< Marc 6 >

1 Et il sortit de là, et vint dans son pays; et ses disciples le suivent.
Na akaondoka hapo na kwenda mjini kwao, na wanafunzi wake wakamfuata.
2 Et le sabbat étant venu, il se mit à enseigner dans la synagogue; et plusieurs, l’ayant entendu, étaient dans l’étonnement, disant: D’où [viennent] ces choses à celui-ci? Et quelle est cette sagesse qui lui est donnée, et [d’où vient] que de tels miracles s’opèrent par ses mains?
Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika Sinagogi. Watu wengi walimsikia na wakashangazwa. Wakasema, “Amepata wapi mafundisho haya?” “Ni hekima gani hii aliyopewa?” “Anatendaje miujiza hii kwa mikono yake?”
3 Celui-ci n’est-il pas le charpentier, le fils de Marie, et le frère de Jacques et de Joses et de Jude et de Simon; et ses sœurs ne sont-elles pas ici auprès de nous? Et ils étaient scandalisés en lui.
“Je huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simioni? Je dada zake si wanaishi papa hapa pamoja nasi?” Na hawakufurahishwa na Yesu.
4 Et Jésus leur dit: Un prophète n’est pas sans honneur, si ce n’est dans son pays et parmi ses parents et dans sa maison.
Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika mji wake na miongoni mwa ndugu zake na nyumbani mwake.”
5 Et il ne put faire là aucun miracle, sinon qu’il imposa les mains à un petit nombre d’infirmes, et les guérit.
Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache akawaponya.
6 Et il s’étonnait de leur incrédulité; et il visitait l’un après l’autre les villages à la ronde, en enseignant.
Alishangazwa sana kwa sababu ya kutokuamini kwao. Kisha alivitembelea vijiji vya jirani akifundisha.
7 Et il appelle les douze; et il se mit à les envoyer deux à deux, et leur donna autorité sur les esprits immondes.
Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili akaanza kuwatuma wawili wawili. Aliwapa mamlaka juu ya pepo wachafu,
8 Et il leur commanda de ne rien prendre pour le chemin, si ce n’est un bâton seulement, ni sac, ni pain, ni monnaie dans leur ceinture,
na kuwaamuru wasichukue chochote wanapokwenda isipokuwa fimbo tu. Wasichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni;
9 mais d’être chaussés de sandales; et ne portez pas deux tuniques.
lakini wavae viatu, na siyo kanzu mbili.
10 Et il leur dit: Partout où vous entrerez dans une maison, demeurez-y jusqu’à ce que vous partiez de là;
Na akawaambia, “Nyumba yoyote mtakayoingia, kaeni hapo mpaka mtakapoondoka.
11 et tous ceux qui ne vous recevront pas et ne vous écouteront pas, quand vous partirez de là, secouez la poussière de dessous vos pieds, pour leur servir de témoignage.
Na mji wowote usipowapokea wala kuwasikiliza, ondokeni kwao, kung'uteni mavumbi ya miguu yenu, iwe ushuhuda kwao.”
12 Et étant partis, ils prêchèrent qu’on se repente,
Nao wakaenda wakitangaza watu watubu na kuacha dhambi zao.
13 et chassèrent beaucoup de démons, et oignirent d’huile beaucoup d’infirmes et les guérirent.
Waliwafukuza pepo wengi, na waliwapaka mafuta wagonjwa na wakaponywa.
14 Et le roi Hérode entendit parler [de lui], car son nom était devenu public; et il dit: Jean le baptiseur est ressuscité d’entre les morts; et c’est pourquoi les miracles s’opèrent par lui.
Mfalme Herode aliposikia hayo, kwa kuwa jina la Yesu lilikuwa limejulikana sana. Baadhi walisema, “Yohana mbatizaji amefufuka na kwa sababu hiyo, hii nguvu ya miujiza inafanya kazi ndani yake.”
