< Ézéchiel 18 >
1 La parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 "Qu’avez-vous à colporter le dicton suivant, sur la terre d’Israël: "Les pères ont mangé du verjus et les dents des enfants en sont agacées"?
“Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli: “‘Baba wamekula zabibu zenye chachu, nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?
3 Par ma vie, dit le Seigneur Dieu, vous ne devrez plus citer ce dicton en Israël!
“Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli.
4 Oui, toutes les âmes sont à moi; l’âme du père comme l’âme du fils, elles sont à moi: l’âme pécheresse seule mourra.
Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.
5 Un homme qui se montre vertueux, qui pratique la justice et la vertu,
“Mtu aweza kuwa ni mwenye haki atendaye yaliyo haki na sawa.
6 qui ne mange pas sur les montagnes, et ne lève pas les yeux vers les idoles de la maison d’Israël, qui ne déshonore pas la femme de son prochain et ne s’approche pas d’une femme impure
Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima wala hakuziinulia macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake, wala hakukutana kimwili na mwanamke wakati wa siku zake za hedhi.
7 qui ne fraude personne, qui restitue le gage de la dette, qui ne commet pas de vol, qui donne son pain à l’affamé et qui couvre d’un vêtement celui qui est nu,
Hamwonei mtu yeyote, bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
8 qui ne prête pas à usure et n’accepte pas de surcroît, qui écarte sa main de l’iniquité et exerce une justice loyale entre les hommes,
Hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huuzuia mkono wake usifanye mabaya, naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.
9 qui marche selon mes statuts et qui observe mes commandements pour agir avec loyauté, celui-là est un juste, il vivra à coup sûr, dit le Seigneur Dieu.
Huzifuata amri zangu na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu. Huyo mtu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana Mwenyezi.
10 Que (s’il engendre un fils violent, sanguinaire, et qui fasse à son frère une de ces choses,
“Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya
11 tandis que lui (son père) n’a rien fait de tout cela; un fils qui mange sur les montagnes et déshonore la femme de son prochain,
(ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya): “Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima. Humtia unajisi mke wa jirani yake.
12 qui exploite le pauvre et le nécessiteux, commet des vols, ne restitue pas le gage, et lève les yeux vers les idoles, fait des abominations,
Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.
13 prête à intérêt et accepte le surcroit, il vivrait? II ne vivra pas, il a commis toutes ces infamies, il faut qu’il meure, son sang sera sur lui.
Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada. Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
14 Mais s’il a engendré un fils, lequel a vu tous les péchés que son père a commis; il les a vus et n’agit pas de même.
“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
15 Il n’a pas mangé sur les montagnes, ni levé les yeux vers les idoles de la maison d’Israël, il n’a pas déshonoré la femme de son prochain.
“Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima, wala hainulii macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake.
16 Il n’a exploité personne, n’a pas retenu de gage, ni commis de vol, il a donné son pain à l’affamé et couvert d’un vêtement qui était nu.
Hakumwonea mtu yeyote wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
17 Il a retenu sa main du pauvre, il n’a pas pris d’intérêt ni de surcroît, il a observé mes préceptes et suivi mes lois, lui, il ne mourra pas pour la faute de son père, mais il vivra.
Huuzuia mkono wake usitende dhambi, hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huzishika amri zangu na kuzifuata sheria zangu. Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi.
18 Quant à son père, qui a exercé des actes d’oppression, qui a volé son frère, et n’a pas bien agi au milieu de son peuple, voici qu’il meurt pour sa faute.
Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.
19 Et vous dites: Pourquoi le fils n’a-t-il pas supporté la faute du père? C’Est que le fils a pratiqué la justice et la vertu, il a observé toutes mes lois et les a pratiquées: il vivra.
“Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi.
20 C’Est la personne qui pèche qui mourra: le fils ne portera pas la faute du père, ni le père la faute du fils; la justice du juste est imputable au juste, la méchanceté du méchant au méchant.
Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.
21 Mais si le méchant revient de toutes les fautes qu’il a commises, qu’il observe toutes mes lois, qu’il pratique le droit et la vertu, il vivra et ne mourra pas.
“Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa.
22 Aucun des péchés qu’il a commis ne lui sera compté; grâce à la justice qu’il a pratiquée, il vivra.
Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi.
23 Est-ce que je souhaite la mort du méchant, dit le Seigneur Dieu, ne préféré-je pas qu’il revienne de sa conduite et qu’il vive?
Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?
24 Et si le juste renonce à sa vertu et commet l’iniquité, et s’il fait des abominations pareilles à celles qu’a faites le méchant, vivra-t-il? On ne lui tiendra compte d’aucune des vertus qu’il a pratiquées; pour l’infidélité qu’il a commise et les péchés qu’il a fait, il mourra.
“Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.
25 Et vous dites: La voie de l’Eternel n’est pas régulière! Ecoutez donc, maison d’Israël, est-ce ma voie qui n’est pas régulière? Ne sont-ce pas vos voies qui ne sont pas régulières?
“Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?
26 Si le juste renonce à sa vertu et fait le mal, il en mourra; pour la faute qu’il a commise, il mourra.
Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa.
27 Et si le méchant revient de sa méchanceté et qu’il pratique le droit et la vertu, il sauvera sa vie.
Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake.
28 Qu’il voie et revienne de tous les péchés qu’il a commis: il vivra et ne mourra pas.
Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa.
29 La maison d’Israël dit: "La voie de l’Eternel n’est pas régulière!" Sont-ce mes voies qui ne sont pas régulières, maison d’Israël, ne sont-ce pas les vôtres?
Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”
30 C’Est pourquoi je vous jugerai chacun selon ses oeuvres, maison d’Israël, dit le Seigneur Dieu; revenez, détachez-vous de tous vos péchés, pour qu’il n’y ait plus pour vous d’occasion de faute.
“Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu.
31 Rejetez loin de vous tous les péchés que vous avez commis, faites-vous un coeur nouveau et une âme nouvelle, et pourquoi mourriez-vous, maison d’Israël?
Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli?
32 Car je ne désire pas la mort de qui meurt, dit le Seigneur Dieu, revenez et vivez!
Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!