< Daniel 2 >

1 Dans la deuxième année du règne de Nabuchodonosor, celui-ci eut des songes; son esprit en fut troublé et il perdit le sommeil.
Katika mwaka wa pili wa utawala wa Nebukadneza, alikuwa na ndoto. Akili yake ilisumbuka, na hakuweza kulala.
2 Le roi ordonna de mander devins, magiciens, sorciers et astrologues, afin qu’ils révélassent au roi ses songes. Quand ils furent venus et mis en présence du roi,
Ndipo mfalme alipowaita waganga na wale wenye kuongea na wafu. Lakini pia aliwaita wachawi na watu wenye hekima. Aliwataka wamwambie juu ya ndoto zake. Basi walikuja na kusimama mbele za mfalme.
3 celui-ci leur dit: "J’Ai eu un songe, et mon esprit est anxieux de connaître ce songe."
Mfalme akawambia, “Nilikuwa na ndoto, na akili yangu ina mashaka nataka kujua ndoto hiyo nini maana yake.”
4 Les astrologues répondirent au roi en araméen: "O roi, puisses-tu vivre éternellement! Expose le songe à tes serviteurs, et nous t’en donnerons l’explication."
Kisha watu wenye hekima wakamwambia mfalme katika Kiaramaiki, “Mfalme, aishi milele! Twambie sisi ndoto, watumishi wako, nasi tutaifunua maana yake.”
5 Le roi répliqua en disant aux astrologues: "C’Est une chose décidée par moi: si vous ne me faites pas connaître le songe et son interprétation, vous serez taillés en pièces, et vos maisons seront converties en cloaques.
Mfalme akawajibu watu wenye hekima, “Jambo hili limeshamalizika. Kama hamtaweza kuiweka wazi ndoto kwangu na kuitafsiri, miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu.
6 Si, au contraire, vous révélez le songe et sa signification, vous recevrez de moi des dons, de riches présents et de grands honneurs; donc dévoilez-moi le songe et sa signification."
Lakini kama mtaniambia ndoto na maana yake, mtapokea zawadi kutoka kwangu, thawabu, na heshima kubwa. Basi niambie ndoto na maana yake.”
7 Eux de répondre pour la seconde fois: "Que le roi, dirent-ils, expose le songe à ses serviteurs, et nous en donnerons l’explication."
Wakamjibu tena na kusema, “Mfalme na atuambie, watumishi wake, ndoto nasi tukwambia maana yake.”
8 A cela le roi répliqua: "Je sais parfaitement que vous voulez gagner du temps, parce que vous voyez que ma résolution est bien arrêtée.
Mfalme akawajibu, “Ninajua kwa hakika mnahitaji muda zaidi kwasababu mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili.
9 Si donc vous ne me faites connaître le songe, un même arrêt vous atteindra. Vous vous êtes arrangés pour m’adresser des paroles fausses et mensongères, espérant que les circonstances pourront changer; c’est pourquoi dites-moi le songe, et je saurai que vous pourrez aussi m’en fournir l’explication."
Lakini kama hamtaweza kuniambia ndoto, kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu. Mmeamua kuandaa uongo na maneno ya kudanganya ambayo mmekubaliana kwa pamoja kuniambia mpaka pale nitakapobadili akili zangu. Basi, niambieni ndoto, na kisha nitajua kuwa mnaweza kuitafsiri kwa ajili yangu.”
10 Les astrologues reprirent la parole devant le roi et dirent: "II n’est nul homme sur la terre qui soit capable de dévoiler ce que demande le roi; aussi bien, jamais roi grand et puissant n’a exigé pareille chose d’aucun devin, ni magicien, ni astrologue.
Watu wenye hekima wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu katika dunia anayeweza kutimiza matakwa ya mfalme. Hakuna mfalme yoyote mkuu na mwenye nguvu ambaye alishataka jambo kama hilo kutoka kwa wachawi, wala wenye kuongea na wafu, wala mwenye hekima.
11 La chose que demande le roi est malaisée, et il n’est personne d’autre capable de la dévoiler au roi que les dieux, qui ne séjournent pas au milieu des mortels."
Kile anachokitaka mfalme ni kigumu, na hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu, ambayo haishi miongoni mwa watu.”
12 Là-dessus, le roi s’irrita et entra dans une violente colère, et il ordonna de faire périr tous les sages de Babylone.
