< Psaumes 75 >

1 Au chef de musique. Al-Tashkheth. Psaume d’Asaph. Cantique. Nous te célébrons, ô Dieu! nous te célébrons, et ton nom est proche: tes merveilles le racontent.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Quand je recevrai l’assemblée, je jugerai avec droiture.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 La terre et tous ses habitants se sont fondus; moi, j’affermis ses piliers. (Sélah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 J’ai dit à ceux qui se glorifient: Ne vous glorifiez pas; et aux méchants: N’élevez pas [votre] corne;
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 N’élevez pas en haut votre corne, ne parlez pas avec arrogance, d’un cou [roide].
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 Car ce n’est ni du levant, ni du couchant, ni du midi, que vient l’élévation.
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 Car c’est Dieu qui juge; il abaisse l’un, et élève l’autre.
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 Car une coupe est dans la main de l’Éternel, et elle écume de vin; elle est pleine de mixtion, et il en verse: oui, tous les méchants de la terre en suceront la lie, ils la boiront.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 Mais moi, je raconterai [ces choses] à toujours; je chanterai au Dieu de Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 Et toutes les cornes des méchants, je les abattrai; [mais] les cornes des justes seront élevées.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psaumes 75 >