< 2 Chroniques 19 >

1 Josaphat, roi de Juda, retourna sain et sauf chez lui, à Jérusalem.
Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
2 Jéhu, fils de Hanani, le Voyant, alla à sa rencontre et dit au roi Josaphat: "Devais-tu prêter ton concours à cet impie? Sont-ce les ennemis du Seigneur que tu aimes? Par là, tu as provoqué contre toi la colère de l’Eternel.
Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
3 Toutefois, des mérites réels se trouvent en toi, puisque tu as fait disparaître les Achêrot de ce pays, et que tu t’es appliqué, de cœur, à rechercher l’Eternel."
Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
4 Josaphat, après s’être réinstallé à Jérusalem, se remit à visiter les populations depuis Bersabée jusqu’aux monts d’Ephraïm et les ramena à l’Eternel, Dieu de leurs ancêtres.
Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
5 Il institua des juges dans le pays, dans chacune des villes fortes de Juda,
Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
6 et dit à ces juges: "Soyez attentifs à ce que vous faites! Ce n’est pas au nom d’un homme que vous rendez justice, mais au nom de l’Eternel: Il est présent quand vous prononcez un jugement.
Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
7 Puisse donc la crainte du Seigneur vous inspirer! Soyez circonspects dans vos actes, car l’Eternel, notre Dieu, n’admet ni iniquité, ni acception de personnes, ni corruption par les présents."
Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
8 A Jérusalem également, Josaphat choisit des Lévites, des prêtres et des chefs de famille d’Israël pour connaître des affaires religieuses et des autres litiges. (On était revenu à Jérusalem.)
Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
9 Il leur adressa ces recommandations: "Voici comment vous agirez, guidés par la crainte du Seigneur, en toute droiture et d’un cœur intègre.
Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
10 Chaque fois que vos frères, demeurant dans leurs villes respectives, porteront un procès devant vous, qu’il s’agisse d’une question de meurtre ou qu’il s’agisse de doctrine, de prescriptions, de statuts et de droits, vous les éclairerez pour qu’ils ne se rendent pas coupables envers le Seigneur, ce qui vous attirerait à vous et à vos frères la colère divine. Faites ainsi, et vous éviterez les fautes.
Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
11 Et voyez, le prêtre Amariahou sera à votre tête pour toutes les affaires religieuses, et Zebadiahou, fils d’Ismaël, le prince de la maison de Juda, pour toutes les affaires du roi. Les Lévites seront à votre disposition comme prévôts. Courage donc et à l’œuvre! Que l’Eternel assiste quiconque veut le bien!"
“Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”

< 2 Chroniques 19 >