15 Et d’autres disaient: C’est Élie; et d’autres disaient: C’est un prophète, comme un des prophètes.
Baadhi yao wakasema, “Huyu ni Eliya,” Bado wengine wakasema, “Huyu ni nabii, kama mmoja wa wale manabii wa zamani.”
16 Mais Hérode, ayant appris [ce qu’il faisait], dit: C’est Jean que j’ai fait décapiter; il est ressuscité d’entre les morts.
Lakini Herode aliposikia haya akasema, “Yohana, niliyemkata kichwa amefufuliwa.”
17 Car Hérode lui-même avait envoyé prendre Jean, et l’avait fait lier dans une prison, à cause d’Hérodias, la femme de Philippe son frère; car il l’avait épousée.
Maana Herode mwenyewe aliagiza Yohana akamatwe na alimfunga gerezani kwa sababu ya Herodia (mke wa kaka yake Filipo) kwa sababu yeye alikuwa amemuoa.
18 Car Jean disait à Hérode: Il ne t’est pas permis d’avoir la femme de ton frère.
Kwa maana Yohana alimwambia Herode, “Si halali kumuoa mke wa kaka yako.”
19 Et Hérodias lui en voulait, et aurait désiré le faire mourir; et elle ne pouvait pas,
Lakini Herodia alianza kumchukia na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza,
20 car Hérode craignait Jean, le sachant homme juste et saint, et il le gardait soigneusement; et lorsqu’il l’avait entendu, il faisait beaucoup de choses, et il l’écoutait volontiers.
maana Herode alimwogopa Yohana; alijua kwamba ni mwenye haki mtu mtakatifu, na alimwacha salama. Na alipoendelea kumsikiliza alihuzunika sana, lakini alifurahi kumsikiliza.
21 Et un jour favorable étant venu, lorsque Hérode, le jour anniversaire de sa naissance, donnait un repas à ses grands seigneurs, et aux chiliarques, et aux principaux de la Galilée;
Hata ilipofika wakati mwafaka ikiwa imekaribia siku ya kuzaliwa Herode akawaandalia moafisa wake karamu, na makamanda, na viongozi wa Galilaya.
22 et la fille de cette même Hérodias, étant entrée et ayant dansé, plut à Hérode et à ceux qui étaient à table avec lui. Et le roi dit à la jeune fille: Demande-moi tout ce que tu voudras, et je te le donnerai.
Ndipo binti wa Herodia akaingia na kucheza mbele yao, akamfurahisha Herode na wageni walioketi wakati wa chakula cha jioni. Ndipo mfalme akamwambia binti, “Niombe chochote unachotaka nami nitakupa.”
23 Et il lui jura: Tout ce que tu me demanderas, je te le donnerai, jusqu’à la moitié de mon royaume.
Akamwapia na kusema, chochote utakachoniomba, nitakupa, hata nusu ya ufalme wangu.”
24 Et elle sortit et dit à sa mère: Que dois-je demander? Et celle-ci dit: La tête de Jean le baptiseur.
Akatoka nje akamuuliza mama yake, “Niombe nini?” Akasema, “Kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
25 Et aussitôt elle entra avec empressement vers le roi, et fit sa demande, disant: Je veux que sur-le-champ tu me donnes dans un plat la tête de Jean le baptiseur.
Na mara moja akaingia kwa mfalme akaanza kusema, “Nataka unipatie ndani ya sahani, kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
26 Et le roi en fut très attristé, mais, à cause des serments et de ceux qui étaient à table avec lui, il ne voulut pas lui manquer de parole.
Mfalme alisikitishwa sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake na kwa ajili ya wageni, hakuweza kumkatalia ombi lake.
27 Et le roi aussitôt envoya un de ses gardes, et lui commanda d’apporter la tête de Jean. Et celui-ci, s’en étant allé, le décapita dans la prison,
Hivyo, mfalme akatuma askari kati ya walinzi wake na kuwaagiza kwenda kumletea kichwa cha Yohana. Mlinzi alikwenda kumkata kichwa akiwa kifungoni.
