurKasdim pour se rendre au pays de Canaan, allèrent jusqu’à Harân et s’y fixèrent.
Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
32 Les jours de Tharé avaient été de deux cent cinquante ans lorsqu’il mourut à Harân.
Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.

< Genèse 11 >