< Ézéchiel 40 >

1 La vingt-cinquième année de notre exil, au commence—ment de l’année, le dix du mois, quatorze ans après la ruine de la ville, en ce même jour, la main de l’Eternel se posa sur moi, et il me transporta là-bas.
Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya mji kuchukuliwa-katika siku hiyo hiyo, mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu na alinichukua huko.
2 Dans des visions divines, il me transporta au pays d’Israël et me déposa sur une très haute montagne, sur laquelle se montrait vers le Midi comme une bâtisse de ville.
Katika maono ya Mungu akanileta hata nchi ya Israeli. Akanileta kupumzika juu ya kila mlima mrefu sana; upande wa kusini kulikuwa na monekano kana kwamba majengo ya mji.
3 II m’y amena, et voici il y avait là un homme, dont l’aspect était pareil à l’aspect de l’airain, avec un cordeau de lin dans la main et une canne à mesurer. Il se tenait debout près de la porte.
Kisha akanileta huko. Tazama, kulikuwa na mtu! Mwonekano wake ulikuwa kama mwonekano wa shaba. Alikuwa na uzi wa kitani na mwanzi wa kupimia mkononi mwake, na alisimama katika lango la mji.
4 L’Homme m’adressa ces paroles: "Fils de l’homme, regarde de tes yeux, de tes oreilles écoute, et prête ton attention à tout ce que je vais te montrer; car c’est pour te faire tout voir qu’on t’a amené ici. Rapporte tout ce que tu vas voir à la maison d’Israël.
Huyo mtu akanambia, “Mwanadamu, tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako, na elekeza moyo wako juu ya yote ninayokufunulia, kwa kuwa ulinileta hapa ili niweze kukufunulia haya wewe. Toa taarifa ya kila kitu utakachokiona kwa nyumba ya Israeli.
5 Or, voici, un mur régnait à l’extérieur de l’édifice tout autour. La main de l’homme tenait une canne à mesurer de six coudées, chaque coudée augmentée d’une palme; il mesura la largeur de la construction, qui était d’une canne, et sa hauteur, également d’une canne.
Kulikuwa ukuta uliokuwa umezunguka eneo la hekalu. Urefu wa kipimo cha mwanzi katika mkono wa mtu ulikuwa dhiraa sita urefu, kila urefu wa dhiraa ulikuwa dhiraa moja na kipimo cha kiganja cha mkono urefu. Aliupima ukuta; ulikuwa kipimo cha mwanzi mmoja na ufito mmoja urefu.
6 Ensuite, il entra par une porte qui regardait vers l’Est, en monta les degrés et mesura le seuil de la porte, large d’une canne: le seuil, en lui-même, mesurait une canne en largeur.
Kisha akaenda hata kwenye lango la hekalu lililokuwa limeelekea mashariki. Akapanda ngazi na kuipima kizingiti cha lango-mwanzi mmoja upana.
7 Puis, la loge de service mesurait une longueur d’une canne et une largeur d’une canne, et entre les loges de service il y avait un intervalle de cinq coudées. Le seuil de la porte près du vestibule de la porte à l’intérieur mesurait une canne.
Vyumba vya ulinzi vilikuwa kila mwanzi mmoja urefu na mwanzi mmoja upana; kulikuwa na dhiraa tano katika kila vyumba viwili, na kizingiti cha lango la hekalu karibu na tawa la hekalu kilikuwa mwanzi mmoja urefu.
8 II mesura le vestibule de la porte, à l’intérieur; il était d’une canne.
Akapima tawa la lango; ulikuwa mwanzi mmoja urefu.
9 Il mesura le vestibule de la porte, huit coudées, et les pilastres, deux coudées: le vestibule de la porte était à l’intérieur.
Akapima tawa la lango. Ilikuwa mwanzi mmoja kwenda chini. Mihimili ilikuwa dhiraa mbili upana. Hili lilikuwa tawa la lango kuelekea hekalu.
10 Les loges de service de la porte du côté oriental étaient au nombre de trois d’un côté et de trois de l’autre côté. Toutes trois avaient même mesure, pareillement les pilastres avaient même mesure de part et d’autre.
Kulikuwa na vyumba vitatu vya ulinzi pande zote za lango la mashariki, na yote yalikuwa na kipimo kile kile, na kuta zilizokuwa zimezigawanya zilikuwa na kipimo kile kile.