Jambo hili lilimfanya mfalme akasirike na kughadhabika sana, na alitoa amri kuwaangamiza wale wote waliojulikana kuwa ni wenye hekima zao katika Babeli.
13 L’Ordre fut publié et les sages allaient être mis à mort: on chercha aussi Daniel et ses compagnons pour les tuer.
Hivyo, amri ilitoka kwamba wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe. Na kwa sababu ya amri hii, walimtafuta Daniel na rafiki zake ili kwamba wauawe.
14 Alors Daniel répondit avec prudence et mesure à Arioc, chef des exécuteurs du roi, qui était sorti pour mettre à mort les sages de Babylone.
Ndipo Daniel alipomjibu kwa busara na umakini, Arioki, kamanda wa walinzi wa mfalme, ambaye alikuwa amekuja kuwaua wale wote waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
15 Il prit la parole et dit à Arioc, l’officier du roi: "Pourquoi cet édit rigoureux a-t-il été rendu par le roi?" Alors Arioc fit connaître l’affaire à Daniel.
Danieli alimwuliza kamanda wa mfalme, “Kwanini amri ya mfalme ni ya haraka hivyo?” Hivyo, Arioki akamwambia Danieli kile kilichotokea.
16 Aussitôt Daniel alla demander au roi de lui accorder un délai qui lui permît de donner l’explication au roi.
Ndipo Danieli aliingia ndani na akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme ili kwamba aweze kuwasilisha tafsiri kwa mfalme.
17 Puis, Daniel se rendit dans sa demeure et raconta la chose à ses compagnons, Hanania, Misaël et Azaria,
Kisha Danieli aliingia ndani ya nyumba na aliwaelezea Hanania, Mishaeli, na Azaria, kile kilichotokea.
18 leur demandant d’implorer la miséricorde du Dieu du ciel au sujet de ce mystère, afin que Daniel et ses compagnons ne subissent pas la mort avec les autres sages de Babylone.
Aliwasihi kutafuta rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusiana na siri hii ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa pamoja na watu wengine waliosalia waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
19 Alors le mystère fut dévoilé à Daniel dans une vision nocturne, et Daniel bénit le Dieu du ciel.
Usiku ule siri ilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Kisha Danieli akamtukuza Mungu wa mbinguni
20 Daniel prit la parole et dit: "Que le nom de Dieu soit béni d’éternité en éternité! Car à lui appartiennent la sagesse et la puissance.
na kusema, “Litukuzwa jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na nguvu ni zake.
21 C’Est lui qui modifie les temps et les époques, qui tour à tour renverse les rois et élève les rois, qui donne la sagesse aux sages et la science à ceux qui savent comprendre.
Anabadili wakati na majira; anaondoa wafalme na kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi. Anawapa hekima wenye hekima na ufahamu kwa wenye weledi.
22 C’Est lui qui révèle les choses profondes et cachées; il connaît ce que recèlent les ténèbres, et la lumière réside avec lui.
Hufunua vitu vya chini na vilifichika kwa sababu anajua kile kilicho gizani, naye anaishi pamoja na mwanga.
23 C’Est toi, Dieu de mes pères, que je remercie et exalte pour m’avoir donné sagesse et force; et à l’heure présente, tu m’as fait connaître ce que nous t’avons demandé: ce qui préoccupe le roi, tu nous l’as fait connaître."
Mungu wa baba zetu, ninakushukuru na kukutukuza wewe kwa ajili ya hekima na nguvu uliyonipa. Sasa umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba; umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme.”
24 Sur cela, Daniel se rendit auprès d’Arioc, que le roi avait chargé d’exécuter les sages de Babylone; il alla et lui parla de la sorte: "Ne fais point mourir les sages de Babylone: introduis-moi auprès du roi, et je révélerai au roi l’interprétation de son songe."
Ndipo Danieli alienda kumwona Arioki ( yule ambaye mfalme alimchagua kuua kila mtu aliyekuwa na hekima katika Babeli). Alimwendea na kumwambia, “Usiwauwe watu wenye hekima katika Babeli. Nipeleke kwa mfalme na nitamwonesha mfalme tafsiri ya ndoto yake.”
25 Aussitôt Arioc, en toute hâte, introduisit Daniel auprès du roi et lui dit: "J’Ai trouvé un homme parmi les exilés de Juda, qui fera connaître au roi l’interprétation de son songe."
Kisha Arioki kwa haraka alimleta Danieli mbele za mfalme na kusema, “Nimempata miongoni wa watu wa mateka wa Yuda mtu ambaye atafunua maana ya ndoto ya mfalme.”
