< Jean 11 >
1 Or il y avait un certain homme malade, Lazare, de Béthanie, du village de Marie et de Marthe sa sœur.
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
2 (Et c’était la Marie qui oignit le Seigneur d’un parfum et qui lui essuya les pieds avec ses cheveux, de laquelle Lazare, le malade, était le frère.)
Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
3 Les sœurs donc envoyèrent vers lui, disant: Seigneur, voici, celui que tu aimes est malade.
Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
4 Jésus, l’ayant entendu, dit: Cette maladie n’est pas à la mort, mais pour la gloire de Dieu, afin que le Fils de Dieu soit glorifié par elle.
Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
5 Or Jésus aimait Marthe, et sa sœur, et Lazare.
Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
6 Après donc qu’il eut entendu que Lazare était malade, il demeura encore deux jours au lieu où il était.
baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 Puis après cela, il dit à ses disciples: Retournons en Judée.
Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
8 Les disciples lui disent: Rabbi, les Juifs cherchaient tout à l’heure à te lapider, et tu y vas encore!
Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
9 Jésus répondit: N’y a-t-il pas douze heures au jour? Si quelqu’un marche de jour, il ne bronche pas, car il voit la lumière de ce monde;
Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
10 mais si quelqu’un marche de nuit, il bronche, car la lumière n’est pas en lui.
Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
11 Il dit ces choses; et après cela il leur dit: Lazare, notre ami, s’est endormi; mais je vais pour l’éveiller.
Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
12 Les disciples donc lui dirent: Seigneur, s’il s’est endormi, il sera guéri.
Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
13 Or Jésus avait parlé de sa mort; mais eux pensaient qu’il avait parlé du dormir du sommeil.
Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
14 Jésus leur dit donc alors ouvertement: Lazare est mort;
Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
15 et je me réjouis, à cause de vous, de ce que je n’étais pas là, afin que vous croyiez. Mais allons vers lui.
Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
16 Thomas donc, appelé Didyme, dit à ses condisciples: Allons-y, nous aussi, afin que nous mourions avec lui.
Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
17 Jésus étant donc arrivé trouva qu’il était déjà depuis quatre jours dans le sépulcre.
Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
18 Or Béthanie était près de Jérusalem, à une distance d’environ 15 stades.
Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
19 Et plusieurs d’entre les Juifs étaient venus auprès de Marthe et de Marie, pour les consoler au sujet de leur frère.
na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
20 Marthe donc, quand elle eut entendu dire que Jésus venait, alla au-devant de lui; mais Marie se tenait assise dans la maison.
Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
21 Marthe donc dit à Jésus: Seigneur, si tu avais été ici mon frère ne serait pas mort;
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
22 [mais] même maintenant je sais que tout ce que tu demanderas à Dieu, Dieu te le donnera.
Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Jésus lui dit: Ton frère ressuscitera.
Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
24 Marthe lui dit: Je sais qu’il ressuscitera en la résurrection, au dernier jour.
Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
25 Jésus lui dit: Moi, je suis la résurrection et la vie: celui qui croit en moi, encore qu’il soit mort, vivra;
Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
26 et quiconque vit, et croit en moi, ne mourra point, à jamais. Crois-tu cela? (aiōn )
na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn )
27 Elle lui dit: Oui, Seigneur, moi je crois que tu es le Christ, le Fils de Dieu, qui vient dans le monde.
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
28 Et ayant dit cela, elle s’en alla et appela secrètement Marie, sa sœur, disant: Le maître est venu, et il t’appelle.
Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
29 Celle-ci, aussitôt qu’elle l’eut entendu, se lève promptement et s’en vient à lui.
Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
30 (Or Jésus n’était pas encore arrivé dans le village; mais il était au lieu où Marthe l’avait rencontré.)
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
31 Les Juifs donc qui étaient avec Marie dans la maison et qui la consolaient, ayant vu que Marie s’était levée promptement et était sortie, la suivirent, disant: Elle s’en va au sépulcre pour y pleurer.
Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
32 Marie donc, quand elle fut venue là où était Jésus, et qu’elle l’eut vu, se jeta à ses pieds, lui disant: Seigneur, si tu avais été ici, mon frère ne serait pas mort.
Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
33 Jésus donc, quand il la vit pleurer, et les Juifs qui étaient venus avec elle, pleurer, frémit en [son] esprit, et se troubla,
Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
34 et dit: Où l’avez-vous mis? Ils lui disent: Seigneur, viens et vois.
Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
36 Les Juifs donc dirent: Voyez comme il l’affectionnait.
Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
37 Mais quelques-uns d’entre eux dirent: Celui-ci, qui a ouvert les yeux de l’aveugle, n’aurait-il pas pu faire aussi que cet homme ne meure pas?
Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
38 Jésus donc, frémissant encore en lui-même, vient au sépulcre (or c’était une grotte, et il y avait une pierre dessus ).
Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
39 Jésus dit: Ôtez la pierre. Marthe, la sœur du mort, lui dit: Seigneur, il sent déjà, car il est [là] depuis quatre jours.
Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
40 Jésus lui dit: Ne t’ai-je pas dit que, si tu crois, tu verras la gloire de Dieu?
Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
41 Ils ôtèrent donc la pierre. Et Jésus leva les yeux en haut et dit: Père, je te rends grâces de ce que tu m’as entendu.
Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
42 Or moi je savais que tu m’entends toujours; mais je l’ai dit à cause de la foule qui est autour de moi, afin qu’ils croient que toi, tu m’as envoyé.
Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
43 Et ayant dit ces choses, il cria à haute voix: Lazare, sors dehors!
Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
44 Et le mort sortit, ayant les pieds et les mains liés de bandes; et son visage était enveloppé d’un suaire. Jésus leur dit: Déliez-le, et laissez-le aller.
Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
45 Plusieurs donc d’entre les Juifs qui étaient venus auprès de Marie, et qui avaient vu ce que Jésus avait fait, crurent en lui;
Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
46 mais quelques-uns d’entre eux s’en allèrent auprès des pharisiens et leur dirent ce que Jésus avait fait.
Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.
47 Les principaux sacrificateurs et les pharisiens donc assemblèrent un sanhédrin, et dirent: Que faisons-nous? car cet homme fait beaucoup de miracles.
Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
48 Si nous le laissons ainsi [faire], tous croiront en lui, et les Romains viendront, et ôteront et notre lieu et notre nation.
Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
49 Et l’un d’entre eux, [appelé] Caïphe, qui était souverain sacrificateur cette année-là, leur dit: Vous ne savez rien,
Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
50 ni ne considérez qu’il nous est avantageux qu’un seul homme meure pour le peuple et que la nation entière ne périsse pas.
Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
51 Or il ne dit pas cela de lui-même; mais étant souverain sacrificateur cette année-là, il prophétisa que Jésus allait mourir pour la nation;
Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi,
52 et non pas seulement pour la nation, mais aussi pour rassembler en un les enfants de Dieu dispersés.
wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
53 Depuis ce jour-là donc, ils consultèrent [ensemble] pour le faire mourir.
Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.
54 Jésus donc ne marcha plus ouvertement parmi les Juifs; mais il s’en alla de là dans la contrée qui est près du désert, en une ville appelée Éphraïm; et il séjourna là avec les disciples.
Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
55 Or la Pâque des Juifs était proche, et plusieurs montèrent de la campagne à Jérusalem, avant la Pâque, afin de se purifier.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase.
56 Ils cherchaient donc Jésus, et se disaient l’un à l’autre, comme ils étaient dans le temple: Que vous semble? [Pensez-vous] qu’il ne viendra point à la fête?
Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?
57 Or les principaux sacrificateurs et les pharisiens avaient donné ordre que si quelqu’un savait où il était, il le déclare, afin qu’on le prenne.
Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.