< Nombres 1 >

1 Et l’Éternel parla à Moïse, au désert de Sinaï, dans la tente d’assignation, le premier [jour] du second mois de la seconde année après leur sortie du pays d’Égypte, disant:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 Relevez la somme de toute l’assemblée des fils d’Israël, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, tous les mâles, par tête:
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux d’Israël qui sont propres au service militaire, vous les compterez selon leurs armées, toi et Aaron.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 Et, avec vous, il y aura un homme par tribu, un homme chef de sa maison de pères.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 Et ce sont ici les noms des hommes qui se tiendront avec vous: pour Ruben, Élitsur, fils de Shedéur;
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 pour Siméon, Shelumiel, fils de Tsurishaddaï;
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 pour Juda, Nakhshon, fils d’Amminadab;
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 pour Issacar, Nethaneël, fils de Tsuar;
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 pour Zabulon, Éliab, fils de Hélon;
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 pour les fils de Joseph, pour Éphraïm, Élishama, fils d’Ammihud; pour Manassé, Gameliel, fils de Pedahtsur;
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 pour Benjamin, Abidan, fils de Guidhoni;
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 pour Dan, Akhiézer, fils d’Ammishaddaï;
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 pour Aser, Paghiel, fils d’Ocran;
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 pour Gad, Éliasaph, fils de Dehuel;
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 pour Nephthali, Akhira, fils d’Énan.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 Ce sont là ceux qui furent les principaux de l’assemblée, les princes des tribus de leurs pères, les chefs des milliers d’Israël.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Et Moïse et Aaron prirent ces hommes-là, qui avaient été désignés par leurs noms,
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 et ils réunirent toute l’assemblée, le premier [jour] du second mois; et chacun déclara sa filiation, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, par tête.
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 Comme l’Éternel l’avait commandé à Moïse, ainsi il les dénombra dans le désert de Sinaï.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 Et les fils de Ruben, premier-né d’Israël, leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, par tête, tous les mâles, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Ruben furent 46 500.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Des fils de Siméon: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, ceux qui furent dénombrés suivant le nombre des noms, par tête, tous les mâles, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Siméon furent 59 300.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Des fils de Gad: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Gad furent 45 650.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Des fils de Juda: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Juda furent 74 600.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 Des fils d’Issacar: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 ceux qui furent dénombrés de la tribu d’Issacar furent 54 400.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Des fils de Zabulon: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Zabulon furent 57 400.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 Des fils de Joseph, des fils d’Éphraïm: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 ceux qui furent dénombrés de la tribu d’Éphraïm furent 40 500.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Des fils de Manassé: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Manassé furent 32 200.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Des fils de Benjamin: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Benjamin furent 35 400.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Des fils de Dan: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Dan furent 62 700.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Des fils d’Aser: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 ceux qui furent dénombrés de la tribu d’Aser furent 41 500.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 Des fils de Nephthali: leurs générations, selon leurs familles, selon leurs maisons de pères, suivant le nombre des noms, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire,
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 ceux qui furent dénombrés de la tribu de Nephthali furent 53 400.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Ce sont là les dénombrés que Moïse et Aaron et les douze hommes, princes d’Israël, dénombrèrent: il y avait un homme pour chaque maison de pères.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 Et tous les dénombrés des fils d’Israël, selon leurs maisons de pères, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, tous ceux qui étaient propres au service militaire en Israël,
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 tous les dénombrés, furent 603 550.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Mais les Lévites, selon la tribu de leurs pères, ne furent pas dénombrés parmi eux.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 Car l’Éternel avait parlé à Moïse, disant:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 Seulement, tu ne dénombreras pas la tribu de Lévi et tu n’en relèveras pas la somme parmi les fils d’Israël.
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 Et toi, tu préposeras les Lévites sur le tabernacle du témoignage, et sur tous ses ustensiles, et sur tout ce qui lui appartient: ce seront eux qui porteront le tabernacle et tous ses ustensiles; ils en feront le service, et camperont autour du tabernacle;
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 et quand le tabernacle partira, les Lévites le démonteront, et quand le tabernacle campera, les Lévites le dresseront; et l’étranger qui en approchera sera mis à mort.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 Et les fils d’Israël camperont chacun dans son camp, et chacun près de sa bannière, selon leurs armées.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Et les Lévites camperont autour du tabernacle du témoignage, afin qu’il n’y ait point de colère sur l’assemblée des fils d’Israël; et les Lévites auront la garde du tabernacle du témoignage.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 Et les fils d’Israël firent selon tout ce que l’Éternel avait commandé à Moïse; ils firent ainsi.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Nombres 1 >