< Job 8 >

1 Et Bildad, le Shukhite, répondit et dit:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 Jusques à quand diras-tu ces choses, et les paroles de ta bouche seront-elles un vent impétueux?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Est-ce que Dieu pervertit le droit? Le Tout-puissant pervertira-t-il la justice?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 Si tes fils ont péché contre lui, il les a aussi livrés en la main de leur transgression.
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 Si tu recherches Dieu et que tu supplies le Tout-puissant,
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 Si tu es pur et droit, certainement il se réveillera maintenant en ta faveur, et rendra prospère la demeure de ta justice;
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 Et ton commencement aura été petit, mais ta fin sera très grande.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 Car interroge, je te prie, la génération précédente, et sois attentif aux recherches de leurs pères;
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 Car nous sommes d’hier et nous n’avons pas de connaissance, car nos jours sont une ombre sur la terre.
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 Ceux-là ne t’enseigneront-ils pas, ne te parleront-ils pas, et de leurs cœurs ne tireront-ils pas des paroles?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Le papyrus s’élève-t-il où il n’y a pas de marais? Le roseau croît-il sans eau?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 Encore dans sa verdeur, sans qu’on l’ait arraché, avant toute herbe il sèche.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Tels sont les sentiers de tous ceux qui oublient Dieu; et l’attente de l’impie périra;
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 Son assurance sera retranchée, et sa confiance sera une toile d’araignée:
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 Il s’appuiera sur sa maison, et elle ne tiendra pas; il s’y cramponnera, et elle ne restera pas debout.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 Il est verdoyant devant le soleil, et son rameau s’étend sur son jardin;
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 Ses racines s’entrelacent dans un tas de rocaille, il voit la demeure des pierres;
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 S’Il l’ôte de sa place, celle-ci le désavouera: Je ne t’ai pas vu!
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Telles sont les délices de ses voies; et de la poussière, d’autres germeront.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Voici, Dieu ne méprisera pas l’homme parfait, et ne soutiendra pas les mains des méchants:
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 Tandis qu’il remplira ta bouche de rire et tes lèvres de chants de joie,
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 Ceux qui te haïssent seront revêtus de honte, et la tente des méchants ne sera plus.
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.

< Job 8 >