< Psaumes 78 >
1 Pour instruire. D’Asaph. Prête l’oreille à ma loi, mon peuple! inclinez vos oreilles aux paroles de ma bouche.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 J’ouvrirai ma bouche en paraboles, j’annoncerai les énigmes [des jours] d’autrefois,
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Que nous avons entendues et connues, et que nos pères nous ont racontées.
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 Nous ne les cèlerons pas à leurs fils; nous raconterons à la génération à venir les louanges de l’Éternel, et sa force, et ses merveilles qu’il a faites.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Il a établi un témoignage en Jacob, et il a mis en Israël une loi qu’il a commandée à nos pères, pour qu’ils les fassent connaître à leurs fils,
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 Afin que la génération à venir, les fils qui naîtraient, les connaissent, [et] qu’ils se lèvent et les annoncent à leurs fils,
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 Et qu’ils mettent leur confiance en Dieu, et qu’ils n’oublient pas les œuvres de Dieu, et qu’ils observent ses commandements,
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 Et qu’ils ne soient pas, comme leurs pères, une génération indocile et rebelle, une génération qui n’a point affermi son cœur, et dont l’esprit n’a pas été fidèle à Dieu.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 Les fils d’Éphraïm, armés [et] tirant de l’arc, ont tourné le dos le jour du combat.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 Ils n’ont pas gardé l’alliance de Dieu, et ont refusé de marcher selon sa loi;
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 Et ils ont oublié ses actes et ses œuvres merveilleuses, qu’il leur avait fait voir.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Il fit des merveilles devant leurs pères dans le pays d’Égypte, dans la campagne de Tsoan.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 Il fendit la mer, et les fit passer: il fit se dresser les eaux comme un monceau;
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Et il les conduisit, le jour par une nuée, et toute la nuit par une lumière de feu.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Il fendit les rochers dans le désert, et les abreuva comme aux abîmes, abondamment;
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Et il fit sortir des ruisseaux du rocher, et fit couler les eaux comme des fleuves.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Et ils péchèrent de nouveau contre lui, irritant le Très-haut dans le désert;
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 Et ils tentèrent Dieu dans leurs cœurs, en demandant de la viande selon leur désir;
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Et ils parlèrent contre Dieu; ils dirent: Dieu pourrait-il dresser une table dans le désert?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Voici, il a frappé le rocher, et les eaux ont coulé, et des rivières ont débordé: pourrait-il aussi donner du pain, ou préparer de la chair à son peuple?
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 C’est pourquoi l’Éternel les entendit, et se mit en grande colère; et le feu s’alluma contre Jacob, et la colère aussi monta contre Israël,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 Car ils ne crurent pas Dieu, et ne se fièrent pas en son salut,
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Bien qu’il ait commandé aux nuées d’en haut, et qu’il ait ouvert les portes des cieux,
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 Et qu’il ait fait pleuvoir sur eux la manne pour manger, et qu’il leur ait donné le blé des cieux:
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 L’homme mangea le pain des puissants; il leur envoya des vivres à satiété.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 Il fit lever dans les cieux le vent d’orient, et il amena par sa puissance le vent du midi;
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 Et il fit pleuvoir sur eux de la chair comme de la poussière, et, comme le sable des mers, des oiseaux ailés;
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Et il les fit tomber au milieu de leur camp, autour de leurs demeures.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Et ils en mangèrent, et en furent abondamment rassasiés. Il leur envoya ce qu’ils convoitaient.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Ils ne s’étaient pas encore détournés de leur convoitise, leur viande était encore dans leur bouche,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 Que la colère de Dieu monta contre eux; et il tua de leurs hommes forts, et abattit les hommes d’élite d’Israël.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Avec tout cela ils péchèrent encore, et ne crurent point par ses œuvres merveilleuses;
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Et il consuma leurs jours par la vanité, et leurs années par la frayeur.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 S’il les tuait, alors ils le recherchaient, et ils se retournaient, et cherchaient Dieu dès le matin;
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 Et ils se souvenaient que Dieu était leur rocher, et Dieu, le Très-haut, leur rédempteur;
