< 2 Chroniques 28 >

1 Achaz avait vingt ans à son avènement et il régna seize ans à Jérusalem; il ne fit pas ce qui est droit aux yeux de l’Eternel comme David, son aïeul.
Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, na akatawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Hakufanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe, kama Daudi babu yake alivyokuwa amefanya.
2 Au contraire, il suivit l’exemple des rois d’Israël et fit même des idoles de fonte en l’honneur des Bealim.
Badala yake, alitembea katika njia za wafalme wa Israeli; pia alitengeneza sanamu za kusubu kwa ajila ya Mabaali.
3 Il offrit de l’encens dans la vallée de Ben-Hinnom, fit brûler ses fils dans le feu, imitant les abominations des peuples que l’Eternel avait dépossédés au profit des enfants d’Israël.
Zaidi ya hayo, akafukiza uvumba katika bonde la Beni Hinomu na akawaweka watoto wake ndani ya moto, kwa mjibu wa desturi za uzinzi za watu ambao Yahwe aliwafukuza nje ya nchi zao mbele za watu wa Israeli.
4 Il offrit des sacrifices et de l’encens sur les hauts lieux et les collines et sous tous les arbres verdoyants.
Akatoa sadaka na kufukiza uvumba katika sehemu za juu na juu ya vilima na chini ya kila mti wenye majani mabichi.
5 Alors l’Eternel, son Dieu, le livra au pouvoir du roi des Syriens, qui le battirent, lui prirent un grand nombre de captifs, qu’ils emmenèrent à Damas. Il fut livré aussi au roi d’Israël, qui lui infligea une grande défaite.
Kwa hiyo Yahwe Mungu wa Ahazi, akamweka katika mikono ya mfalme wa Shamu. Waaramu wakamshinda na kuchukua kutoka kwake kundi kubwa la mateka, wakawapeleka Damesiki. Ahazi pia aliwekwa katika mikono ya mfalme wa Israeli ambaye alimshinda kwa mauji makuu.
6 Pékah, fils de Remaliahou, tua en Juda cent vingt mille hommes en un jour, tous de vaillants guerriers, parce qu’ils avaient abandonné l’Eternel, le Dieu de leurs pères.
Kwa maana Peka mwana wa Remalia, aliwaua katika Yuda wanajeshi 120, 00 kwa siku moja, wote walikuwa wanaume hodari, kwa maana walikuwa wamemsahau Yahwe, Mungu wa babu zao.
7 Zikhri, un guerrier d’Ephraïm, tua Maassêyahou, fils du roi, Azrikam, intendant du palais, et Elkana, le vice-roi.
Zikri, mtu mwenye nguvu kutoka Efraimu, akawaua Maaseya mwana wa mfalme, Azrikamu, mwangalizi mkuu wa ikulu, na Elkana, ambaye alikuwa karibu na mfalme.
8 Les enfants d’Israël capturèrent d’entre leurs frères deux cent mille âmes, femmes, fils et filles et ils leur prirent, en outre, un butin abondant, qu’ils emportèrent à Samarie.
Jeshsi la Israeli likachukua mateka kutoka kwa ndugu zao 200, 000 wake, wana, na mabinti. Pia wakachukua nyara nyingi, ambazo walipeleka Samaria.
9 Là se trouvait un prophète de l’Eternel, nommé Oded. Il sortit à la rencontre de l’armée revenant à Samarie et leur dit: "Voyez! C’Est dans sa colère contre Juda que l’Eternel, Dieu de vos pères, les a livrés entre vos mains; mais vous en avez fait un carnage féroce qui s’est amoncelé jusqu’au ciel.
Lakini nabii wa Yahwe alikuwapo huko, jina lake aliitwa Odedi. Alikwenda nje kukutana na jeshi likiingia Samaria. Akawaambia, “Kwa sababu Yahwe, Mungu wa babu zenu, alikuwa na hasiri na Yuda, akawatia katika mikono yenu. Lakini mmewaua katika hasira inayofika juu mbinguni.
