< 1 Chroniques 16 >

1 On introduisit l’arche de Dieu et on l’installa dans le pavillon que David avait dressé pour elle, et on offrit devant Dieu des holocaustes et des rémunératoires.
Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 Lorsque David eut achevé d’offrir ces holocaustes et ces rémunératoires, il bénit le peuple au nom de l’Eternel,
Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
3 fit distribuer à tout Israël, hommes et femmes, à chacun une miche de pain, une pièce de viande et une mesure de vin.
Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
4 Il établit devant l’arche de l’Eternel des Lévites chargés du culte, pour célébrer, louer et chanter l’Eternel, Dieu d’Israël:
Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
5 à savoir Assaph, comme chef, Zekharia, comme second, Yeïêl, Chemiramot, Yehïêl, Mattitia, Elïab, Benaïahou, Obed-Edom. Yeïêl jouait du luth et de la harpe, Assaph de la cymbale,
Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
6 Benaïahou et Yahazïêl, prêtres, de la trompette, régulièrement devant l’arche d’alliance de Dieu.
nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
7 C’Est ce jour-là que David confia la direction des chants de grâce à l’Eternel à Assaph et à ses frères.
Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
8 Rendez hommage à l’Eternel, proclamez son nom, Publiez parmi les nations ses hauts faits.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
9 Chantez, en son honneur, célébrez-le, Entretenez-vous de toutes ses merveilles.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10 Glorifiez-vous de son saint nom; Que le cœur de ceux qui recherchent l’Eternel soit en joie!
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
11 Mettez-vous en quête de l’Eternel et de sa puissance, Aspirez constamment à jouir de sa présence.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12 Souvenez-vous des merveilles qu’il a opérées, De ses prodiges et des arrêts sortis de sa bouche,
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
13 Vous, ô postérité d’Israël, son serviteur, Fils de Jacob, ses élus!
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 Il est, lui, l’Eternel, notre Dieu; Ses jugements s’étendent à toute la terre.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15 Rappelez-vous éternellement son alliance, Le pacte qu’il a promulgué pour mille générations,
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16 Qu’il a conclu avec Abraham, Qu’il a fait par serment avec Isaac.
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17 Il l’a érigé en loi pour Jacob, En contrat immuable pour Israël.
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18 "C’Est à toi, disait-il, que je donnerai le pays de Canaan Comme un lot héréditaire,
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19 Quoique vous soyez encore en petit nombre, Et à peine établis comme étrangers dans ce pays."
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
20 Puis ils se mirent à errer de nation en nation, D’Un royaume vers un autre peuple.
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21 Il ne permit à personne de les opprimer, Et à cause d’eux il châtia des rois:
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22 "Ne touchez pas à mes oints, Ne faites pas de mal à mes prophètes!"
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
23 Chantez à l’Eternel, toute la terre, Publiez de jour en jour son secours.
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24 Proclamez parmi les peuples sa gloire, Parmi toutes les nations, ses merveilles,
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25 Car grand est l’Eternel et infiniment digne de louanges; Il est redoutable plus que toutes les divinités.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
26 Car tous les dieux des nations sont de vaines idoles, Mais l’Éternel est l’auteur des cieux.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27 Majesté et splendeur forment son avant-garde, Force et magnificence emplissent sa résidence.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28 Célébrez l’Eternel, groupes de nations, Célébrez sa gloire et sa puissance;
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29 Rendez hommage au nom glorieux de l’Eternel, Apportez des offrandes et présentez-vous devant Lui; Prosternez-vous devant l’Eternel en un saint apparat.
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
30 Que toute la terre tremble devant lui! Grâce à lui, l’univers est stable et ne vacille point.
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31 Que les cieux se réjouissent Que la terre soit dans l’allégresse, Qu’on dise parmi les peuples: "L’Eternel est roi!"
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32 Que la mer gronde avec ce qu’elle contient, Que les champs éclatent en transports Avec tout ce qui les couvre!
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33 Qu’en même temps les arbres de la forêt résonnent joyeusement A l’approche de l’Eternel! Car il vient pour juger la terre.
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
34 Rendez hommage à l’Eternel, car il est bon, Car sa grâce dure à jamais.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
35 Dites: "Viens à notre secours, Dieu de notre salut, Rassemble-nous et délivre-nous d’entre les nations, Pour que nous rendions hommage à ton saint nom, Et célébrions tes louanges.
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
36 Béni soit l’Eternel, le Dieu d’Israël, D’Éternité en éternité!" Et le peuple tout entier dit: "Amen et louange à l’Eternel!"
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
37 David commit donc là, devant l’arche d’alliance de l’Eternel, à Assaph et à ses frères, la mission de faire le service devant l’arche d’une manière régulière, suivant les exigences de chaque jour.
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
38 Obed-Edom, fils de Yedithoun, et Hossa et leurs frères, au nombre de soixante-huit, furent établis portiers.
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
39 Çadok, le pontife, et ses frères, les prêtres, restèrent devant le sanctuaire de l’Eternel, au haut lieu qui était à Gabaon,
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
40 pour offrir des holocaustes à l’Eternel, sur l’autel des holocaustes, régulièrement, matin et soir, accomplissant tout ce qui est écrit dans la Loi de l’Eternel, prescrite à tout Israël.
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
41 Avec eux étaient Hêmân, Yedouthoun et les autres hommes de choix, qui avaient été désignés nominativement. Ils louaient l’Eternel, disant: "Car éternelle est sa grâce."
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
42 Hêmân et Yedouthoun avaient la garde des trompettes et des cymbales dont on jouait et des instruments de musique du culte. Les fils de Yedouthoun étaient préposés aux portes.
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
43 Puis tout le peuple se retira, chacun chez soi, et David rentra pour bénir sa famille.
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

< 1 Chroniques 16 >