26 Le roi prit la parole et dit à Daniel, qui portait le nom de Beltchaçar: "Est-il vrai que tu sois capable de me faire connaître le songe que j’ai eu et son explication?"
Mfalme akamwambia Danieli (ambaye alikuwa akiitwa Beliteshaza), “Je unaweza kunimbia ndoto niliyoiona na maana yake?”
27 Daniel répliqua au roi: "Le mystère, dit-il, que veut éclaircir le roi, ni sages, ni devins, ni magiciens, ni astrologues ne peuvent le révéler au roi.
Danieli alimjibu mfalme na kusema, “Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota.
28 Mais il est un Dieu au ciel, qui dévoile les secrets; c’est lui qui a révélé au roi ce qui arrivera dans la suite des temps. Ton songe et les visions qui ont frappé ton esprit sur ta couche, les voici:
Isipokuwa kuna Mungu ambaye anaishi mbinguni, ambaye hufunua siri, na amekwisha kukujulisha wewe, mfalme Nebukadneza, kile kitakachotokea katika siku zijazo. Hizi ndizo Ndoto na maono ya akili zako uliyoyaona wakati ulipokuwa umelala kitandani mwako.
29 O roi, il a surgi en toi, sur ta couche, des pensées touchant ce qui arrivera dans la suite, et celui qui révèle les mystères t’a annoncé ce qui sera.
Na kwako Wewe, mfalme, mawazo yako kitandani mwako yalikuwa ni juu ya mambo yajayo, na yule afichuaye siri ameifanya ijulikane kwako kuhusu kile kilicho karibu kutokea.
30 Quant à moi, si ce mystère m’a été découvert, ce n’est pas que je possède une sagesse refusée à tous les vivants; mais c’est aux seules fins qu’on en apprenne la signification au roi, et que tu connaisses les pensées de ton cœur.
Na kuhusu mimi, siri hii haikufunuliwa kwangu kwa sababu ya hekima yoyote niliyo nayo zaidi ya mtu yoyote anayeishi. Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe, mfalme, uweze kufahamu maana, na ili kwamba ujuwe mawazo yaliyo ndani mwako.
31 Toi, ô roi, tu regardais, et voilà qu’une formidable statue se dressait devant toi: cette statue était grande, d’un éclat extraordinaire et d’un aspect effrayant.
Mfalme, uliangalia juu na ukaona sanamu kubwa. Sanamu hii ambayo ilikuwa yenye nguvu na yenye kung'aa, ilisimama mbele yako. Mng'ao wake ulikuwa unatisha.
32 Cette statue avait la tête d’or fin, la poitrine et les bras d’argent, le ventre et les cuisses d’airain,
Kichwa cha sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi. Matiti yake na mikono ilikuwa ya fedha. Sehemu ya katikati na mapaja yake yalikuwa yametengenezwa kwa shaba,
33 les jambes de fer et les pieds en partie de fer et en partie d’argile.
na miguu yake ilikuwa imetengenezwa kwa chuma. Miguu yake ilikuwa ilitengenezwa kwa sehemu chuma na sehemu kwa udongo.
34 Tu la regardais, quand une pierre, se détachant, sans l’intervention d’aucune main, vint frapper les pieds qui étaient de fer et d’argile et les broya.
Ulitazama juu, na jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na liliipiga sanamu katika miguu yake ya chuma na udongo, na ponda ponda.
35 Alors, du même coup, furent broyés le fer, l’argile, l’argent et l’or; ils devinrent comme la balle qui s’envole des aires de blé, et furent emportés par le vent, sans qu’il en restât aucun vestige; mais la pierre qui avait frappé la statue se changea en une grande montagne et remplit toute la terre.
Kisha chuma, udongo, fedha, na dhahabu zilivunjwa katika vipande vipande kwa wakati mmoja na yakawa kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi. Upepo huyapeperushia mbali na hakuna alama inayoachwa. Lakini jiwe lililoipiga sanammu likawa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.
36 Tel était le songe; et ce qu’il signifie, nous allons le dire au roi:
Hii ndiyo ilikuwa ndotoyako. Na sasa tutamwambia mfalme maana yake.
37 Toi, ô roi, le roi des rois, à qui le Dieu du ciel a donné royauté et force, puissance et gloire;
Wewe, mfalme, ni mfalme wa wafalme kwa wale ambao Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, nguvu, uweza na heshima.
