< 1 Chroniques 10 >
1 Cependant les Philistins livraient bataille aux Israélites. Ceux-ci s’enfuirent devant eux et laissèrent des morts sur la montagne de Ghelboé.
Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika mlima Gilboa.
2 Les Philistins atteignirent Saül et ses fils et tuèrent Jonathan, Abinadab et Malki-Choua, fils de Saül.
Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
3 L’Attaque s’acharna contre Saül; il fut surpris par les archers qui lui causèrent de la frayeur.
Mapigano yakawa makali kumzunguka Sauli na wakati wapiga mishale walipompata, wakamjeruhi.
4 Saül dit alors à son écuyer: "Tire ton épée et me transperce pour que je ne sois pas en butte aux coups de ces incirconcis et à leurs outrages." Mais l’écuyer, saisi de peur, n’osa. Alors Saül prit l’épée et se jeta dessus.
Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
5 L’Écuyer de Saül, le voyant mort, se jeta, lui aussi, sur son épée et mourut.
Mbeba silaha wake alipoona kwamba Sauli amekufa, naye pia akauangukia upanga wake akafa.
6 Ainsi périrent Saül, ses trois fils; et tous les gens de sa maison moururent ensemble.
Kwa hiyo Sauli na wanawe watatu wakafa, pamoja na nyumba yake yote.
7 Les Israélites qui étaient dans la vallée, voyant que leurs frères avaient lâché pied et que Saül et ses fils étaient morts, abandonnèrent leurs villes et se sauvèrent. Les Philistins y pénétrèrent et s’y établirent.
Waisraeli wote waliokuwa bondeni walipoona kwamba jeshi limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliacha miji yao wakakimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
8 Le lendemain, les Philistins vinrent dépouiller les cadavres; ils trouvèrent ceux de Saül et de ses fils gisant sur le mont Ghelboé.
Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe wameanguka katika Mlima Gilboa.
9 Ils le dépouillèrent, lui tranchèrent la tête et lui enlevèrent ses armes, qu’ils envoyèrent dans le pays des Philistins à la ronde, pour annoncer la nouvelle à leurs idoles et au peuple.
Wakamvua mavazi, wakachukua kichwa chake pamoja na silaha zake, wakawatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari hizi miongoni mwa sanamu zao na watu wao.
10 Ils déposèrent ses armes dans le temple de leur dieu et attachèrent son crâne au temple de Dagon.
Waliweka silaha zake katika hekalu la miungu yao, wakatundika kichwa chake katika hekalu la Dagoni.
11 Tous les habitants de Jabès-Galaad ayant appris ce que les Philistins avaient fait à Saül,
Wakazi wote wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yote Wafilisti waliyomtendea Sauli,
12 les plus résolus allèrent enlever le corps de Saül et ceux de ses fils et les transportèrent à Jabès; puis ils enterrèrent leurs ossements sous le tamarisc de Jabès, et l’on jeûna durant sept jours.
mashujaa wao wote wakaondoka, wakautwaa mwili wa Sauli na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi. Wakaizika mifupa yao chini ya mti mkubwa huko Yabeshi, nao wakafunga kwa siku saba.
13 Ainsi mourut Saül à cause de l’infidélité qu’il avait commise envers Dieu, en désobéissant à sa parole et en allant consulter les nécromanciens,
Sauli alikufa kwa sababu hakuwa mwaminifu kwa Bwana. Hakulishika neno la Bwana, hata akataka shauri kwa mwaguzi kwa ajili ya uongozi,
14 au lieu de rechercher l’Eternel. Celui-ci le fit périr et fit passer la royauté à David, fils de Jessé.
hakumuuliza Bwana. Kwa hiyo Bwana alimuua, na ufalme akampa Daudi mwana wa Yese.