< 1 Chroniques 19 >

1 Sur ces entrefaites, Nahach, le roi des Ammonites, mourut, et son fils lui succéda.
Ikajakuwa baadae kwamba Nahashi, mfalme wa watu wa Amoni, akafa, na mwanae akawa mfalme baada yake.
2 David se dit: "Je veux agir amicalement avec Hanoun, fils de Nahach, comme son père a agi à mon égard." Et David envoya des émissaires pour lui présenter des condoléances au sujet de son père, et les serviteurs de David se rendirent au pays des Ammonites pour porter des condoléances à Hanoun.
Daudi akasema, “Nitaonyesha ukarimu kwa mwana wa Hanuni wa Nahashi, kwasababu baba yake alionyesha ukarimu kwangu.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kumfariji kuhusu baba yake. Watumishi wa Daudi wakaingia nchi ya Waamoni na kumfuata Hanuni, ilikumfariji.
3 Mais les princes ammonites dirent à Hanoun: "Est-ce, à ton avis, pour honorer ton père que David t’a envoyé des consolateurs? N’Est-ce pas plutôt pour explorer, troubler et espionner le pays que ses serviteurs sont venus te trouver?"
Lakini viongozi wakamwambia Hanuni, “Unadhani Daudi anamheshimu baba yako sababu ametuma watu kukufaraji? Je watumishi wake hawajaja kutadhimini nchi iliwaipindue?
4 Alors Hanoun fit saisir les serviteurs de David, ordonna de les raser et de couper la moitié de leurs vêtements jusqu’aux hanches, puis il les congédia.
Hanuni akawakamata watumishi wa Daudi, akawanyoa, akakata mavazi ya nusu kwenye kiuno kushuka, na kuwarudisha.
5 Ceux-ci partis, on mit David au courant de ce qui était arrivé à ces hommes, et il envoya au-devant d’eux car ces hommes étaient accablés de honte et leur fit dire: "Restez à Jéricho jusqu’à ce que votre barbe ait repoussé, puis vous reviendrez."
Walipo eleza haya kwa Daudi, alienda kukutana nao, kwa kuwa walifedheeka sana. Mfalme akasema, “Bakini Yeriko hadi ndevu zenu ziote tena, kisha mrudi.”
6 Les Ammonites, voyant qu’ils s’étaient mis en mauvaise odeur auprès de David, envoyèrent, de concert avec Hanoun, mille kikkar d’argent pour soudoyer dans la Syrie du Double-Fleuve, dans la Syrie de Maakha et de Çoba des chars et des cavaliers.
Waamoni walipoona wamekuwa kikwazo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni walituma talanta elfu moja za fedha kukodisha magari ya farasi kwa Waaremei na wanaume wa farasi kutoka Naharaimu, Maka, na Zoba.
7 Ils soudoyèrent ainsi trente-deux mille chars ainsi que le roi de Maakha et son peuple, qui vinrent camper devant Mèdeba; de leur côté, les Ammonites sortirent ensemble de leurs villes et entrèrent en campagne.
Waliwakodishia magari ya farasi elfu thelathini na mbili pamoja na mfalme wa Maka na watu wake, walio kuja na kueka kambi mbele ya Medeba. Waamoni walijikusanya pamoja kutoka miji yao, na wakaja kwa vita.
8 A cette nouvelle, David envoya Joab avec toute son armée de vaillants.
Daudi alipo sikia, alimtuma Yoabu na wanajeshi wake wote.
9 Les Ammonites s’avancèrent et se mirent en bataille à l’entrée de la ville, tandis que les rois qui étaient accourus restaient séparés dans la campagne.
Watu wa Amoni walikuja na kupanga mstari kwa ajili ya pambano katika lango la mji, wafalme waliokuja walikuwa peke yao katika shamba.
10 Joab, voyant que la bataille le menaçait par-devant et par-derrière, fit choix des meilleurs guerriers d’Israël et les disposa devant les Syriens.
Yoabu alipoona mistari ya pambano imemzunguka mbele na nyuma, alichagua wapambanaji shupavu wa Israeli na kuwa panga dhidi ya Waaremi.
11 Pour le reste de l’armée, il le mit sous les ordres de son frère Abchaï et le rangea devant les Ammonites.
Wanajeshi wengine wote, aliwaeka chini ya Abishai kaka yake, akawapanga kwa mstari dhidi ya Amoni.
12 Et il dit: "Si les Syriens l’emportent sur moi, tu viendras à mon secours; si les Ammonites l’emportent sur toi, c’est moi qui viendrai te secourir.
Yoabu akasema, “Kama Waaremi wananguvu kunizidi, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini kama jeshi la Waamoni lina nguvu kukuzidi, nitakuja kukuokoa.
13 Sois fort, soyons forts pour notre peuple et pour les villes de notre Dieu, et que le Seigneur agisse selon sa volonté!"
Kuwa thabiti, natujionyeshe kwa watu wetu kuwa ni wenye nguvu na kwa miji ya Mungu wetu, kwa kuwa Yahweh ata fanya lililo jema kwa kusudi lake.”
14 Joab, avec la troupe qui l’accompagnait, engagea la bataille contre les Syriens, qui s’enfuirent devant lui.
Hivyo Yoabu na wanajeshi wasogea kwenye pambano dhidi ya Waaremi, walio lazimika kukimbia mbele ya jeshi la Waisraeli.
15 Les Ammonites, voyant fuir les Syriens, lâchèrent pied devant son frère Abchaï et rentrèrent dans la ville; et Joab revint à Jérusalem.
Jeshi la Waamoni walipoona kuwa Waaremi wamekimbia, wao pia wakamkimbia kaka yake Yoabu Abishai na kurudi mjini. Kisha Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na kurudi Yerusalemu.
16 Mais les Syriens, se voyant battus par les Israélites, envoyèrent des messagers et firent avancer les Syriens de delà le Fleuve, sous le commandement de Chopakh, chef de l’armée de Hadadézer.
Waaremi walipoona kuwa wanashindwa na Waisraeli, wakatuma msaada nyuma ya Mto Frati, na Shofaki mkuu wajeshi la Hadadezeri.
17 Quand David en fut informé, il rassembla tout Israël, traversa le Jourdain, arriva à Hélam et aligna ses troupes en face d’eux. Il commença à combattre les Syriens, qui acceptèrent la bataille.
Daudi alipo ambiwa haya, akakusanya Israeli yote, akuvuka Yordani, na kuja juu yao. Alipanga jeshi kwa ajili ya pambano dhidi ya Waaremi, na wakapigana nao.
18 Aram prit la fuite devant Israël, et David lui tua sept mille attelages et quarante mille hommes de pied. Il fit périr aussi Chopakh, chef de l’armée.
Waaremi waliwakimbia Waisraeli, na Daudi akaua waendesha magari ya farasi ya Waaremi elfu saba na wanajeshi wa miguu elfu arobaini. Pia alimuua Shopaki, mkuu wa jeshi.
19 Les serviteurs de Hadadézer, voyant qu’Israël les avait défaits, firent la paix avec David et devinrent ses tributaires; et les Syriens ne furent plus disposés à venir en aide aux Ammonites.
Wafalme wote walio kuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Daudi na kumtumikia. Hivyo watu wa Aramu hawakuwa tayari kuwasaidia Waamoni.

< 1 Chroniques 19 >