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Mais ils le flattaient de leur bouche et ils lui mentaient de leur langue;
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 Et leur cœur n’était pas ferme envers lui, et ils ne furent pas fidèles dans son alliance.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 Mais lui, étant miséricordieux, pardonna l’iniquité et ne [les] détruisit pas; mais il détourna souvent sa colère, et n’éveilla pas toute sa fureur.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Et il se souvint qu’ils étaient chair, un souffle qui passe et ne revient pas.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Que de fois ils l’irritèrent dans le désert, [et] le provoquèrent dans le lieu désolé!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Et ils recommencèrent et tentèrent Dieu, et affligèrent le Saint d’Israël:
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 Ils ne se souvinrent pas de sa main au jour où il les avait délivrés de l’oppresseur,
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 Lorsqu’il mit ses signes en Égypte, et ses prodiges dans les campagnes de Tsoan,
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 Et qu’il changea en sang leurs canaux et leurs courants d’eau, de sorte qu’ils n’en puissent pas boire;
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Il envoya contre eux des mouches qui les dévorèrent, et des grenouilles qui les détruisirent;
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 Et il livra leurs fruits à la locuste, et leur travail à la sauterelle.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 Il fit périr leurs vignes par la grêle, et leurs sycomores par les grêlons;
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 Et il livra leur bétail à la grêle, et leurs troupeaux à la foudre.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Il envoya sur eux l’ardeur de sa colère, la fureur, et l’indignation, et la détresse, une troupe d’anges de malheur.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 Il fraya un chemin à sa colère; il ne préserva pas leurs âmes de la mort, et livra leur vie à la peste;
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 Et il frappa tout premier-né en Égypte, les prémices de la vigueur dans les tentes de Cham.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 Et il fit partir son peuple comme des brebis, et les mena comme un troupeau dans le désert;
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Et il les conduisit sains et saufs, et ils furent sans crainte; et la mer couvrit leurs ennemis.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 Et il les introduisit dans les confins de sa sainte [terre], cette montagne que sa droite s’est acquise.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Et il chassa de devant eux les nations, et leur partagea un héritage, et fit habiter dans leurs tentes les tribus d’Israël.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Mais ils tentèrent et irritèrent le Dieu Très-haut, et ne gardèrent pas ses témoignages,
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Et se retirèrent, et agirent infidèlement, comme leurs pères; ils tournèrent comme un arc trompeur.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Et ils le provoquèrent à colère par leurs hauts lieux, et l’émurent à jalousie par leurs images taillées.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Dieu l’entendit, et se mit en grande colère, et il méprisa fort Israël.
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Et il abandonna la demeure de Silo, la tente où il avait habité parmi les hommes;
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Et il livra à la captivité sa force, et sa magnificence en la main de l’ennemi;
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Et il livra son peuple à l’épée, et se mit en grande colère contre son héritage:
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Le feu dévora leurs jeunes hommes, et leurs vierges ne furent pas célébrées;
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Leurs sacrificateurs tombèrent par l’épée, et leurs veuves ne se lamentèrent pas.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Alors le Seigneur s’éveilla comme un homme qui dort, et comme un homme puissant qui, [animé] par le vin, pousse des cris.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 Et il frappa ses ennemis par-derrière, il les livra à un opprobre éternel.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Et il méprisa la tente de Joseph, et ne choisit pas la tribu d’Éphraïm;
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Mais il choisit la tribu de Juda, la montagne de Sion qu’il aima.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 Et il bâtit son sanctuaire comme des lieux très hauts, comme la terre qu’il a fondée pour toujours.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 Et il choisit David, son serviteur, et le prit des parcs des brebis;
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 Il le fit venir d’auprès des brebis qui allaitent, pour paître Jacob, son peuple, et Israël, son héritage.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 Et il les fit paître selon l’intégrité de son cœur, et les conduisit par l’intelligence de ses mains.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.