< Amos 6 >

1 Malheur à vous, qui vous croyez en sécurité à Sion, et à vous, si pleins de quiétude sur le mont de Samarie, qui formez l’élite de la première des nations et attirez à vous la maison d’Israël!
Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
2 Passez donc à Calné et regardez; de là, rendez-vous à Hamath-la-Grande, puis descendez à Gath au pays des Philistins: sont-ils plus prospères que ces royaumes-ci, leur territoire est-il plus considérable que le vôtre?
Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
3 Vous vous imaginez reculer le jour du malheur et vous avancez le règne de la violence!
Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
4 Couchés sur des lits d’ivoire, étendus sur leurs divans, nourris d’agneaux choisis dans le troupeau, de veaux mis à l’engrais,
Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
5 fredonnant au son du luth, comme David inventant à leur usage des instruments de musique,
Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
6 ils boivent du vin à même les amphores, se frottent d’huiles de choix et ne s’affligent guère du désastre de Joseph!
Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
7 C’Est pourquoi, tantôt, ils s’en iront en tête des déportés; alors c’en sera fini des chants bruyants de ces voluptueux.
Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
8 "Le Seigneur a juré par lui-même, c’est la parole de l’Eternel Dieu-Cebaot: Je déteste l’orgueil de Jacob, je hais ses palais, je livrerai donc en proie la ville et ce qu’elle renferme.
Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
9 Que s’il reste dix hommes dans une maison, ils mourront.
Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
10 Et quand le proche parent, chargé de l’incinération, emportera le corps afin de débarrasser la maison des ossements, il demandera à celui qui se trouve au fond de l’appartement: "Y a-t-il encore quelqu’un?", et l’autre répondra: "Non, personne!" et ajoutera: "Silence!" car ce ne sera pas le moment de prononcer le nom de l’Eternel."
Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
11 En vérité, l’Eternel donne des ordres: il fera tomber en ruines les grandes maisons et mettra en morceaux les petites.
Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
12 Est-ce que les chevaux courent sur le roc? Le laboure-t-on avec des bœufs? Mais vous, vous avez changé le bon droit en poison, et l’œuvre de la justice en plante vénéneuse.
Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
13 Vous trouvez votre joie dans ce qui est néant, vous dites: "N’Est-ce pas grâce à notre énergie que nous avons conquis la puissance?"
ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
14 Eh bien! Me voici, suscitant contre vous, maison d’Israël, dit l’Eternel, Dieu-Cebaot, un peuple qui vous serrera de près dès la région de Hamath jusqu’au torrent de la Plaine.
Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”

< Amos 6 >