28 et apporta sa tête dans un plat, et la donna à la jeune fille; et la jeune fille la donna à sa mère.
Akakileta kichwa chake kwenye sahani na kumpatia binti, na binti akampa mama yake.
29 Et ses disciples, l’ayant appris, vinrent et enlevèrent son corps et le mirent dans un sépulcre.
Na wanafunzi wake waliposikia hayo, walikwenda kuuchukua mwili wake wakaenda kuuzika kaburini.
30 Et les apôtres se rassemblent auprès de Jésus; et ils lui racontèrent tout: et tout ce qu’ils avaient fait, et tout ce qu’ils avaient enseigné.
Na mitume, walikusanyika pamoja mbele ya Yesu, wakamweleza yote waliyofanya na waliyoyafundisha.
31 Et il leur dit: Venez à l’écart vous-mêmes dans un lieu désert, et reposez-vous un peu; car il y avait beaucoup de gens qui allaient et qui venaient, et ils n’avaient pas même le loisir de manger.
Naye akawaambia, “Njooni wenyewe mahali pa faragha na tupumzike kwa muda.” Watu wengi walikuwa wanakuja na kuondoka, hata hawakupata nafasi ya kula.
32 Et ils s’en allèrent dans un bateau en un lieu désert, à l’écart.
Hivyo wakapanda mashua wakaenda mahali pa faragha peke yao.
33 Et plusieurs les virent qui s’en allaient, et les reconnurent, et accoururent là, à pied, de toutes les villes, et arrivèrent avant eux, [et se rassemblèrent auprès de lui].
Lakini waliwaona wakiondoka na wengi wakawatambua, kwa pamoja walikimbia kwa miguu kutoka miji yote, nao wakafika kabla yao.
34 Et Jésus, étant sorti, vit une grande foule; et il fut ému de compassion envers eux, parce qu’ils étaient comme des brebis qui n’ont pas de berger; et il se mit à leur enseigner beaucoup de choses.
Walipofika pwani, aliona umati mkubwa na akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji. Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35 Et comme l’heure était déjà fort avancée, ses disciples venant à lui, disent: Le lieu est désert et l’heure est déjà fort avancée,
Muda ulipoendelea sana, wanafunzi wakamjia wakamwambia,”Hapa ni mahali pa faragha na muda umeendelea.
36 renvoie-les, afin qu’ils s’en aillent dans les campagnes et les villages d’alentour, et qu’ils s’achètent du pain; car ils n’ont rien à manger.
Uwaage waende miji ya jirani na vijiji ili wakajinunulie chakula.”
37 Et lui, répondant, leur dit: Vous, donnez-leur à manger. Et ils lui disent: Irons-nous acheter pour 200 deniers de pain, et leur donnerons-nous à manger?
Lakini akawajibu akisema, “Wapeni ninyi chakula.” Wakamwambia, “Tunaweza kwenda na kununua mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa wale?”
38 Mais il leur dit: Combien de pains avez-vous? Allez et regardez. Et quand ils le surent, ils disent: Cinq, et deux poissons.
Akawambia,” Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie.” walipopata wakamwambia, “Mikate mitano na samaki wawili.”
39 Et il leur commanda de les faire tous asseoir par troupes sur l’herbe verte.
Akawaamuru watu waketi katika makundi juu ya majani mabichi.
40 Et ils s’assirent en rangs, les uns de 100, et les autres de 50.
Wakawaketisha katika makundi; makundi ya mamia kwa hamsini.
41 Et ayant pris les cinq pains et les deux poissons, et regardant vers le ciel, il bénit, et rompit les pains et les donna à ses disciples, afin qu’ils les mettent devant eux; et il partagea les deux poissons entre tous.
Kisha akachukua mikate mitano na samaki wawili, na kutazama mbinguni, akaibariki kisha akawapa wanafunzi waweke mbele ya umati. Na kisha aligawa samaki wawili kwa watu wote.
