< Ézéchiel 7 >
1 La parole du Seigneur me fut adressée en ces termes:
Neno la Yahwe likanijia, likisema,
2 "O toi, fils de l’homme, ainsi a parlé le Seigneur Dieu au pays d’Israël: Fin! La fin est venue pour les quatre coins du pays.
Wewe, mwanadamu-Bwana Yahwe asema hivi kwa nchi ya Israeli.”'Mwisho! Mwisho umekuja kwenye mipaka minne ya nchi.
3 Maintenant la fin est sur toi, je déchaînerai ma colère contre toi, je te jugerai selon tes voies, et ferai retomber sur toi toutes tes abominations.
Sasa mwisho uko juu yako, kwa kuwa natuma ghadhabu yangu juu yako, nitakuhukumu kulingana na njia zako; nitaleta machukizo yako yote juu yako.
4 Et mon oeil ne te prendra pas en pitié, je n’aurai pas de compassion, car je ferai retomber sur toi ta conduite, et tes abominations se manifesteront au milieu de toi, et vous saurez que je suis l’Eternel."
Kwa kuwa macho yangu hayatakuhurumia, na sitakuharibu. Badala yake, nitaleta njia zako zote juu yako, na machukizo yako yote yatakuwa katikati yako, hivyo utajua kwamba mimi ni Yahwe.
5 Ainsi a dit le Seigneur Dieu: "Un malheur, voici qu’un malheur est venu!
Bwana Yahwe asema hivi: Msiba! Msiba wa pekee! Tazama, unakuja.
6 La fin est venue, elle est venue la fin, elle s’est éveillée contre toi, voilà qu’elle est venue!
Mwisho unakuja hakika. Mwisho umeamsha dhidi yenu. Tazama! unakuja!
7 L’Aurore s’est levée sur toi, habitant du pays, le temps est arrivé; il est proche, le jour; c’est le désarroi et non les clameurs joyeuses sur les montagnes.
Kifo chako kinakuja kwako ukaaye kwenye nchi. Mda umefika; siku ya uharibifu iko karibu, na milima haitakuwa na shangwe tena.
8 Maintenant, sans retard, je déverserai mon courroux sur toi et j’épuiserai contre toi ma colère; je te jugerai selon tes voies, et te chargerai de toutes tes abominations.
Sasa baada ya mda mfupi nitamwaga dhahabu yangu juu yako na kujaza hasira yangu juu yako wakati nitakapokuhukumu kulingana na njia zako na kuleta machukizo yako yote juu yako.
9 Mon regard ne s’attendrira pas et je n’aurai pas pitié; selon tes voies je te punirai, et tes abominations se manifesteront dans ton sein, vous saurez ainsi que c’est moi l’Eternel 'qui frappe.
Kwa kuwa jicho langu halitaona kwa huruma, sitakuharibu, kama ulivyofanya, nitafanya kwako; na machukizo yako yatakuwa katikati yako hivyo utajua kwamba ni mimi Yahwe, anayekuadhibu.
10 Voici le jour! Voici qu’elle vient, qu’elle pointe, l’aurore; la verge a fleuri, l’impudence est éclose.
Tazama, siku! Tazama, inakuja! Kifo kimetoka! fimbo ya kuadhibia imechanua, kiburi kimechipua!
11 La violence se dresse en verge vengeresse de l’iniquité, rien d’eux ne reste, ni de leur richesse, ni de leur multitude, pas même de plaintes à leur sujet.
Udhalimu umekua kwenye fimbo ya udhaifu-hakuna kati yao, na hakuna katika ya kundi lao, hakuna katika utajiri wao, na hakuna wa muhimu wao atakaye baki!
12 Le temps est venu, le jour est arrivé; que l’acquéreur ne se réjouisse pas, que le vendeur ne se désole pas; car la colère éclate sur toute leur richesse.
Muda unakuja; siku imekaribia. Usimuache anayenunua shangwe, wala asihuzunike auzaye, kwa kuwa hasira yangu iko juu ya kikundi kizima!
13 Car le vendeur ne rentrera plus en possession de ce qu’il a vendu, même s’il demeure encore en vie, car il y a une vision contre tout leur avoir, elle ne sera pas révoquée, chacun a sa vie attachée à son péché; ils ne se maintiendront pas.
Kwa kuwa muuzaji hatarudia kile kilichouzwa, kadiri wanapoendelea kuishi, kwa kuwa maono yako juu yako kikundi kizima. Hawatarudi, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi kwenye dhambi atakayejitia nguvu!
14 Ils ont sonné de la trompette, on a préparé tout, et personne ne part en guerre, car ma colère est sur toute leur foule.
Wamepiga tarumbeta na kufanya kila kitu tayari, lakini hakuna mtu anayeenda kupigana; kwa kuwa hasira yangu iko juu ya kundi zima.
