< Marc 14 >

1 Or, deux jours après, c’était la Pâque et les Pains sans levain. Et les principaux sacrificateurs et les scribes cherchaient comment ils pourraient se saisir de lui par ruse, et le faire mourir;
Ilikuwa siku mbili tu baada ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na waandishi walikuwa wakitafuta namna ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
2 car ils disaient: Non pas pendant la fête, de peur qu’il n’y ait du tumulte parmi le peuple.
Kwa kuwa walisema, “Sio wakati huu wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”
3 Et comme il était à Béthanie dans la maison de Simon le lépreux, et qu’il était à table, une femme vint, ayant un vase d’albâtre [plein] d’un parfum de nard pur et de grand prix; et, ayant brisé le vase, elle le répandit sur sa tête.
Wakati Yesu alipokuwa Bethania nyumbani kwa Simoni mkoma, na alipokuwa akielekea mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa na chupa ya marashi ya nardo safi yenye gharama kubwa sana, aliivunja chupa na kuimimina juu ya kichwa chake.
4 Et quelques-uns étaient [là], qui s’indignaient en eux-mêmes et disaient: À quoi bon la perte de ce parfum?
Lakini kulikuwa na baadhi yao waliokasirika. Waliambiana wao kwa wao wakisema, “Ni nini sababu ya upotevu huu?
5 Car ce parfum aurait pu être vendu plus de 300 deniers, et être donné aux pauvres; et ils la reprenaient vivement.
Manukato haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari mia tatu, na wakapewa maskini.” Nao walimkemea.
6 Mais Jésus dit: Laissez-la; pourquoi lui donnez-vous du déplaisir? Elle a fait une bonne œuvre envers moi;
Lakini Yesu alisema, “Mwacheni peke yake. Kwa nini mnamsumbua? Amefanya jambo zuri kwangu.
7 car vous avez toujours les pauvres avec vous, et quand vous voudrez, vous pourrez leur faire du bien; mais moi, vous ne m’avez pas toujours.
Siku zote maskini mnao, na wakati wowote mnapotamani mnaweza kufanya mazuri kwao, lakini hamtakuwa nami wakati wote.
8 Ce qui était en son pouvoir, elle l’a fait; elle a anticipé [le moment] d’oindre mon corps pour ma sépulture.
Amefanya kile anachoweza: ameupaka mwili wangu mafuta kwa ajili ya maziko.
9 Et en vérité, je vous dis: en quelque lieu que cet évangile soit prêché dans le monde entier, on parlera aussi de ce que cette femme a fait, en mémoire d’elle.
Kweli nawaambia, kila mahali injili inapohubiriwa katika ulimwengu wote, kile alichofanya mwanamke huyu kitazungumzwa kwa ukumbusho wake.
10 Et Judas Iscariote, l’un des douze, s’en alla vers les principaux sacrificateurs pour le leur livrer;
Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale kumi na wawili, alikwenda kwa wakuu wa makuhani ili kwamba apate kumkabidhi kwao.
11 et ceux-ci, l’ayant entendu, s’en réjouirent et promirent de lui donner de l’argent; et il cherchait comment il le livrerait commodément.
Wakati wakuu wa Makuhani waliposikia hivyo, walifurahi na wakaahidi kumpa fedha. Alianza kutafuta nafasi ya kumkabidhi kwao.
12 Et le premier jour des pains sans levain, lorsqu’on sacrifiait la pâque, ses disciples lui disent: Où veux-tu que nous allions préparer [ce qu’il faut], afin que tu manges la pâque?
Katika siku ya kwanza ya mkate usiotiwa chachu, wakati walipotoa mwanakondoo wa pasaka, wanafunzi wake walimwambia, “Unataka twende wapi tukaandae ili upate kula mlo wa Pasaka?”
13 Et il envoie deux de ses disciples et leur dit: Allez à la ville; et un homme portant une cruche d’eau viendra à votre rencontre; suivez-le.
