< Josué 21 >
1 Et les chefs des pères des Lévites s’approchèrent d’Éléazar, le sacrificateur, et de Josué, fils de Nun, et des chefs des pères des tribus des fils d’Israël,
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2 et leur parlèrent à Silo, dans le pays de Canaan, disant: L’Éternel a commandé par Moïse qu’on nous donne des villes pour y habiter, et leurs banlieues pour nos bêtes.
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 Et les fils d’Israël donnèrent de leur héritage aux Lévites, selon le commandement de l’Éternel, ces villes-ci, avec leurs banlieues:
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 Et le lot échut aux familles des Kehathites. Et il y eut, par le sort, pour les fils d’Aaron, le sacrificateur, d’entre les Lévites, 13 villes de la tribu de Juda, et de la tribu des Siméonites, et de la tribu de Benjamin;
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 et pour les autres fils de Kehath, dix villes des familles de la tribu d’Éphraïm, et de la tribu de Dan, et de la demi-tribu de Manassé, par le sort;
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 et pour les fils de Guershon, 13 villes des familles de la tribu d’Issacar, et de la tribu d’Aser, et de la tribu de Nephthali, et de la demi-tribu de Manassé, en Basan, par le sort;
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 [et] pour les fils de Merari, selon leurs familles, douze villes de la tribu de Ruben, et de la tribu de Gad, et de la tribu de Zabulon.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 Et les fils d’Israël donnèrent aux Lévites, par le sort, ces villes-là et leurs banlieues, comme l’Éternel l’avait commandé par Moïse.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 Et ils donnèrent, de la tribu des fils de Juda et de la tribu des fils de Siméon, ces villes-ci, qu’on nomma par leurs noms,
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 et qui furent pour les fils d’Aaron, des familles des Kehathites, d’entre les fils de Lévi; car le premier lot fut pour eux.
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 On leur donna: Kiriath-Arba ([Arba était] père d’Anak), c’est Hébron, dans la montagne de Juda, et sa banlieue autour d’elle.
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 Mais la campagne de la ville et ses hameaux, ils les donnèrent à Caleb, fils de Jephunné, pour sa possession.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 Et ils donnèrent aux fils d’Aaron, le sacrificateur, la ville de refuge pour l’homicide: Hébron et sa banlieue; et Libna et sa banlieue,
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 et Jatthir et sa banlieue, et Eshtemoa et sa banlieue,
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 et Holon et sa banlieue, et Debir et sa banlieue,
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 et Aïn et sa banlieue, et Jutta et sa banlieue, [et] Beth-Shémesh et sa banlieue, neuf villes de ces deux tribus-là;
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 et de la tribu de Benjamin: Gabaon et sa banlieue, Guéba et sa banlieue,
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
18 Anathoth et sa banlieue, et Almon et sa banlieue, quatre villes.
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 Toutes les villes des fils d’Aaron, sacrificateurs: 13 villes et leurs banlieues.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 Et pour les familles des fils de Kehath, les autres Lévites d’entre les fils de Kehath, les villes de leur lot furent de la tribu d’Éphraïm.
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 Ils leur donnèrent la ville de refuge pour l’homicide: Sichem et sa banlieue, dans la montagne d’Éphraïm; et Guézer et sa banlieue,
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 et Kibtsaïm et sa banlieue, et Beth-Horon et sa banlieue, quatre villes;
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 et de la tribu de Dan: Eltheké et sa banlieue, Guibbethon et sa banlieue,
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 Ajalon et sa banlieue, Gath-Rimmon et sa banlieue, quatre villes;
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 et de la demi-tribu de Manassé: Thaanac et sa banlieue, et Gath-Rimmon et sa banlieue, deux villes.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 En tout dix villes et leurs banlieues, pour les familles des autres fils de Kehath.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 Et pour les fils de Guershon, d’entre les familles des Lévites, il y eut, de la demi-tribu de Manassé, la ville de refuge pour l’homicide: Golan, en Basan, et sa banlieue; et Beeshtra et sa banlieue, deux villes;
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 et de la tribu d’Issacar: Kishion et sa banlieue, Dabrath et sa banlieue,
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 Jarmuth et sa banlieue, En-Gannim et sa banlieue, quatre villes;
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 et de la tribu d’Aser: Misheal et sa banlieue, Abdon et sa banlieue,
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 Helkath et sa banlieue, et Rehob et sa banlieue, quatre villes;
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 et de la tribu de Nephthali, la ville de refuge pour l’homicide: Kédesh, en Galilée, et sa banlieue; et Hammoth-Dor et sa banlieue, et Karthan et sa banlieue, trois villes.
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 Toutes les villes des Guershonites, selon leurs familles: 13 villes et leurs banlieues.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 Et pour les familles des fils de Merari, les autres Lévites, [on donna], de la tribu de Zabulon: Jokneam et sa banlieue, Kartha et sa banlieue,
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 Dimna et sa banlieue, Nahalal et sa banlieue, quatre villes;
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
36 et de la tribu de Ruben: Bétser et sa banlieue, et Jahtsa et sa banlieue,
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
37 Kedémoth et sa banlieue, et Méphaath et sa banlieue, quatre villes;
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
38 et de la tribu de Gad, la ville de refuge pour l’homicide: Ramoth, en Galaad, et sa banlieue; et Mahanaïm et sa banlieue,
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
39 Hesbon et sa banlieue, Jahzer et sa banlieue: en tout, quatre villes.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 Toutes ces villes étaient aux fils de Merari, selon leurs familles, – le reste des familles des Lévites; leur lot fut de douze villes.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 Toutes les villes des Lévites, au milieu de la possession des fils d’Israël: 48 villes et leurs banlieues.
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 Chacune de ces villes avait sa banlieue autour d’elle; il en était ainsi pour toutes ces villes.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 Et l’Éternel donna à Israël tout le pays qu’il avait juré de donner à leurs pères; et ils le possédèrent, et y habitèrent.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 Et l’Éternel leur donna du repos à l’entour, selon tout ce qu’il avait juré à leurs pères; et, de tous leurs ennemis, pas un homme ne tint devant eux; l’Éternel livra tous leurs ennemis entre leurs mains.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 Il ne tomba pas un mot de toutes les bonnes paroles que l’Éternel avait dites à la maison d’Israël: tout arriva.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.