< Psaumes 112 >

1 Louez Jah. Bienheureux l’homme qui craint l’Éternel [et] qui prend un grand plaisir en ses commandements!
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 Sa semence sera puissante dans le pays; … la génération des hommes droits sera bénie.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 Les biens et la richesse seront dans sa maison, et sa justice demeure à perpétuité.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 La lumière se lève dans les ténèbres pour les hommes droits. Il est plein de grâce, et miséricordieux, et juste.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 Heureux l’homme qui use de grâce, et qui prête! Il maintiendra sa cause dans le jugement;
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 Aussi il ne sera jamais ébranlé. La mémoire du juste sera à toujours.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 Il ne craindra pas une mauvaise nouvelle; son cœur est ferme, se confiant en l’Éternel;
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 Son cœur est soutenu; il ne craint pas, jusqu’à ce qu’il voie [son plaisir] en ses adversaires.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 Il répand, il donne aux pauvres; sa justice demeure à perpétuité; sa corne est élevée en gloire.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 Le méchant [le] verra, et en aura du dépit; il grincera des dents et se fondra; le désir des méchants périra.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

< Psaumes 112 >