Aliwatuma wanafuzi wake wawili na kuwaambia, “Nendeni mjini, na mwanamume ambaye amebeba mtungi ataonana nanyi. Mfuateni.
14 Et où qu’il entre, dites au maître de la maison: Le maître dit: Où est mon logis où je mangerai la pâque avec mes disciples?
Nyumba atakayoingia, mfuateni na mmwambie mwenye nyumba hiyo, 'Mwalimu asema, “Kiko wapi chumba cha wageni mahali nitakapokula Pasaka na wanafunzi wangu?”
15 Et lui vous montrera une grande chambre garnie, toute prête; apprêtez-nous là [ce qu’il faut].
Atawaonesha chumba cha juu kikubwa chenye samani ambacho kiko tayari. Fanyeni maandalizi kwa ajili yetu pale.”
16 Et ses disciples s’en allèrent et entrèrent dans la ville, et trouvèrent [tout] comme il leur avait dit; et ils apprêtèrent la pâque.
Wanafunzi waliondoka wakaenda mjini; walikuta kila kitu kama alivyokuwa amewaambia, na wakaandaa mlo wa Pasaka.
17 Et le soir étant venu, il vient avec les douze.
Wakati ilipokuwa jioni, alikuja na wale Kumi na wawili.
18 Et comme ils étaient à table et qu’ils mangeaient, Jésus dit: En vérité, je vous dis que l’un d’entre vous qui mange avec moi, me livrera.
Na walipokuwa wakiikaribia meza na kula, Yesu alisema, “Kweli nawaambia, mmoja kati yenu anayekula pamoja nami atanisaliti.”
19 Et ils commencèrent à s’attrister et à lui dire l’un après l’autre: Est-ce moi? Et un autre: Est-ce moi?
Wote walisikitika, na mmoja baada ya mwingine walimwambia, “Hakika siyo mimi?”
20 Mais répondant, il leur dit: C’est l’un d’entre les douze qui trempe avec moi au plat.
Yesu alijibu na kuwaambia, “Ni mmoja wa Kumi na wawili kati yenu, mmoja ambaye sasa anachovya tonge katika bakuli pamoja nami.
21 Le fils de l’homme s’en va, selon qu’il est écrit de lui; mais malheur à cet homme par qui le fils de l’homme est livré! Il aurait été bon pour cet homme-là qu’il ne soit pas né.
Kwa kuwa Mwana wa Adamu atakwenda kama vile maandiko yasemavyo juu yake. Lakini ole wake mtu yule ambaye kupitia yeye Mwana wa Adamu atasalitiwa! Ingekuwa vizuri zaidi kwake kama mtu yule asingezaliwa.”
22 Et comme ils mangeaient, Jésus, ayant pris un pain [et] ayant béni, le rompit et le leur donna, et dit: Prenez; ceci est mon corps.
Na walipokuwa wakila, Yesu alichukua mkate, akaubariki, na kuumega. Aliwapa akisema, “Chukueni. Huu ni mwili wangu.”
23 Et ayant pris la coupe [et] ayant rendu grâces, il la leur donna; et ils en burent tous.
Alichukua kikombe, akashukuru, na akawapatia, na wote wakakinywea.
24 Et il leur dit: Ceci est mon sang, le [sang] de la nouvelle alliance, qui est versé pour plusieurs.
Aliwaambia, “Hii ni damu yangu ya agano, damu imwagikayo kwa ajili ya wengi.
25 En vérité, je vous dis que je ne boirai plus du fruit de la vigne, jusqu’à ce jour où je le boirai nouveau dans le royaume de Dieu.
Kweli nawaambia, sitakunywa tena katika zao hili la mzabibu mpaka siku ile nitakapokunywa mpya katika ufalme wa Mungu.”
26 Et ayant chanté une hymne, ils sortirent [et s’en allèrent] à la montagne des Oliviers.
Walipokwisha kuimba wimbo, walikwenda nje katika Mlima wa Mizeituni.
