< 2 Chroniques 26 >

1 Tout le peuple de Juda prit Ouzzia, alors âgé de seize ans, et le proclama roi à la place de son père Amacia.
Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
2 Il rebâtit Elot et la restitua à Juda, après que le roi se fut endormi avec ses aïeux.
Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
3 Agé de seize ans à son avènement, Ouzzia régna cinquante-deux ans à Jérusalem. Le nom de sa mère était Yekholia, de Jérusalem.
Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
4 Il fit ce qui est droit aux yeux de l’Eternel, suivant en tout l’exemple de son père Amacia.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
5 Il s’appliqua à rechercher Dieu tant que vécut Zekhariahou, qui savait inspirer la crainte de Dieu. Et tant qu’il recherchait le Seigneur, Dieu lui donnait le succès.
Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
6 Il entra en campagne pour combattre les Philistins, renversa les remparts de Gath, de Jabné, d’Asdod, et fortifia des villes dans le territoire d’Asdod et d’autres régions des Philistins.
Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
7 Dieu l’assista contre les Philistins, les Arabes établis à Gour-Baal, et les Meounites.
Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
8 Les Ammonites aussi offrirent des présents à Ouzzia. Sa renommée se répandit jusqu’au territoire d’Egypte, car il acquit une extrême puissance.
Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
9 Ouzzia bâtit des tours à Jérusalem, sur la porte de l’Angle, sur la porte de la Vallée et sur l’Encoignure, et les rendit très fortes.
Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
10 Il bâtit aussi des tours dans le désert, fit creuser de nombreuses citernes, car il avait un nombreux bétail dans les terres basses et dans la plaine, des laboureurs et des vignerons dans les montagnes et les champs fertiles, ayant beaucoup de goût pour l’agriculture.
Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
11 Ouzzia eut une armée de gens de guerre allant en campagne par bandes selon le contingent fixé par les soins de Yeïêl, le secrétaire, et Maassêyahou, le préfet, sous la direction de Hananiahou, l’un des lieutenants royaux.
Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
12 Le nombre des chefs de famille parmi ces guerriers était en tout de deux mille six cents.
Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
13 Sous leur direction il y avait une armée active de trois cent sept mille cinq cents combattants, vaillants guerriers pour aider le roi contre l’ennemi.
Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
14 Ouzzia leur fit préparer, à toute l’armée, des boucliers, des lances, des casques, des cuirasses, des carquois et les pierres de fronde.
Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
15 Il fit aussi fabriquer à Jérusalem des engins imaginés par un ingénieur, qui devaient être placés sur les tours et les angles, et lancer des traits et de grosses pierres; aussi sa renommée s’étendit-elle au loin, car il se fit seconder à merveille jusqu’à devenir puissant.
Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
16 Mais dans la puissance, son cœur s’enorgueillit jusqu’au crime; il fut rebelle contre l’Eternel, son Dieu, et pénétra dans le sanctuaire de l’Eternel, pour faire des fumigations sur l’autel des parfums.
Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
17 Azariahou, le prêtre, entra derrière lui, accompagné des prêtres de l’Eternel, au nombre de quatre-vingts hommes courageux,
Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
18 qui s’opposèrent au roi Ouzzia et lui dirent: "Ce n’est pas ton rôle, Ouzzia, d’offrir l’encens à l’Eternel; c’est celui des prêtres, des descendants d’Aaron, consacrés à ce soin; sors du sanctuaire, car tu as péché, et cela ne te fait point honneur devant l’Eternel Dieu.
Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
19 Ouzzia se mit en colère, tandis qu’il tenait en main l’encensoir à fumigation, et alors qu’il s’emportait contre les prêtres, la lèpre brilla sur son front, en présence des prêtres, dans le temple de l’Eternel, auprès de l’autel des parfums.
Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
20 Azariahou, le prêtre en chef, se tourna vers lui ainsi que tous les prêtres, et voici qu’il était atteint de lèpre au front. Ils le firent sortir en hâte du lieu, et lui-même, d’ailleurs, s’empressa de sortir, car l’Eternel l’avait frappé.
Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
21 Le roi Ouzzia resta atteint de lèpre jusqu’au jour de sa mort et demeura lépreux dans une maison d’isolement, car il avait été retranché du temple de l’Eternel. Jotham, son fils, préposé au palais du roi, gouvernait les gens du pays.
Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
22 Le reste de l’histoire d’Ouzzia, du commencement à la fin, a été écrit par Isaïe, fils d’Amoç, le prophète.
Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
23 Ouzzia s’endormit avec ses aïeux, et il fut enterré avec eux dans le champ de la sépulture des rois, car on allégua qu’il était lépreux. Son fils Jotham lui succéda.
Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chroniques 26 >