42 Et ils mangèrent tous, et furent rassasiés.
Walikula wote hadi wakatosheka.
43 Et ils ramassèrent des morceaux douze paniers pleins, et des restes des poissons.
Walikusanya vipande vya mikate iliyobaki, Vikajaa vikapu kumi na viwili, na pia vipande vya samaki.
44 Et ceux qui avaient mangé les pains étaient 5 000 hommes.
Na walikuwa wanaume elfu tano waliokula mikate.
45 Et aussitôt il contraignit ses disciples de monter dans le bateau, et d’aller devant [lui] à l’autre rive, vers Bethsaïda, tandis qu’il renvoyait la foule.
Mara akawaambia wapande kwenye mashua waende sehemu nyingine, hadi Bethsaida, wakati Yeye akiwaaga makutano.
46 Et leur ayant donné congé, il s’en alla sur une montagne pour prier.
Walipokuwa wamekwisha kuondoka, akaenda mlimani kuomba.
47 Et le soir étant venu, le bateau était au milieu de la mer, et lui, seul à terre.
Kulipokuwa jioni, na mashua yao wakati huo ikiwa katikati ya bahari, naye alikuwa peke yake nchi kavu.
48 Et les voyant se tourmenter à ramer, car le vent leur était contraire, vers la quatrième veille de la nuit, il vient vers eux, marchant sur la mer; et il voulait passer à côté d’eux.
Na aliwaona wakitaabika kupiga makasia kwa sababu upepo uliwazuia. Ilipokaribia asubuhi akawaendea, akitembea juu ya maji, na alitaka kuwapita.
49 Mais eux, le voyant marcher sur la mer, crurent que c’était un fantôme, et ils poussèrent des cris;
Lakini walipomwona anatembea juu ya maji, wakaingiwa na wasiwasi wakidhani ni mzimu hata wakapiga kelele.
50 car ils le virent tous, et ils furent troublés. Et aussitôt il parla avec eux, et leur dit: Ayez bon courage; c’est moi; n’ayez point de peur.
kwa sababu walimwona wakajawa na hofu. Mara akasema nao akawaambia, “Muwe wajasiri! ni mimi! Msiwe na hofu.”
51 Et il monta vers eux dans le bateau, et le vent tomba. Et ils furent excessivement frappés et étonnés en eux-mêmes;
Akaingia ndani ya mashua, na upepo ukaacha kuvuma, nao wakamshangaa kabisa.
52 car ils n’avaient pas été rendus intelligents par les pains, car leur cœur était endurci.
Hivyo hawakuwa wameelewa maana ya ile mikate. Maana akili zao zilikuwa na uelewa mdogo.
53 Et ayant passé à l’autre rive, ils vinrent dans la contrée de Génésareth, et ils abordèrent.
Nao walipovuka ng'ambo, walifika nchi ya Genesareti mashua ikatia nanga.
54 Et comme ils sortaient du bateau, ils le reconnurent aussitôt;
Walipotoka nje ya mashua, mara wakamtambua.
55 et ils coururent par tout le pays d’alentour, et se mirent à apporter de tous côtés dans de petits lits ceux qui se portaient mal, là où ils entendaient dire qu’il était.
Wakakimbia kutangaza katika mkoa mzima na wakaanza kuwaleta wagonjwa kwa machela, kila waliposikia anakuja.
56 Et où que ce soit qu’il entrait, dans les villages, ou dans les villes, ou dans les campagnes, ils plaçaient les infirmes dans les marchés et le priaient de les laisser toucher ne serait-ce que le bord de son vêtement; et tous ceux qui le touchaient étaient guéris.
Popote alipoingia katika vijiji, au mjini, au katika nchi, waliwaweka wagonjwa mahali pa soko, na wakamsihi awaruhusu kugusa pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa waliponywa.

< Marc 6 >