27 Et Jésus leur dit: Vous serez tous scandalisés; car il est écrit: « Je frapperai le berger, et les brebis seront dispersées »;
Yesu aliwaaambia, “Ninyi nyote mtajitenga mbali kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, 'Nitampiga mchungaji na kondoo watatawanyika.'
28 mais après que je serai ressuscité, j’irai devant vous en Galilée.
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia mbele yenu Galilaya.”
29 Et Pierre lui dit: Si même tous étaient scandalisés, je ne le serai pourtant pas, moi.
Petro alimwambia, “Hata kama wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
30 Et Jésus lui dit: En vérité, je te dis qu’aujourd’hui, cette nuit-ci, avant que le coq ait chanté deux fois, toi, tu me renieras trois fois.
Yesu alimwambia, “Kweli nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utakuwa umenikana mara tatu.”
31 Mais [Pierre] disait encore plus fortement: Quand il me faudrait mourir avec toi, je ne te renierai point. Et ils dirent tous aussi la même chose.
Lakini Petro alisema, “Hata itanilazimu kufa pamoja nawe, sitakukana.” Wote walitoa ahadi ile ile.
32 Et ils viennent en un lieu dont le nom était Gethsémané. Et il dit à ses disciples: Asseyez-vous ici, jusqu’à ce que j’aie prié.
Walikuja kwenye eneo lililoitwa Gethsemane, na Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nasali.”
33 Et il prend avec lui Pierre et Jacques et Jean; et il commença à être saisi d’effroi et fort angoissé.
Aliwachukua Petro, Yakobo, na Yohana pamoja naye, akaanza kuhuzunika na kutaabika sana.
34 Et il leur dit: Mon âme est saisie de tristesse jusqu’à la mort; demeurez ici et veillez.
Aliwaambia, “Nafsi yangu ina huzuni sana, hata kufa. Bakini hapa na mkeshe.”
35 Et s’en allant un peu plus avant, il se jeta contre terre, et il priait que, s’il était possible, l’heure passe loin de lui.
Yesu alienda mbele kidogo, akaanguka chini, akaomba, kama ingewezekana, kwamba saa hii ingemwepuka.
36 Et il disait: Abba, Père, toutes choses te sont possibles; fais passer cette coupe loin de moi; toutefois non pas ce que je veux, moi, mais ce que tu veux, toi!
Alisema, “Aba, Baba, Mambo yote kwako yanawezekana. Niondolee kikombe hiki. Lakini siyo kwa mapenzi yangu, bali mapenzi yako.”
37 Et il vient, et les trouve dormant; et il dit à Pierre: Simon, tu dors? Tu n’as pu veiller une heure?
Alirudi na kuwakuta wamelala, na akamwambia Petro, “Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?
38 Veillez et priez, afin que vous n’entriez pas en tentation; l’esprit est prompt, mais la chair est faible.
Kesheni na muombe kwamba msije mkaingia katika majaribu. Hakika roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
39 Et il s’en alla de nouveau, et il pria, disant les mêmes paroles.
Alienda tena na kuomba, na alitumia maneno yaleyale.
40 Et s’en étant retourné, il les trouva de nouveau dormant (car leurs yeux étaient appesantis); et ils ne savaient que lui répondre.
Alikuja tena akawakuta wamelala, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito na hawakujua nini cha kumwambia.
41 Et il vient pour la troisième fois et leur dit: Dormez dorénavant et reposez-vous; il suffit, l’heure est venue; voici, le fils de l’homme est livré entre les mains des pécheurs.
Alikuja mara ya tatu na kuwaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Yatosha! Saa imefika. Tazama! Mwana wa Adamu atasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.
42 Levez-vous, allons; voici, celui qui me livre s’est approché.
Amkeni, twendeni. Tazama, yule anayenisaliti yuko karibu.”
43 Et aussitôt, comme il parlait encore, Judas, l’un des douze, se trouve là, et avec lui une grande foule avec des épées et des bâtons, de la part des principaux sacrificateurs et des scribes et des anciens.
