< 1 Chroniques 18 >
1 David défit ensuite les Philistins, abattit leur puissance et leur enleva Gath et ses dépendances.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
2 Puis il vainquit les Moabites, qui furent assujettis à David et devinrent ses tributaires.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
3 Puis David battit Hadarézer, roi de Çoba, du côté de Hamath, tandis qu’il marchait vers l’Euphrate pour étendre sa domination.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
4 David lui captura mille chars, sept mille cavaliers et vingt mille hommes de pied, fit mutiler tous les attelages, et n’en conserva que cent.
Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
5 La Syrie de Damas vint au secours de Hadarézer, roi de Çoba; David tua aux Syriens vingt-deux mille hommes.
Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 Il mit ensuite des garnisons dans la Syrie de Damas, qui devint sujette et tributaire de David. Ainsi le Seigneur protégeait David dans toutes ses campagnes.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 David s’empara des boucliers d’or, que portaient les serviteurs de Hadarézer, et les transporta à Jérusalem.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 Egalement de Thibat et de Koun, villes de Hadarézer, le roi David emporta du cuivre en grande quantité, qui servit à Salomon pour faire la Mer de cuivre, les colonnes et les objets en cuivre.
Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
9 Toou, roi de Hamath, ayant appris que David avait défait toute l’armée de Hadarézer, roi de Çoba,
Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
10 envoya son fils Hadoram au roi David pour le saluer et le féliciter d’avoir combattu et vaincu Hadarézer, car celui-ci était en guerre avec Toou. Il lui envoyait en même temps toute sorte de vases d’or, d’argent et de cuivre.
akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
11 Ceux-là aussi, le roi David les consacra à l’Eternel, comme il avait fait de l’argent et de l’or qu’il avait enlevés à tous les peuples, aux Iduméens, aux Moabites, aux Ammonites, aux Philistins et aux Amalécites.
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
12 Abchaï, fils de Cerouya, avait battu dix-huit mille Iduméens dans la vallée du Sel.
Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
13 Il mit des garnisons dans l’Idumée, de sorte que toute l’Idumée devint tributaire de David. Et le Seigneur protégea David dans toutes ses voies.
Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
14 David régna sur tout Israël, et il gouverna tout son peuple avec justice et équité.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
15 Joab, fils de Cerouya, était chef de l’armée; Josaphat, fils d’Ahiloud, archiviste;
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
16 Çadok, fils d’Ahitoub, et Abimélec, fils d’Ebiatar, prêtres; Chavcha, secrétaire;
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
17 Benaïahou, fils de Joïada, était à la tête des Krêthi et Pelêthi; et les fils de David étaient les premiers ministres du roi.
naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.