< 2 Chroniques 15 >

1 Azariahou, fils d’Oded, fut saisi de l’inspiration divine.
Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
2 Il sortit au devant d’Asa et lui dit: "Ecoutez-moi, Asa et tout Juda et Benjamin! L’Eternel est avec vous, lorsque vous êtes avec lui; si vous le recherchez, il vous sera accessible; mais si vous l’abandonnez, il vous abandonnera.
Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
3 Or, Israël a vécu de longs jours, sans avoir ni vrai Dieu, ni prêtre pour enseigner, ni Loi.
Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
4 Seulement, quand le malheur l’accablait, il revenait à l’Eternel, Dieu d’Israël, et avait recours à lui, qui les accueillait.
Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
5 En ces temps d’impiété, il n’y avait nulle sécurité pour les allants et venants, tant était grande l’anarchie parmi tous les habitants de ces contrées.
Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
6 Un peuple était écrasé par un autre peuple, une ville par une autre ville, car Dieu les mettait en désarroi par toute sorte de calamités.
Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
7 Vous donc, soyez fermes, ne laissez pas défaillir vos bras, car il y aura une récompense pour vos efforts!"
Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
8 Asa, ayant entendu ces paroles, cette prophétie du prophète Oded, en fut encouragé. Il fit disparaître les impures idoles de tout le pays de Juda et de Benjamin et des villes qu’il avait conquises dans les monts d’Ephraïm, et il restaura l’autel du Seigneur, placé devant le portique de l’Eternel.
Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
9 Il rassembla tout Juda et Benjamin et ceux d’Ephraïm, de Manassé et de Siméon qui étaient venus séjourner parmi eux; de fait des gens d’Israël s’étaient ralliés à lui en grand nombre, en voyant que l’Eternel, son Dieu, était avec lui.
Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
10 Ils s’assemblèrent à Jérusalem le troisième mois de la quinzième année du règne d’Asa.
Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
11 Ce jour-là, ils sacrifièrent à l’Eternel, sur le butin qu’ils avaient amené, sept cents têtes de gros bétail et sept mille brebis.
Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
12 Ils promirent, par un pacte solennel, qu’ils auraient recours à l’Eternel, Dieu de leurs pères, de tout leur cœur et de toute leur âme,
Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
13 et que quiconque n’aurait pas recours à l’Eternel, Dieu d’Israël, serait puni de mort, petit ou grand, homme ou femme.
Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
14 Ils en firent le serment au Seigneur à haute voix, en poussant des acclamations et au son des trompettes et des cors.
Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
15 Tout Juda fut en joie à propos de ce serment, car ils l’avaient prêté de tout cœur, et c’est de toutes les forces de leur volonté qu’ils avaient cherché Dieu et, par conséquent, trouvé. Aussi le Seigneur leur assura-t-il le repos de toute part.
Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
16 Le roi Asa destitua même de la Régence sa mère Maakha, qui avait consacré une image à Astarté; par l’ordre d’Asa, cette image fut abattue, réduite en poussière, et brûlée dans la vallée de Cédron.
Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
17 Toutefois, les hauts lieux ne disparurent point d’Israël; mais le cœur d’Asa resta fidèle à Dieu toute sa vie.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
18 Il fit porter dans la maison de Dieu ce que son père et lui-même avaient consacré en fait d’argent, d’or et de vases précieux.
Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
19 De guerre, il n’y en eut pas jusqu’à la trente-cinquième année du règne d’Asa.
Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.

< 2 Chroniques 15 >