Mara tu alipokuwa bado anaongea, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, alifika, na kundi kubwa kutoka kwa wakuu wa makuhani, waandishi na wazee wenye mapanga na marungu.
44 Et celui qui le livrait leur avait donné un signe, disant: Celui que j’embrasserai, c’est lui; saisissez-le, et emmenez-le sûrement.
Wakati huo msaliti wake alikuwa amewapa ishara, akisema, Yule nitakayembusu, ndiye. Mkamateni na kumpeleka chini ya ulinzi.”
45 Et quand il fut venu, aussitôt s’approchant de lui, il dit: Rabbi, Rabbi! et il l’embrassa avec empressement.
Wakati Yuda alipofika, moja kwa moja alienda kwa Yesu na kusema, “Mwalimu!” Na akambusu.
46 Et ils mirent les mains sur lui et se saisirent de lui.
Kisha wakumtia chini ya ulinzi na kumkamata.
47 Et l’un de ceux qui étaient là présents, ayant tiré l’épée, frappa l’esclave du souverain sacrificateur, et lui emporta l’oreille.
Lakini mmoja kati yao aliyesimama karibu naye alichomoa upanga wake akampiga mtumishi wa kuhani mkuu na kumkata sikio.
48 Et Jésus, répondant, leur dit: Êtes-vous sortis comme après un brigand, avec des épées et des bâtons, pour me prendre?
Yesu aliwaambia, “Mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama mnyang'anyi?
49 J’étais tous les jours avec vous, enseignant dans le temple, et vous ne vous êtes pas saisis de moi; mais c’est afin que les écritures soient accomplies.
Wakati kila siku nilikuwa nanyi na nikifundisha hekaluni, hamkunikamata. Lakini hili limefanyika ili maandiko yatimie.
50 Et tous le laissèrent et s’enfuirent.
Na wale wote waliokuwa na Yesu walimwacha na kukimbia.
51 Et un certain jeune homme le suivit, enveloppé d’une toile de fin lin sur le corps nu; et ils le saisissent;
Kijana mmoja alimfuata, aliyekuwa amevaa shuka tu aliyokuwa amejifunika kumzunguka; walimkamata lakini
52 et, abandonnant la toile de fin lin, il leur échappa tout nu.
aliwaponyoka akaiacha shuka pale akakimbia uchi.
53 Et ils amenèrent Jésus au souverain sacrificateur; et tous les principaux sacrificateurs et les anciens et les scribes s’assemblent auprès de lui.
Walimwongoza Yesu kwa kuhani mkuu. Pale walikusanyika pamoja naye makuhani wakuu wote, wazee, na waandishi.
54 Et Pierre le suivit de loin, jusque dans l’intérieur du palais du souverain sacrificateur, et il s’assit avec les huissiers, et se chauffait près du feu.
Petro naye alimfuata Yesu kwa mbali, kuelekea kwenye ua wa kuhani mkuu. Aliketi pamoja na walinzi, waliokuwa karibu na moto wakiota ili kupata joto.
55 Or les principaux sacrificateurs et tout le sanhédrin cherchaient [quelque] témoignage contre Jésus, pour le faire mourir; et ils n’en trouvaient point.
Wakati huo makuhani wakuu wote na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumwua. Lakini hawakuupata.
56 Car plusieurs portaient de faux témoignages contre lui; et les témoignages ne s’accordaient pas.
Kwa kuwa watu wengi walileta ushuhuda wa uongo dhidi yake, lakini hata ushahidi wao haukufanana.
57 Et quelques-uns s’élevèrent et portèrent un faux témoignage contre lui, disant:
Baadhi walisimama na kuleta ushahidi wa uongo dhidi yake; wakisema,
58 Nous l’avons entendu disant: Moi, je détruirai ce temple qui est fait de main, et en trois jours j’en bâtirai un autre qui ne sera pas fait de main.
“Tulimsikia akisema, 'Nitaliharibu hekalu hili lililotengenezwa kwa mikono, na ndani siku tatu nitajenga lingine lisilotengenezwa kwa mikono.'”