10 Et maintenant, ces enfants de Juda et de Jérusalem, vous parlez de les réduire à la condition d’esclaves et de servantes. N’Est-ce pas vous rendre coupables vous-mêmes à l’égard de l’Eternel, votre Dieu?
Sasa ninyi badala ya kuwahifadhi wanaume na wanawake wa Yuda na Yerusalemu kama watumwa wenu. Lakini je hamko na hatia ya dhambi zenu zidi ya Yahwe Mungu wenu?
11 Or donc, écoutez-moi et restituez ces captifs que vous avez faits d’entre vos frères, car la colère de l’Eternel s’enflamme contre vous."
Sasa basi, nisikilizeni: warudisheni wafubgwa, ambao mmewachukua wa ndugu zenu, kwa maana ghadhabu ya Yahwe iko juu yenu.”
12 Alors quelques hommes d’entre les chefs des Ephraïmites, Azariahou, fils de Yehohanan, Bérékhiahou, fils de Mechillêmôt, Yéhizkiyahou, fils de Challoum, et Amassa, fils de Hadlaï, s’élevèrent contre ceux qui revenaient de l’expédition.
Kisha baadhi ya viongozi wa watu wa Efraimu—Azaria mwana wa Yohanani, Berekia mwana wa Meshiremothi, na Yehizikia mwana wa Shalumu, na Amasa mwana wa Hadlai, wakasimama kinyume na wale waliorudi kutoka vitani.
13 Ils leur dirent: "N’Amenez pas ces captifs ici, ce serait nous charger d’un crime envers l’Eternel: vous voudriez ajouter à nos péchés et à notre crime; notre faute est déjà grande et le courroux divin s’est enflammé contre Israël."
Wakasema kwao, “Lazimaa msiwaleta wafungwa hapa, kwa kuwa mlikusudia jambo ambalo litaleta juu yetu dhambi dhidi ya Yahwe, kuongeza dhambi juu yetu na makosa yetu, kwa maana makosa yetu ni makuu, na kuna hasira kali dhidi ya Israeli.”
14 Alors l’armée abandonna la capture et le butin aux chefs et à toute la foule.
Hivyo watu wenye silaha wakawaacha wafungwa na mateka mbele ya viongozi wa Israeli na kusanyiko lote
15 Les hommes désignés nominativement se levèrent, se saisirent des captifs; tous ceux qui étaient nus, ils les vêtirent d’habits pris du butin, les habillèrent, les chaussèrent, leur donnèrent à manger et à boire, les frictionnèrent, conduisirent à âne tous ceux qui trébuchaient, les menèrent à Jéricho, la ville des palmiers, auprès de leurs frères et revinrent à Samarie.
Watu ambao walipangwa kwa majina wakanyanyuka na kuwachukua wafungwa, na kuwavika wote waliokuwa uchi miongoni mwa mateka. Wakawavika na kuwapa viatu. Wakawapa chakula wale na kunywa. Wakawahudumia majeraha yao na kuwaweka waliodhaifu juu ya punda. Wakawarudisha kwenye familia zao katika Yeriko, (Ulioitwa mji wa mitende). Kisha wakarudi Samaria.
16 En ce temps-là, le roi Achaz envoya demander aux rois d’Assyrie de lui venir en aide.
Wakati huo Mfalme Ahazi akatuma wajumbe kwa wafalme wa Ashuru kuwaomba wamsaidie.
17 Des Iduméens vinrent aussi, remportèrent une victoire en Juda et emmenèrent des prisonniers.
Kwa maana Waedomu walikuwa wamekuja tena na kuvamia Yuda, wakachukua wafungwa.
