< Psaumes 57 >

1 Au chef de musique. Al-Tashkheth. De David. Mictam; quand il fuyait devant Saül, dans la caverne. Use de grâce envers moi, ô Dieu! use de grâce envers moi; car en toi mon âme se réfugie, et sous l’ombre de tes ailes je me réfugie, jusqu’à ce que les calamités soient passées.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 Je crierai au Dieu Très-haut, à Dieu qui mène [tout] à bonne fin pour moi.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 Il a envoyé des cieux, et m’a sauvé; il a couvert de honte celui qui veut m’engloutir. (Sélah) Dieu a envoyé sa bonté et sa vérité.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 Mon âme est au milieu de lions; je suis couché parmi ceux qui soufflent des flammes, – les fils des hommes, dont les dents sont des lances et des flèches, et la langue une épée aiguë.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Élève-toi, ô Dieu! au-dessus des cieux; que ta gloire soit au-dessus de toute la terre!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Ils ont préparé un filet pour mes pas, mon âme se courbait; ils ont creusé devant moi une fosse, ils sont tombés dedans. (Sélah)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 Mon cœur est affermi, ô Dieu! mon cœur est affermi; je chanterai et je psalmodierai.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Éveille-toi, mon âme! Éveillez-vous, luth et harpe! Je m’éveillerai à l’aube du jour.
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 Je te célébrerai parmi les peuples, ô Seigneur! je chanterai tes louanges parmi les peuplades;
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 Car ta bonté est grande jusqu’aux cieux, et ta vérité jusqu’aux nues.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 Élève-toi, ô Dieu! au-dessus des cieux; que ta gloire soit au-dessus de toute la terre!
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.

< Psaumes 57 >