11 Il mesura la largeur de la baie de la porte: dix coudées; la longueur de la porte: treize coudées.
Kisha yule mtu akapima upana wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi; na akapima urefu wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi na tatu.
12 Et devant les loges de service il y avait une barrière d’une coudée d’un côté et une barrière d’une coudée de l’autre. Quant à la loge, elle avait six coudées d’un côté et six coudées de l’autre.
Akaupima ukuta uliokuwa mpaka mbele ya vyumba-dhiraa moja urefu. Vyumba vilipimwa dhiraa sita kila upande.
13 Il mesura la porte depuis le toit d’une loge jusqu’à l’autre toit du côté opposé, vingt-cinq coudées de large, une entrée faisant face à l’autre.
Kisha akapima lango la njia kutoka kwenye paa ya chumba kimoja kuelekea chumba kingine-dhiraa ishirini na tano, kutoka lango la kuingia chumba cha kwanza kuelekea kile cha pili.
14 Il donna aux pilastres soixante coudées, et ainsi de chaque pilastre du parvis, pour chaque porte tout autour.
Kisha akapima ukuta uliokuwa umeenda kati ya vyumba vya ulinzi-dhiraa sitini urefu; alipima kwa mbali na tawa la lango.
15 Et depuis le front de la porte d’accès jusqu’au front du vestibule intérieur de la porte, cinquante coudées.
Lango la kuingia kutoka lango la mbele kuelekea lango jingine la tawa la mwisho lilikuwa dhiraa hamsini.
16 Il y avait des fenêtres grillagées aux loges de service et aux pilastres de l’intérieur de la porte tout autour; de même le vestibule avait des fenêtres à l’intérieur tout autour, et sur les piliers il y avait des palmes.
Kulikuwa na madirisha yaliyokuwa yamefungwa kuelekea vyumba na kuelekea nguzo zake kati ya malango kuzunguka kote; na vivyo hivyo kwa mabaraza. Kulikuwa na madirisha pande zote za ndani, na kila mhimili ulikuwa umepambwa kwa mitende.
17 Puis il m’amena dans le parvis extérieur: là se trouvaient des salles et un dallage disposé tout autour du parvis, trente salles donnaient sur le dallage.
Kisha huyo mtu akanileta hata ua wa nje mwa hekalu. Tazama, kulikuwa na vyumba, na kulikuwa na kibamba katika ua, pamoja na vyumba thelathini baada ya kibamba.
18 Et le dallage s’étendait du côté des portes, parallèlement à la longueur des portes: c’était le dallage inférieur.
Kibamba kilienda juu hata upande wa malango, na upana wake ulikuwa sawsawa na urefu wa malango. Hiki kilikuwa kibamba cha chini.
19 Il mesura la largeur du parvis extérieur depuis le front de la porte inférieure jusqu’au front du parvis intérieur, au dehors: cent coudées du côté de l’Est et du Nord.
Kisha huyo mtu akapima umbali kutoka mebele ya lango la chini hata mbele ya lango la ndani; ilikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki, na sawasawa na upande wa kaskazini.
20 Quant à la porte qui regardait du côté du Nord, dans le parvis extérieur, il en mesura la longueur et la largeur.
Kisha akapima urefu na upana wa lango lililokuwa upande wa kaskazini mwa ua wa nje.
21 Ses loges au nombre de trois d’un côté et de l’autre, ses pilastres et son vestibule avaient les mesures de la première porte: cinquante coudées de long et vingt-cinq coudées de large.
Kulikuwa na vyumba vitatu pande zote za lango, na lango na matawa yake yalipimwa sawa na lango kubwa-dhiraa hamsini upana wote na dhiraa ishirini na tano upana.
22 Et ses fenêtres, ses vestibules et ses palmes avaient les mêmes dimensions qu’a la porte tournée vers l’Est. On y montait par sept degrés, avec des vestibules devant eux.
Madirisha yake, tawa, vyumba, na mitende yake vilikabiliana na lango ambalo linaloelekea mashariki. Ngazi saba kuupandia juu hata kwenye tawa lake.
23 Et le parvis intérieur avait une porte faisant face à la porte du Nord comme à celle de l’Est: il mesura d’une porte à l’autre, cent coudées.
Kulikuwa na lango kwenye ua wa ndani mbele kuelekea mashariki; huyo mtu alipima kutoka lango moja hadi lango jingine-dhiraa mia moja umbali.
