< Jean 7 >

1 Et après ces choses, Jésus se tenait en Galilée, car il ne voulait pas se tenir en Judée, parce que les Juifs cherchaient à le faire mourir.
Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2 Or la fête des Juifs, celle des tabernacles, était proche.
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 Ses frères lui dirent donc: Pars d’ici et va en Judée, afin que tes disciples aussi voient les œuvres que tu fais;
Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4 car nul ne fait quelque chose en secret et ne cherche à être lui-même publiquement connu; si tu fais ces choses, montre-toi au monde toi-même.
Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
5 Car ses frères ne croyaient pas en lui non plus.
(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6 Jésus donc leur dit: Mon temps n’est pas encore venu, mais votre temps est toujours prêt.
Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7 Le monde ne peut pas vous haïr; mais il me hait, parce que moi je rends témoignage de lui, que ses œuvres sont mauvaises.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8 Vous, montez à cette fête; moi, je ne monte pas à cette fête, car mon temps n’est pas encore accompli.
Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
9 Leur ayant dit ces choses, il demeura en Galilée.
Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10 Mais lorsque ses frères furent montés, alors lui aussi monta à la fête, non pas publiquement, mais comme en secret.
Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11 Les Juifs donc le cherchaient à la fête et disaient: Où est cet [homme]?
Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
12 Et il y avait une grande rumeur à son sujet parmi les foules. Les uns disaient: Il est homme de bien. D’autres disaient: Non, mais il séduit la foule.
Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
13 Toutefois personne ne parlait ouvertement de lui, par crainte des Juifs.
Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14 Mais, comme on était déjà au milieu de la fête, Jésus monta au temple, et il enseignait.
Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15 Les Juifs donc s’étonnaient, disant: Comment celui-ci connaît-il les lettres, vu qu’il ne [les] a point apprises?
Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
16 Jésus donc leur répondit et dit: Ma doctrine n’est pas mienne, mais de celui qui m’a envoyé.
Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 Si quelqu’un veut faire sa volonté, il connaîtra de la doctrine si elle est de Dieu, ou si moi je parle de par moi-même.
Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18 Celui qui parle de par lui-même cherche sa propre gloire; mais celui qui cherche la gloire de celui qui l’a envoyé, celui-là est vrai, et il n’y a point d’injustice en lui.
Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19 Moïse ne vous a-t-il pas donné la loi? Et nul d’entre vous n’observe la loi. Pourquoi cherchez-vous à me faire mourir?
Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 La foule répondit et dit: Tu as un démon; qui cherche à te faire mourir?
Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
21 Jésus répondit et leur dit: J’ai fait une œuvre, et vous vous étonnez tous.
Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22 C’est pourquoi Moïse vous a donné la circoncision (non qu’elle soit de Moïse, mais elle est des pères), et vous circoncisez un homme en un jour de sabbat.
Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23 Si un homme reçoit la circoncision en un jour de sabbat, afin que la loi de Moïse ne soit pas violée, êtes-vous irrités contre moi de ce que j’ai guéri un homme tout entier en un jour de sabbat?
Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24 Ne jugez pas sur l’apparence, mais portez un jugement juste.
Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
25 Quelques-uns donc de ceux de Jérusalem disaient: N’est-ce pas celui qu’ils cherchent à faire mourir?
Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26 Et voici, il parle librement, et ils ne lui disent rien: les chefs auraient-ils vraiment reconnu que celui-ci est le Christ?
Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27 Mais nous connaissons celui-ci, [et nous savons] d’où il est; mais lorsque le Christ viendra, personne ne sait d’où il est.
Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
28 Jésus donc criait dans le temple, enseignant et disant: Et vous me connaissez, et vous savez d’où je suis: et je ne suis pas venu de par moi-même, mais celui qui m’a envoyé est véritable, et vous ne le connaissez pas.
Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29 Moi, je le connais, car je viens de lui, et c’est lui qui m’a envoyé.
Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
30 Ils cherchaient donc à le prendre; et personne ne mit la main sur lui, parce que son heure n’était pas encore venue.
Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31 Et plusieurs d’entre la foule crurent en lui, et disaient: Le Christ, quand il sera venu, fera-t-il plus de miracles que celui-ci n’en a fait?
Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
32 Les pharisiens entendirent la foule murmurant ces choses de lui; et les pharisiens et les principaux sacrificateurs envoyèrent des huissiers pour le prendre.
Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33 Jésus donc dit: Je suis encore pour un peu de temps avec vous, et je m’en vais à celui qui m’a envoyé.
Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34 Vous me chercherez, et vous ne me trouverez pas; et là où moi je serai, vous, vous ne pouvez venir.
Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
35 Les Juifs donc dirent entre eux: Où celui-ci va-t-il aller que nous ne le trouverons pas? Va-t-il aller à la dispersion [au milieu] des Grecs, et enseigner les Grecs?
Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36 Quelle est cette parole qu’il a dite: Vous me chercherez, et vous ne me trouverez pas; et là où moi je serai, vous, vous ne pouvez venir?
Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
37 Et en la dernière journée, la grande journée de la fête, Jésus se tint là et cria, disant: Si quelqu’un a soif, qu’il vienne à moi, et qu’il boive.
Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38 Celui qui croit en moi, selon ce qu’a dit l’écriture, des fleuves d’eau vive couleront de son ventre.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
39 (Or il disait cela de l’Esprit qu’allaient recevoir ceux qui croyaient en lui; car l’Esprit n’était pas encore, parce que Jésus n’avait pas encore été glorifié.)
(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40 Des gens de la foule donc, ayant entendu cette parole, disaient: Celui-ci est véritablement le prophète.
Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
41 D’autres disaient: Celui-ci est le Christ. D’autres disaient: Le Christ vient-il donc de Galilée?
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42 L’écriture n’a-t-elle pas dit que le Christ vient de la semence de David et de la bourgade de Bethléhem, où était David?
Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
43 Il y eut donc de la division dans la foule à cause de lui.
Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44 Et quelques-uns d’entre eux voulaient le prendre; mais personne ne mit les mains sur lui.
Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45 Les huissiers donc s’en vinrent vers les principaux sacrificateurs et les pharisiens; et ceux-ci leur dirent: Pourquoi ne l’avez-vous pas amené?
Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
46 Les huissiers répondirent: Jamais homme ne parla comme cet homme.
Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
47 Les pharisiens donc leur répondirent: Et vous aussi, êtes-vous séduits?
Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 Aucun d’entre les chefs ou d’entre les pharisiens, a-t-il cru en lui?
Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49 Mais cette foule qui ne connaît pas la loi est maudite.
Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
50 Nicodème, qui était l’un d’entre eux, leur dit:
Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51 Notre loi juge-t-elle l’homme avant de l’avoir entendu et d’avoir connu ce qu’il fait?
“Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
52 Ils répondirent et lui dirent: Et toi, es-tu aussi de Galilée? Enquiers-toi, et vois qu’un prophète n’est pas suscité de Galilée.
Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
53 Et chacun s’en alla dans sa maison.
Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;

< Jean 7 >