< Ézéchiel 43 >

1 Puis, il me conduisit à la porte, à cette porte qui est disposée du côté de l’Est.
Yule mtu kisha akanileta hata kwenye lango lililokuwa linaelekea mashariki.
2 Et voici que la gloire du Dieu d’Israël s’avançait du côté de l’Est; son grondement ressemblait au bruit de grandes eaux, et la terre s’illuminait de sa gloire.
Tazama! Utukufu wa Mungu wa Israeli ukaja kutoka mashariki; sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi, na nchi iling'aa kwa utukufu wake.
3 Cette vision était pareille à la vision qui m’était apparue, à la vision que j’avais eue en venant pour la destruction de la ville; c’étaient des visions comme celle que j’avais eue sur le fleuve de Khebar, et je tombai sur ma face.
Yalikuwa yanalingana na sura ya ono nililolona, kulingana na ono nililokuwa nimeliona wakati alipokuja kuuteketeza mji, na maono yalikuwa kama maono ambayo niliyokuwa nimeyaona Keberi Kanali nikaanguka kifudi fudi.
4 La gloire de l’Eternel entra dans le temple par la porte qui est tournée du côté de l’Est.
Hivyo utukufu wa Yahwe ukaja kwenye nyumba ya karibu na njia ya lango lililokuwa wazi kwa upande wa magharibi.
5 Et l’esprit me souleva et m’amena dans le parvis intérieur, et voici que la gloire de l’Eternel remplissait le temple.
Kisha Roho akanichukua na kunileta kwenye ua wa ndanni. Tazama! Utukufu wa Yahwe ulikuwa umeijaza nyumba.
6 J’Entendis quelqu’un me parler du fond du temple, tandis que l’homme se tenait debout auprès de moi.
Mtu alisimama karibu na mimi, na nikamsikia mtu mwingine akizungumza na mimi kutoka kwenye nyumba.
7 Il me dit: "Fils de l’homme, c’est ici l’emplacement de mon trône, le lieu où se pose la plante de mes pieds, où je résiderai à jamais au milieu des enfants d’Israël. Désormais la maison d’Israël ne profanera plus mon saint nomni eux, ni leurs roispar leurs prostitutions et les cadavres de leurs rois sur leurs hauts-lieux;
Akanambia, “Mwanadamu, hapa ndipo mahali pangu pa enzi na mahali kwa ajili ya ya miguu yangu, ambapo nitaishi kati ya watu wa Israeli milele. Nyumba ya Israeli haitalikufuru tena jina langu takatifu-wao au wafalme wao katika mahali patakatifu pao.
8 car ils mettaient leur seuil près de mon seuil, leurs poteaux près de mes poteaux, avec un simple mur entre moi et eux. C’Est ainsi qu’ils profanaient mon nom par les abominations qu’ils commettaient, et que je les ai consumés dans ma colère.
Hawatalikufuru tena jina langu takatifu kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu, na nguzo yao ya lango karibu na nguzo yangu ya lango, bila kitu lakini ukuta kati yangu na wao. Wamelikufuru jina langu kwa matendo yao machafu, hivyo nimewala kwa hasira yangu.
9 A présent, ils éloigneront de moi leurs prostitutions et les cadavres de leurs rois, et je résiderai parmi eux pour toujours.
Sasa waache waondoe udanganyifu wao na maiti za wafalme wao kutoka kwangu, na nitaishi katikati yao milele.
10 Toi, fils de l’homme, décris le temple à la maison d’Israël, pour qu’ils rougissent de leurs iniquités; qu’ils en vérifient le plan!
Mwanadamu, wewe mwenyewe utaiambia nyumba ya Israeli kuhusu nyumba hii hivyo watajiskia aibu ya uovu wao. Wanaweza kutafakari kuhusu haya maelezo.
11 S’Ils rougissent de tout ce qu’ils ont fait, expose-leur et dessine devant eux le plan du temple, ses dispositions, ses issues, ses accès, toutes ses parties, ses dimensions, sa forme et son ordonnance; qu’ils en retiennent tout le plan et l’architecture, afin de les exécuter.
Kwa kuwa wameaibika kwa yote waliyoyafanya, kisha waonyeshe mchoro wa nyumba, maelezo yake, matokeo yake, maingio yake, na mchoro wake, sheria zake zote na kanuni. Kisha andika hivi chini mbele ya macho yao ili waweze kutunza michoro yote na kanuni zake zote, hivyo kama wazitiivo.
12 Voici la règle relative au temple: situé sur le sommet de la montagne, tout son circuit à l’entour est éminemment saint. Telle est la règle relative au temple.
Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba: Kutoka kwenye kilele cha mlima hata mpaka wote unaoizunguka, patakuwa patakatifu sana. Tazama! Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba.
13 Et voici les dimensions de l’autel en coudées, chaque coudée valant une coudée et une palme: la cavité est d’une coudée de profondeur, plus une coudée de largeur, le rebord qui le limite à l’entour ayant un empan pour chaque face; tel est le support de l’autel.
Hivi vitakuwa vipimo vya madhabahu katika dhiraa-hiyo dhiraa kuwa dhiraa ya kawaida na urefu wa kiganja. Hivyo mfereji ulio uzunguka madhabahu utakuwa dhiraa moja chini, na upana wake pia utakuwa dhiraa moja. Mpaka wa karibu uizungukayo machinjio shubiri moja. Hii itakuwa kitako cha madhabahu.