24 Ensuite, il me conduisit du côté du Sud, et il y avait dans la direction du Sud une porte, dont il mesura les pilastres, les vestibules ayant les dimensions précédentes.
Kisha huyo mtu akanileta hata kwenye lango la kuingia la kusini, na kuta zake na tawa vilipimwa sawa kama malango mengine ya nje.
25 Elle avait, de—même que ses vestibules, des fenêtres tout autour, pareilles aux fenêtres précédentes; elle avait cinquante coudées de long et en largeur vingt-cinq coudées.
Kulikuwa na madirisha yaliyofungwa katika lango la njia na tawa lake kama lile lango. Lango la kusini na tawa lake vilipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
26 On y montait par sept degrés, avec des vestibules devant eux; des palmes se trouvaient d’un côté et de l’autre sur ses pilastres.
Kulikuwa na ngazi saba hadi kwenye lango na matawa yake, na kulikuwa na mitende iliyochongoka juu ya kuta pande zote.
27 Et il y avait une porte conduisant au parvis intérieur dans la direction Sud: il mesura d’une porte à l’autre porte du côté du Sud, cent coudées.
Kulikuwa na lango la ua wa ndani upande wa kusini, na yule mtu akapima kutoka hilo lango hata lango la kuingia upande wa kusini-dhiraa mia moja umbali.
28 Puis il m’introduisit dans le parvis intérieur par la porte du Sud, et il mesura la porte du Sud selon les dimensions déjà indiquées.
Kishi huyo mtu akanileta hata ua wa ndani karibu na lango lake la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo vile vile kama malango mengine.
29 Ses loges, ses pilastres et son vestibule avaient également ces dimensions: elle avait, ainsi que son vestibule, des fenêtres tout autour. Sa longueur était de cinquante coudées et sa largeur de vingt-cinq coudées.
Vyumba vyake, kuta, na matao vilipimwa sawa kama malango mengine; kulikuwa na madirisha kuzunguka matao yote. Lango la ndani na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
30 Il y avait des vestibules tout autour, de vingt-cinq coudées de long et de cinq coudées de large.
Pia kulikuwa na matao pande zote za kuta za ndani; haya yalikuwa dhiraa ishirini na tano urefu na dhiraa tano upana.
31 Son vestibule donnait dans le parvis extérieur, il y avait des palmes sur ses pilastres, et il était précédé d’un escalier de huit degrés.
Hili tawa lilielekea ua wa nje pamoja na mitende iliyochongwa juu ya kuta zake na ngazi nane kuupandia.
32 Il m’introduisit dans le parvis intérieur dans la direction de l’Est et mesura la porte, qui avait les dimensions indiquées.
Kisha yule mtu akanileta hata kwenye ua wa ndani karibu na njia ya kaskazini na kulipima lango, ambalo lilikuwa na vipimo sawa kama malango mengine.
33 Ses loges, ses pilastres et son vestibule avaient également ces dimensions; elle avait, ainsi que son vestibule, des fenêtres tout autour. Sa longueur était de cinquante coudées et sa largeur de vingt-cinq coudées.
Vyumba vyake, kuta, na matawa yalikuwa na kipima sawa kama cha malango, na kulikuwa na madirisha pande zote. Laango la ndani na matawa yake yalikuwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
34 Et son vestibule donnait sur le parvis extérieur; il y avait des palmes sur ses pilastres d’un côté et de l’autre, et il était précédé d’un escalier de huit degrés.
Matawa yake yalielekea nje ya ua; ilikuwa na mitende pande zote za hiyo na ngazi nane za kuupandia.
35 Puis il me conduisit à la porte du Nord et mesura, suivant les mêmes dimensions,
Kisha huyo mtu akanileta hata lango la kaskazini na kulipima; likapimwa vivyo hivyo kama malango mengine.
36 ses loges, ses pilastres et son vestibule; elle avait des fenêtres tout autour. Sa longueur était de cinquante coudées et sa largeur de cinquante coudées.
Vyumba vyake, kuta, na ukumbi vilipimwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha pande zote. Njia ya lango na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na upana dhiraa ishirini na tano.
37 Son vestibule donnait sur le parvis extérieur; il y avait des palmes sur ses pilastres d’un côté et de l’autre, et il était précédé d’un escalier de huit degrés.