15 Le glaive est au dehors, et la peste et la famine à l’intérieur; ceux des champs mourront par l’épée, ceux de la ville, la famine et la peste les dévoreront.
Upanga uko nje, na tauni na njaa viko nje kwenye jengo. Wale walioko shambani watakufa kwa upanga, wakati njaa na tauni zitakapowala wale waliopo kwenye mji.
16 Et s’il en est qui sont épargnés, ils se sauveront et ils seront sur les montagnes comme les colombes des vallées, toutes gémissantes, chacun pour son péché.
Lakini watakao salia watatoroka kutoka miongoni mwao, na watakwenda kwenye milima. Kama hua wa mabondeni, wote watalia-kila mtu kwa ajili ya uovu wake.
17 Toutes les mains seront défaillantes, et tous les genoux s’en iront en eau.
Kila mkono utasita na kila goti litakuwa dhaifu kama maji, na watavaa nguo za magunia, na hofu kuu itawafunika,
18 Ils se ceindront de cilices, et l’épouvante les enveloppera, sur toutes les faces il y aura de la confusion et sur toutes leurs têtes de la calvitie.
na aibu itakuwa juu ya kila uso, na upara juu ya vichwa vyao vyote.
19 Leur argent, ils le jetteront dans les rues, et leur or sera un objet de répulsion; leur argent et leur or ne pourront les sauver au jour de la colère du Seigneur, ils ne rassasieront pas leurs corps et leurs entrailles, ils ne les rempliront pas, car leur richesse les a fait tomber dans le crime.
Watatupa fedha yao kwenye mitaa na dhahabu yao itakuwa kama jalala. Fedha yao na dhahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe. Maisha yao hayataokolewa, na njaa yao haitashiba, kwa sababu uovu wao umekuwa kizuizi.
20 De l’éclat de leur parure, ils ont fait un sujet d’orgueil, confectionné leurs idoles abominables, leurs horreurs; c’est pourquoi j’en fais pour eux un objet de répulsion.
Kwenye fahari yao walichukua kito yake nzuri za mapambo, pamoja nao wakatengeza sanamu zao za vinyago, na vitu vyao vichukizavyo. Kwa hiyo, nayabadilisha haya kuwa kitu najisi kwao.
21 Et je le donnerai en proie aux mains d’étrangers et en butin aux impies de la terre et ils le profaneront.
Kisha nitawapatia hivyo vitu kwenye mikono ya wageni kama mateka na kwa waovu wa dunia kama mateka, na watapanajisi.
22 Je détournerai d’eux ma face, et on profanera le lieu de ma retraite; des gens de rapine y pénétreront et le déshonoreront.
Kisha nitaugeuza uso wangu mbali kutoka kwao watakapo najisi mahali pangu pa siri; maharamia wataingia humo na kupanajisi.
23 Qu’on prépare les chaînes, car le pays est plein de crimes méritant la mort et la ville est pleine d’actes de violence.
Tengeneza mnyororo, kwa sababu nchi imejaa hukumu ya damu, na mji umejaa udhalimu.
24 J’Amènerai les plus méchants d’entre les nations et ils prendront possession de leurs maisons; je mettrai fin à l’orgueil des puissants et on s’emparera de leurs sanctuaires.
Hivyo nitaleta waovu wengi wa mataifa, na watamilki nyumba zao, na nitaleta mwisho kwenye fahari ya uweza, kwenda mahali pao patakatifu patanajisiwa!
25 Le frisson de la terreur survient, ils cherchent le salut, il n’en est point!
Hofu itakuja! Wataitafuta amani, lakini haitakuwepo.
26 Il arrive désastre sur désastre, et une mauvaise nouvelle suit une mauvaise nouvelle, on sollicitera une vision du prophète, et l’enseignement échappera au pontife, et la sagesse aux vieillards.
Majanga juu ya majanga yatakuja juu yangu, na kutakuwa na tetesi juu ya tetesi. Kisha watatafuta ono moja kutoka kwa nabii, lakini sheria itawaangamiza kutoka kwa kuhani na shauri kutoka kwa wazee.
27 Le roi prendra le deuil et le prince se vêtira de stupeur, et les mains du vulgaire seront prises de tremblement; je les traiterai en raison de leurs actes, je les jugerai selon leurs jugements, et ils sauront que je suis l’Eternel."
Mfalme ataomboleza na mwana wa mfalme atakata tamaa, wakati mikono ya watu wa nchi itatetemeka kwa hofu. Kulingana na njia zao wenyewe nitafanya hivi kwao! Nitawahukumu sawa sawa na wanavyostahili hadi watakapojua yakwamba mimi ni Yahwe.'”