< Juges 20 >

1 Et tous les fils d’Israël sortirent, depuis Dan jusqu’à Beër-Shéba, et le pays de Galaad; et l’assemblée se réunit comme un seul homme, vers l’Éternel, à Mitspa.
Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
2 Et les principaux de tout le peuple, toutes les tribus d’Israël, se présentèrent dans la congrégation du peuple de Dieu, 400 000 hommes de pied, tirant l’épée.
Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
3 Et les fils de Benjamin apprirent que les fils d’Israël étaient montés à Mitspa. Et les fils d’Israël dirent: Dites comment ce mal est arrivé.
(Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
4 Et le Lévite, le mari de la femme tuée, répondit et dit: J’étais venu à Guibha, qui est à Benjamin, moi et ma concubine, pour passer la nuit;
Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
5 et les hommes de Guibha se levèrent contre moi, et entourèrent de nuit la maison, à cause de moi; ils avaient l’intention de me tuer, et ils ont humilié ma concubine, et elle est morte.
Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
6 Et j’ai saisi ma concubine et je l’ai coupée en morceaux, et je l’ai envoyée dans toutes les campagnes de l’héritage d’Israël; car ils ont commis une énormité et une infamie en Israël.
Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
7 Voici, vous tous, fils d’Israël, délibérez, et donnez ici [votre] avis.
Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
8 Et tout le peuple se leva comme un seul homme, disant: Aucun de nous n’ira à sa tente, et aucun de nous ne se retirera dans sa maison;
Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
9 et maintenant, voici ce que nous ferons à Guibha: nous la traiterons selon ce que le sort décidera;
Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
10 et nous prendrons 10 hommes sur 100, de toutes les tribus d’Israël, et 100 sur 1 000, et 1 000 sur 10 000, qui prendront des provisions pour le peuple, afin que, à leur arrivée, on traite Guibha de Benjamin selon toute l’infamie qu’elle a commise en Israël.
Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
11 Et tous les hommes d’Israël se rassemblèrent contre la ville, unis comme un seul homme.
Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
12 Et les tribus d’Israël envoyèrent des hommes dans toutes les familles de Benjamin, disant: Quel est ce mal qui est arrivé au milieu de vous?
Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
13 Et maintenant, livrez-nous ces hommes, fils de Bélial, qui sont à Guibha, afin que nous les fassions mourir et que nous ôtions le mal du milieu d’Israël. Mais [les fils de] Benjamin ne voulurent pas écouter la voix de leurs frères, les fils d’Israël;
Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
14 et les fils de Benjamin se rassemblèrent de leurs villes à Guibha, pour sortir en guerre contre les fils d’Israël.
Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
15 Et en ce jour-là furent dénombrés les fils de Benjamin qui vinrent de leurs villes: 26 000 hommes tirant l’épée, sans les habitants de Guibha, qui furent dénombrés: 700 hommes d’élite.
Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
16 De tout ce peuple, il y avait 700 hommes d’élite qui étaient gauchers; tous ceux-là lançaient avec la fronde une pierre contre un cheveu, et ne manquaient pas.
Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
17 Et les hommes d’Israël furent dénombrés, sauf Benjamin: 400 000 hommes tirant l’épée, tous gens de guerre.
Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
18 Et les fils d’Israël se levèrent, et montèrent à Béthel, et interrogèrent Dieu, et dirent: Qui de nous montera le premier pour livrer bataille aux fils de Benjamin? Et l’Éternel dit: Juda, le premier.
Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
19 Et les fils d’Israël se levèrent le matin, et campèrent contre Guibha.
Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
20 Et les hommes d’Israël sortirent en guerre contre Benjamin, et les hommes d’Israël se rangèrent en bataille contre eux devant Guibha.
Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
21 Et les fils de Benjamin sortirent de Guibha; et en ce jour-là ils étendirent morts par terre 22 000 hommes de ceux d’Israël.
Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
22 Et le peuple, les hommes d’Israël, se fortifièrent, et se rangèrent de nouveau en bataille dans le lieu où ils s’étaient rangés le premier jour.
Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
23 Et les fils d’Israël montèrent, et ils pleurèrent devant l’Éternel jusqu’au soir, et ils interrogèrent l’Éternel, disant: M’approcherai-je de nouveau pour livrer bataille aux fils de Benjamin, mon frère? Et l’Éternel dit: Montez contre lui.
Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
24 Et les fils d’Israël s’avancèrent contre les fils de Benjamin, le second jour;
Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
25 et Benjamin sortit contre eux de Guibha, le second jour; et de nouveau ils étendirent morts par terre 18 000 hommes des fils d’Israël, tous tirant l’épée.
Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
26 Et tous les fils d’Israël et tout le peuple montèrent et vinrent à Béthel, et pleurèrent et demeurèrent là devant l’Éternel, et jeûnèrent ce jour-là jusqu’au soir; et ils offrirent des holocaustes et des sacrifices de prospérités devant l’Éternel.
Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
27 Et les fils d’Israël interrogèrent l’Éternel (et l’arche de l’alliance de Dieu était là, en ces jours;
Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
28 et Phinées, fils d’Éléazar, fils d’Aaron, se tenait devant elle, en ces jours), et ils dirent: Sortirai-je encore de nouveau pour livrer bataille aux fils de Benjamin, mon frère, ou cesserai-je? Et l’Éternel dit: Montez; car demain je les livrerai en ta main.
na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
29 Et Israël plaça des embuscades contre Guibha, tout autour.
Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
30 Et les fils d’Israël montèrent, le troisième jour, contre les fils de Benjamin; et ils se rangèrent contre Guibha, comme les autres fois.
Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
31 Et les fils de Benjamin sortirent à la rencontre du peuple; ils furent attirés loin de la ville, et commencèrent à frapper quelques-uns du peuple, qui furent tués comme les autres fois, environ 30 hommes d’Israël, sur les routes, dont l’une monte à Béthel, et l’autre à Guibha, par la campagne.
Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
32 Et les fils de Benjamin dirent: Ils sont battus devant nous comme la première fois. Et les fils d’Israël dirent: Fuyons, et nous les attirerons loin de la ville, sur les routes.
Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
33 Et tous les hommes d’Israël se levèrent de leur lieu, et se rangèrent à Baal-Thamar; et l’embuscade d’Israël s’élança de son lieu, de la prairie de Guibha.
Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
34 Et 10 000 hommes d’élite de tout Israël vinrent contre Guibha, et la bataille fut rude; et ceux [de Benjamin] ne savaient pas que le mal les atteignait.
Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
35 Et l’Éternel battit Benjamin devant Israël, et les fils d’Israël étendirent morts en ce jour-là 25 100 hommes de Benjamin, tous tirant l’épée.
Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
36 Et les fils de Benjamin virent qu’ils étaient battus. – Or les hommes d’Israël firent place à ceux de Benjamin, car ils se confiaient en l’embuscade qu’ils avaient placée contre Guibha.
Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
37 Et l’embuscade se hâta, et se jeta sur Guibha; et l’embuscade se porta en avant, et frappa toute la ville par le tranchant de l’épée.
Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
38 Et le signal convenu entre les hommes d’Israël et l’embuscade était qu’ils fassent monter de la ville une épaisse colonne de fumée.
Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
39 Et les hommes d’Israël avaient tourné visage dans la bataille, et Benjamin avait commencé de frapper à mort une trentaine d’hommes parmi les hommes d’Israël, car ils disaient: Certainement il est complètement battu devant nous comme dans la première bataille.
ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
40 Et quand l’incendie commença à monter de la ville comme une colonne de fumée, Benjamin se tourna en arrière, et voici, toute la ville montait [en fumée] vers les cieux.
Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
41 Et les hommes d’Israël tournèrent visage: et les hommes de Benjamin furent épouvantés; car ils virent que le mal les avait atteints.
Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
42 Et ils tournèrent le dos devant les hommes d’Israël, vers le chemin du désert, et la bataille les serra de près. Et ceux qui sortirent des villes les détruisirent au milieu d’eux.
Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
43 Ils environnèrent Benjamin, le poursuivirent, le foulèrent aux pieds là où il voulait se reposer, jusque vis-à-vis de Guibha, vers le soleil levant.
Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
44 Et il tomba de Benjamin 18 000 hommes, tous hommes vaillants.
Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
45 Et ils tournèrent le dos, et s’enfuirent au désert, vers le rocher de Rimmon; et [les Israélites] en grappillèrent sur les routes 5 000 hommes, et ils les serrèrent de près en les poursuivant jusqu’à Guidhom, et en frappèrent 2 000 hommes.
Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
46 Et tous ceux de Benjamin qui tombèrent en ce jour-là, furent 25 000 hommes tirant l’épée, tous hommes vaillants.
Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
47 Et 600 hommes tournèrent le dos et s’enfuirent au désert, vers le rocher de Rimmon, et ils demeurèrent au rocher de Rimmon quatre mois.
Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
48 Et les hommes d’Israël retournèrent vers les fils de Benjamin et les frappèrent par le tranchant de l’épée, et les hommes de chaque ville, et les bêtes, et tout ce qui fut trouvé; même toutes les villes qu’ils rencontrèrent, ils les livrèrent au feu.
Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.

< Juges 20 >