Tatawa lake lilielekea ua wa nje; ilikuwa na mitende pande zote za huo na ngazi nane kuupandia.
38 Et il y avait une salle, dont l’entrée donnait sur le vestibule de la porte orientale; là on devait laver les holocaustes.
Kulikuwa na chumba pamoja na mlango karibu na kila lango la ndani. Hapa ndipo ambako walipooshea sadaka za kutekezwa.
39 Dans le vestibule de la même porte se trouvaient deux tables d’un côté et deux tables de l’autre côté, pour y immoler les holocaustes, les sacrifices expiatoires et les délictifs.
Kulikuwa na meza mbili kila upande wa kila ukumbi, ambako sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa, na pia sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
40 Et du côté extérieur qui longe l’entrée de la porte, dans la direction du Nord, il y avait deux tables; de même du côté opposé qui longe le vestibule de la porte il y avait deux tables.
Karibu na ukuta wa ua, kuelekea juu kwenye lango kuelekea kaskazini, kulikuwa na meza mbili. Pia kwa upande mwingine kulikuwa na meza mbili kwenye lango la ukumbi.
41 Donc quatre tables d’une part et quatre tables d’autre part aux côtés de la porte: huit tables sur lesquelles on devait immoler les sacrifices.
Kulikuwa na meza nne pande zote karibu na lango; wakachinja wanyama juu ya meza nane.
42 Il y avait, en outre, quatre tables pour les sacrifices, en pierre de taille, longues d’une coudée et demie, larges d’une coudée et demie et hautes d’une coudée, où l’on devait déposer les instruments servant à immoler holocaustes et autres victimes.
Kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, dhiraa moja na nusu urefu, dhiraa moja na nusu upana, na kimo dhiraa moja. Juu yake waliweka vyombo pamoja ambavyo walivichinjia sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya sadaka.
43 Et des crochets d’une palme étaient fixés à la bâtisse tout autour, et sur les tables devait être déposée la chair des sacrifices.
Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote, na nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza.
44 En dehors de la porte intérieure étaient des salles pour les chanteurs dans le parvis intérieur, l’une longeant le côté de la porte du Nord et regardant vers le Sud, l’autre longeant le côté de la porte de l’Est et regardant vers le Nord.
Karibu na lango la ndani, katika ua wa ndani, kulikuwa na vyumba vya waimbaji. Moja ya hivi vyumba kilikuwa upande wa kaskazini, na kingine kusini.
45 II me dit: "Cette salle qui regarde vers le Sud est pour les prêtres chargés du service du temple,
Kisha yule mtu akanambia, “Hiki chumba kinachoelekea kusini ni kwa ajili ya makuhani walio zamu katika hekalu.
46 et la salle qui regarde vers le Nord est pour les prêtres chargés du service de l’autel: ce sont les fils de Çadok qui, parmi les descendants de Lévi, s’approchent de l’Eternel pour le servir."
Chumba kilichoelekea kaskazini kilikuwa kwa ajili ya makuhani waliokuwa zamu kwenye madhabahu. Hawa ni wana wa Sadoki ambaye huja humkaribia Yahwe kumtumikia; ambao ni miongoni mwa wana wa Lawi.”
47 Puis il mesura le parvis, long de cent coudées et large de cent coudées, en forme de carré; et l’autel se trouvait en avant du temple.
Kisha akaupima ule ua-dhiraa mia moja urefu na dhiraa mia moja upana mraba, pamoja na madhabahu mbele ya nyumba.
48 Puis il m’introduisit dans le vestibule du temple, et il mesura les pilastres du vestibule, cinq coudées d’un côté et cinq coudées de l’autre, et la largeur de la porte, trois coudées d’un côté et trois de l’autre.
Kisha yule mtu akanileta hata kwenye varanda ya nyumba na kupima mwimo wa milango yake-ilikuwa dhiraa tano unene upande huu. Njia ya kuingilia yenyewe ilikuwa dhiraa kumi na nne, na kuta pande zote za huo zilikuwa dhraa tatu upana.
49 La longueur du vestibule était de vingt coudées, la largeur de onze coudées, avec des degrés pour y monter; et des colonnes étaient adossées aux pilastres, l’une d’un côté et l’autre de l’autre.
Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa kumi na moja. Kulikuwa na ngazi zilizokuwa zimepanda juu na nguzo zilizokuwa zimesimama pande zote za huo.

< Ézéchiel 40 >