18 De plus, des Philistins envahirent les villes de la Basse-Terre et du Sud de Juda, conquirent Beth-Chémech, Ayyalôn, Ghedèrôt, Sokho avec ses dépendances, Timna avec ses dépendances et Ghimzo avec ses dépendances, et s’y établirent.
Wafilisti pia wakavamia miji ya nchi ya chini na ya Negebu ya Yuda. Waliichukua Beth-shemeshi, Ayaloni, Giderothi, SoKo pamoja na vijiji vyake, Timna pamoja na vijiji vyake. Wakaenda kuishi katika sehemu hizo.
19 Car l’Eternel avait humilié Juda à cause d’Achaz, roi d’Israël, qui s’était déréglé en Juda et montré rebelle à l’Eternel.
Kwa kuwa Yahwe aliishusha chini Yuda kwa sababu ya Ahazi, mfalme wa Israeli; kwa maana alikuwa ametenda maovu katika Yuda na alikuwa ametenda dhambi nzito sana dhidi ya Yahwe.
20 Tilgat-Pilneécer, roi d’Assyrie, marcha contre lui et l’assiégea au lieu de l’assister.
Tiglath-pileseri, mfalme wa Ashuru, akaja kwake na akampa tabu badala ya kumpa nguvu.
21 Car Achaz avait dépouillé la maison de l’Eternel, le palais du roi et les chefs pour tout donner au roi d’Assyrie, mais cela ne lui servit de rien.
Kwa kuwa Ahazi aliteka nyara nyumba ya Yahwe na nyumba ya mfalme na viongozi, kwa ajili ya kuvitoa vitu vya thamani kwa mfalme wa Ashuru. Lakini kufanya hivyo hakukumfaidisha yeye.
22 Et dans le temps de sa détresse, il continua ses infidélités à l’Eternel, lui, le roi Achaz.
Mfalme Ahazi huyu huyu akatenda dhambi hata zaidi dhidi ya Yahwe katika muda wa mateso yake.
23 Il sacrifia aux dieux de Damas qui l’avaient battu et dit: "Ce sont les dieux des rois de Syrie qui les ont secourus, je vais leur sacrifier et ils me secourront." Mais ce furent eux qui causèrent sa chute et celle de tout Israël.
Kwa maana aliwatolea dhabihu mingu wa Dameski, miungu ambao walimshinda. Akasema, “Kwa sababu miungu wa mfalme wa Aramu waliwasaidia, nitawatolea sadaka ili wanisaidie.” Lakini walikuwa watesi wake na Israeli yote.
24 Achaz réunit les vases du temple de Dieu et les brisa. Il ferma les portes du temple de l’Eternel et se fit des autels dans tous les coins de Jérusalem.
Ahazi akazikusanya pamoja samani za nyumba ya Mungu na kuzikata vipande vipande. Akaifunga milango ya nyumba ya Yahwe na kuzitengeneza madhabahu kwa ajili yake mwenyewe katika kila kona ya Yerusalemu.
25 Et dans chaque ville de Juda il érigea des hauts lieux pour encenser les dieux étrangers, irritant ainsi l’Eternel, le Dieu de ses pères.
Katika kila mji wa Yuda akafanya sehemu za juu kwa ajili ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa miungu wengine. Akamfanya Yahwe, Mungu wa babu zake, akasirike.
26 Le reste de ses faits et gestes et toutes ses actions, des premières aux dernières, se trouvent consignés dans le livre des Rois de Juda et d’Israël.
Sasa matendo yake yaliyobaki, na njia zake zote, mwanzo na mwisho, ona, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
27 Achaz s’endormit avec ses pères et fut enterré dans la ville, à Jérusalem, car on ne le plaça point dans le sépulcre des rois d’Israël. Son fils Ezéchias lui succéda.
Ahazi akalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji, katika Yerusalemu, lakini hawakumleta kwenye makaburi ya wafalme wa Israeli. Hezekia, mwanaye, akawa mfamle katika nafasi yake.

< 2 Chroniques 28 >