38 toi, aux mains de qui il a livré tout ce qui habite sur la terre, les hommes, les bêtes des champs et les oiseaux du ciel, et qu’il a rendu maître de toutes choses, tu es la tête d’or.
Amevitia mkononi mwako sehemu ambazo binadamu huishi. Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako, na amekufanya wewe utawale juu yao wote. Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu.
39 Après toi, s’élèvera un autre empire, inférieur au tien; puis un troisième empire, qui sera d’airain et qui dominera sur toute la terre,
Baada yako, ufalme mwingine utainuka ambao ni mdogo kwako, na hata ufalme wa tatu wa shaba utatawala juu ya dunia yote.
40 puis viendra un quatrième empire, puissant comme le fer; puisque le fer broie et écrase tout, cet empire, pareil au fer qui brise tout le reste, ne fera qu’écraser et causer des ruines.
Kutakuwa na ufalme wa tatu, wenye nguvu kama chuma, kwa kuwa chuma huvunja vipande vipande vitu vingine na kuponda ponda kila kitu. Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.
41 Et si tu as vu que tes pieds et les orteils étaient partie en argile de potier et partie en fer, c’est que ce sera un empire divisé; toutefois il aura en lui quelque chose de la solidité du fer, en raison de ce que tu as vu du fer mêlé avec de l’argile boueuse.
Kama vile ulivyoona, miguu na vidole vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma, hivyo utakuwa ni ufalme uliogawanyika; baadhi ya nguvu za chuma zitakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona kuwa chuma kimechanganyikana na udongo laini.
42 Les orteils des pieds étaient partie de fer et partie d’argile: c’est que cet empire sera en partie fort et en partie fragile.
Kama vile vidole vya miguuni vilivyokuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa chuma na kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo, ndivyo ufalme utakuwa kwa sehemu una nguvu na kwa sehemu utakuwa dhaifu.
43 Et si tu as vu le fer mêlé avec de l’argile boueuse, c’est que ces deux parties se mêleront par des alliances humaines, mais sans qu’elles s’attachent solidement l’une à l’autre, pas plus que le fer ne s’amalgame avec l’argile.
Kama ulivyoona chuma kimechanganywa na udongo laini, na hivyo na watu watakuwa wamechanganyikana; hawakaa kwa pamoja, kama vile chuma kisivyoweza kushikamana na udongo
44 Et du temps de ces rois-là, le Dieu du ciel suscitera un empire qui ne sera jamais détruit, un empire qui ne cédera la place à aucun autre peuple: il écrasera et anéantira tous les autres empires et subsistera lui-même éternellement,
Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine. Utazivunja falme zingine vipande vipande na kuzikomesha zote, nao utadumu milele.
45 tout comme tu as vu que de la montagne s’est détachée une pierre, sans l’intervention d’aucune main, et qu’elle a broyé le fer, l’airain, l’argile, l’argent et l’or. Un grand Dieu a révélé au roi ce qui arrivera dans la suite: certain est le songe et digne de foi son interprétation!"
Kama tu ulivyoona, jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu. Lilivunja vunja chuma, shaba, udongo, fedha, na dhahabu katika vipande vipande. Mungu mkuu amekujulisha wewe, mfalme, kile kitakachotokea baada ya haya. Ndoto ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.
46 Alors le roi Nabuchodonosor se prosterna contre terre, puis s’agenouilla devant Daniel et ordonna de lui présenter des offrandes et des parfums.
Mfalme Nebukadneza alianguka kifudifudi mbele ya Daniel na alimweshimu; aliamuru kwamba sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake.
47 S’Adressant ensuite à Daniel, le roi lui dit: "En vérité, votre Dieu est le Dieu des dieux, le souverain des rois, le révélateur des mystères, puisque tu as pu dévoiler ce mystère-là."
Mfalme alimwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme, na ambaye hufunua mafumbo, kwa kuwa umekuwa ukiweza kufumbua mafumbo haya.”
48 Alors le roi rendit de grands honneurs à Daniel, le combla de nombreux et riches présents, et l’institua gouverneur de toute la province de Babylone et chef suprême de tous les sages de Babylone.
Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu watu wenye hekima wa Babeli.
49 Et Daniel en ayant fait la demande au roi, celui-ci préposa Chadrac, Mêchac, et Abêd-Nego aux affaires de la province de Babylone, tandis que Daniel restait à la cour du roi.
Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.

< Daniel 2 >