59 Et ainsi non plus leur témoignage ne s’accordait pas.
Lakini hata ushahidi wao haukufanana.
60 Et le souverain sacrificateur, se levant devant tous, interrogea Jésus, disant: Ne réponds-tu rien? De quoi ceux-ci témoignent-ils contre toi?
Kuhani mkuu alisimama katikati yao na akamwuliza Yesu, “Je, huna jibu? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
61 Et il garda le silence, et ne répondit rien. Le souverain sacrificateur l’interrogea encore, et lui dit: Toi, tu es le Christ, le Fils du Béni?
Lakini alikaa kimya na hakujibu chochote. Mara Kuhani mkuu alimwuliza tena, “Je wewe ni Kristo, mwana wa Mbarikiwa?”
62 Et Jésus dit: Je le suis; et vous verrez le fils de l’homme assis à la droite de la puissance, et venant avec les nuées du ciel.
Yesu alisema, “Mimi ndiye. Na utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wa nguvu akija na mawingu ya mbinguni.”
63 Et le souverain sacrificateur, ayant déchiré ses vêtements, dit: Qu’avons-nous encore besoin de témoins?
Kuhani mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Je, bado tunahitaji mashahidi?
64 Vous avez entendu le blasphème: que vous en semble? Et tous le condamnèrent comme méritant la mort.
Mmesikia kufuru. Uamuzi wenu ni upi?” Na wote walimhukumu kama mmoja aliyestahili kifo.
65 Et quelques-uns se mirent à cracher contre lui, et à lui couvrir le visage, et à lui donner des soufflets, et à lui dire: Prophétise. Et les huissiers le frappaient de leurs mains.
Baadhi wakaanza kumtemea mate na kumfunika uso na kumpiga na kumwambia, “Tabiri!” Maafisa walimchukua na kumpiga.
66 Et comme Pierre était en bas, dans la cour, une des servantes du souverain sacrificateur vient,
Na Petro alipokuwa bado yuko chini uani, mtumishi mmoja wa wasichana wa kuhani mkuu alikuja kwake.
67 et, apercevant Pierre qui se chauffait, elle le regarda et dit: Et toi, tu étais avec le Nazarénien Jésus.
Alimwona Petro alipokuwa amesimama akiota moto, na alimtazama kwa kumkaribia. Kisha alisema, “Nawe pia ulikuwa na Mnazareti, Yesu”.
68 Et il le nia, disant: Je ne sais ni n’entends ce que tu dis. Et il sortit dehors dans le vestibule; et le coq chanta.
Lakini alikataa, akisema, “Sijui wala sielewi kuhusu kile unachosema!” Kisha alitoka akaenda nje uani. (Zingatia; Mstari huu, “Na jogoo akawika” haumo kwenye nakala za kale).
69 Et la servante, l’apercevant encore, se mit à dire à ceux qui étaient là: Celui-ci est de ces gens-là.
Lakini mtumishi wa kike pale, alimwona na alianza kuwaambia tena wale ambao walikuwa wamesimama pale, “Mtu huyu ni mmoja wao!”
70 Et il le nia de nouveau. Et encore un peu après, ceux qui étaient là présents dirent à Pierre: Certainement tu es de ces gens-là; car aussi tu es Galiléen.
Lakini alikana tena. Baadaye kidogo wale waliokuwa wamesimama pale walikuwa wakimwambia Petro, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya.”
71 Et il se mit à faire des imprécations et à jurer: Je ne connais pas cet homme dont vous parlez.
Lakini alianza kujiweka mwenyewe chini ya laana na kuapa, “Simjui mtu huyu mnayemsema.”
72 Et le coq chanta pour la seconde fois. Et Pierre se ressouvint de la parole que Jésus lui avait dite: Avant que le coq chante deux fois, tu me renieras trois fois. Et en y pensant, il pleura.
Kisha jogoo aliwika mara ya pili. Kisha Petro alikumbuka maneno ambayo Yesu aliyokuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Na alianguka chini na kulia.

< Marc 14 >