< Josué 16 >

1 Et le lot échut aux fils de Joseph depuis le Jourdain de Jéricho, jusqu’aux eaux de Jéricho, vers le levant, [vers] le désert qui monte de Jéricho à la montagne de Béthel.
Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
2 Et [la frontière] sortait de Béthel vers Luz, et passait vers la frontière de l’Arkite à Ataroth,
Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
3 et elle descendait vers l’occident, à la frontière des Japhlétiens, jusqu’à la frontière de Beth-Horon la basse, et jusqu’à Guézer, et aboutissait à la mer.
ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
4 Et les fils de Joseph, Manassé et Éphraïm, eurent [cela pour] héritage.
Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
5 Et le territoire des fils d’Éphraïm fut selon leurs familles: la frontière de leur héritage vers le levant était Ataroth-Addar, jusqu’à Beth-Horon la haute.
Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
6 Et la frontière sortait à l’occident vers Micmethath, au nord; et la frontière tournait vers l’orient, jusqu’à Thaanath-Silo, et la dépassait vers l’orient, vers Janokha,
na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
7 et descendait de Janokha à Ataroth et à Naaratha, et touchait à Jéricho, et aboutissait au Jourdain.
Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
8 Depuis Tappuakh la frontière allait vers l’occident, au torrent de Kana, et aboutissait à la mer. Ce fut là l’héritage de la tribu des fils d’Éphraïm, selon leurs familles,
Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
9 avec les villes qui furent séparées pour les fils d’Éphraïm, au milieu de l’héritage des fils de Manassé, toutes ces villes et leurs hameaux.
Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
10 Mais ils ne dépossédèrent pas le Cananéen qui habitait à Guézer; et le Cananéen a habité au milieu d’Éphraïm jusqu’à ce jour; et il a été asservi au tribut.
Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.

< Josué 16 >