14 Depuis la cavité du sol jusqu’à la saillie inférieure, deux coudées; largeur, une coudée. Depuis la petite saillie jusqu’à la grande saillie, quatre coudées, sur une de largeur.
Usawa wa kutoka kwenye mferji hadi kwenye machinijo ya chini ya madhabahu itakuwa dhiraa mbili, na hiyo machinjio yenyewe itakuwa dhiraa moja upana. Kisha kutoka machinjio madogo hadi kwenye machinjio makubwa ya madhabahu, itakuwa dhiraa nne, na machinjio makubwa yatakuwa dhraa moja upana.
15 Pour le harêl, quatre coudées de hauteur, et au-dessus de l’ariêl s’élèvent les quatre cornes.
Meko juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ni dhiraa nne juu, na kuna pembe nne zilizoelekea juu kwenye meku.
16 L’Ariêl, long de douze coudées sur douze de large, forme un carré par ses quatre côtés.
Meku ina dhiraa kumi na moja urefu na dhiraa kumi na mbili upana, za mraba.
17 L’Enceinte a donc quatorze coudées de long sur quatorze de large, formant un carré par ses quatre côtés; le rebord qui le circonscrit a une demi-coudée, et la cavité intérieure une coudée en tous sens. Ses degrés sont dans la direction de l’Orient."
Mpaka wake ni dhiraa kumi na nne urefu na dhiraa kumi na nne upana pande zake zote nne, na ukingo wake ni nusu dhiraa upana. Mfereji ni dhiraa moja upana kuzuka kote pamoja na ngazi zielekeazo mashariki.”
18 Il me dit: "Fils de l’homme, ainsi parle le Seigneur Dieu: Voici quelles seront les règles de l’autel, du jour où il aura été construit: on y offrira des holocaustes et l’on y aspergera du sang.
Kisha akanambia, “Mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Hizi ndizo sheria kwa ajili ya madhabahu katika siku watakayoitengeza, kwa ajili kutoa sadaka ya kuteketezwa kwenye hiyo, na kwa jili ya kunyunyiza damu juu yake.
19 Tu donneras aux pontifesaux Lévites qui sont de la lignée de Çadokqui s’approchent de moi, dit le Seigneur Dieu, pour me servir, un jeune taureau comme expiatoire.
Utatoa ng'ombe kutoka kwenye kundi kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya Walawi makuhani ambao ni uzao wa Zadoki, wale wajao karibu nami kunitumikia-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
20 Tu prendras de son sang, que tu appliqueras aux quatre cornes, aux quatre angles de la saillie et tout autour du rebord; par là tu le purifieras et tu lui ôteras sa souillure.
Kisha utachukua baadhi ya damu yake na kuiweka juu pembe nne za madhabahu na pande nne za machinjio na kuuzunguka ukingo; utaitakasa na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 Puis tu enlèveras ce taureau expiatoire, qu’on brûlera dans la dépendance du temple désignée pour cela, en dehors du sanctuaire.
Kisha chukua ng'ombe kama sadaka ya dhambi na iteketezwe katika eneneo lililotengwa la nje ya patakatifu.
22 Le deuxième jour, tu offriras comme expiatoire un bouc sans défaut, et l’on purifiera l’autel comme on l’aura purifié par le taureau.
Kisha katika siku ya pili utatoa mbuzi dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini kama sadaka ya dhambi; makuhani wataisafisha madhabahu kama walivyoisafisha kwa ng'ombe.
23 La purification terminée, tu présenteras un jeune taureau sans défaut et un bélier sans défaut choisi dans le menu bétail.
Utakapomaliza kusafisha, toa ng'ombe asiyekuwa na dosari kutoka kwenye mifugo na kondoo dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini.
24 Tu les présenteras devant l’Eternel; les pontifes y répandront du sel et les offriront en holocauste à l’Eternel.
Watoe mbele ya Yahwe; makuhani watanyunyiza chumvi juu yao na kuwainua juu kama sadaka ya kutekezwa kwa Yahwe.
25 Sept jours durant, tu offriras chaque jour un bouc expiatoire; puis on offrira un jeune taureau et un bélier du menu bétail, on les offrira sans défaut.
Utaandaa mbuzi dume kama sadaka ya dhambi kila siku kwa mda wa siku saba, na makuhani pia wataandaa ng'ombe asiye na dosari kutoka kwenye kundi na kondoo dume kutoka kwenye kundi.
26 On mettra sept jours à faire l’expiation de l’autel, à le purifier et à l’inaugurer.
Wataipatanisha madhabahu kwa siku saba na kuitakasa, wataitakasa kwa njia hii.
27 Quand on aura épuisé cette série de jours, c’est-à-dire à partir du huitième jour, les pontifes offriront sur l’autel vos holocaustes et vos rémunératoires, et je vous serai propice, dit le Seigneur Dieu."
Watamaliza hizi siku saba, na katika siku ya nane na kuendelea itakuwa kwamba makuhani wataandaa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani kwenye madhabahu, ndipo nitakapowakubali-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ézéchiel 43 >