< Ézéchiel 24 >
1 Dans la neuvième année, le dixième jour du dixième mois, la parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 "Fils de l’homme, note-toi le nom de ce jour, du jour même où nous sommes: le roi de Babylone prend le contact de Jérusalem aujourd’hui même.
“Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
3 Imagine aussi une parabole à l’endroit de la maison de rébellion; tu leur diras: Ainsi parle le Seigneur Dieu: Pose la marmite, pose-la, et puis verses-y de l’eau.
Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
4 Rassembles-y les morceaux, rien que de bons morceaux, cuisse et épaule, remplis-la d’os excellents.
Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
5 Prends ce qu’il y a de mieux dans les agneaux, fais aussi cuire les os par dessous; qu’elle bouille à gros bouillons, pour que les os également puissent y cuire.
chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea mpaka ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
6 C’Est pourquoi, ainsi parle le Seigneur Dieu: Malheur, ô ville de sang, marmite à laquelle la crasse reste fixée, qui n’a pas été débarrassée de sa crasse! Qu’on la vide morceau par morceau, sans que le sort ait à intervenir à son sujet.
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
7 Car le sang qu’elle a versé est demeuré au milieu d’elle; elle l’a jeté sur une roche aride, elle ne l’a pas répandu sur le sol, de façon à le recouvrir de terre.
“‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
8 C’Est pour faire éclater la colère, pour en tirer vengeance que j’ai exposé son sang sur une roche aride, où il ne pouvait être recouvert.
Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
9 C’Est pourquoi, ainsi parle le Seigneur Dieu: Malheur, ô ville de sang! Moi aussi j’élèverai un grand bûcher.
“‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
10 Qu’on accumule le bois, qu’on allume le feu, qu’on consume la viande, qu’on brouille la mixture et que les os soient carbonisés!
Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya viungo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
11 Puis, qu’on la pose à vide sur ses charbons, afin qu’elle s’échauffe, que s’embrase son cuivre, que son impureté fonde au dedans et que sa crasse disparaisse.
Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
12 Elle a coûté de vains efforts, l’abondance de sa crasse n’en sort pas: au feu sa crasse!
Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
13 II y a de l’infamie dans ton impureté: puisque j’ai cherché à t’épurer et que tu n’es pas devenue pure, tu ne te débarrasseras plus de ton impureté, jusqu’à ce que j’aie assouvi ma colère sur toi.
“‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
14 Moi, le Seigneur, j’ai parlé; cela arrivera, je l’accomplirai; je ne me raviserai point, je n’aurai ni pitié ni regret. Selon tes voies et selon tes actes, on te jugera, dit le Seigneur Dieu."
“‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’”
15 La parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
Neno la Bwana likanijia kusema:
16 "Fils de l’homme, je vais t’enlever les délices de tes yeux par un coup soudain; mais tu ne te lamenteras pas, tu ne pleureras pas et tes larmes ne couleront pas.
“Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
17 Soupire en silence, ne prends pas le deuil comme pour des morts; attache sur toi ta coiffure, mets tes chaussures à tes pieds. Tu ne t’envelopperas pas jusqu’aux lèvres et tu ne mangeras pas le pain des hommes.
Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”
18 Je parlai au peuple le matin, et le soir ma femme mourut; le lendemain matin je fis comme il m’avait été ordonné.
Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.
19 Le peuple me dit: "Ne nous expliqueras-tu pas ce que signifie pour nous ta manière d’agir?"
Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
20 Je leur répondis: "La parole de l’Eternel m’a été adressée en ces termes:
Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
21 Dis à la maison d’Israël: Ainsi parle le Seigneur Dieu: Je vais profaner mon sanctuaire, votre orgueil et votre force, les délices de vos yeux, l’objet de votre amour; et vos fils et vos filles que vous avez laissés tomberont sous l’épée.
‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
22 Et vous ferez comme j’ai fait; vous ne vous envelopperez point jusqu’aux lèvres, et vous ne mangerez pas le pain des hommes.
Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
23 Votre coiffure restera sur votre tête et vos chaussures à vos pieds; vous ne vous lamenterez point et ne pleurerez point; mais vous vous consumerez par vos fautes et vous geindrez l’un en présence de l’autre.
Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
24 Et Ézéchiel vous servira de symbole: tout ce qu’il a fait, vous l’imiterez; quand cela arrivera, vous saurez que je suis le Seigneur Dieu."
Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’
25 Pour toi, fils de l’homme, certes, le jour où je leur prendrai le boulevard de leur force, la joie de leur parure, les délices de leurs yeux et l’attrait de leur âme, leurs fils et leurs filles,
“Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile,
26 ce jour-là, il viendra un fuyard auprès de toi pour l’annoncer aux oreilles de tous.
siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
27 Ce jour-là, ta bouche s’ouvrira avec celle du fuyard, tu parleras et ne seras plus réduit au mutisme; tu leur serviras de symbole, et ils sauront que je suis l’Eternel."
Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”