< Job 6 >
1 Et Job répondit et dit:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Oh! si mon chagrin était bien pesé, et si on mettait toute ma calamité dans la balance!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 Car maintenant elle pèserait plus que le sable des mers; c’est pourquoi mes paroles sont outrées;
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Car les flèches du Tout-puissant sont en moi, leur venin boit mon esprit; les frayeurs de Dieu se rangent en bataille contre moi.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 L’âne sauvage brait-il auprès de l’herbe? Le bœuf mugit-il auprès de son fourrage?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 Ce qui est insipide, le mange-t-on sans sel? Y a-t-il de la saveur dans le blanc d’un œuf?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 Ce que mon âme refusait de toucher est comme ma dégoûtante nourriture.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 Oh! si ma demande s’accomplissait, et si Dieu m’accordait mon désir,
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 S’il plaisait à Dieu de m’écraser, de lâcher sa main et de me retrancher!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 Alors il y aurait encore pour moi une consolation, et, dans la douleur qui ne m’épargne pas, je me réjouirais de ce que je n’ai pas renié les paroles du Saint.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 Quelle est ma force pour que j’attende, et quelle est ma fin pour que je patiente?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 Ma force est-elle la force des pierres? Ma chair est-elle d’airain?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 N’est-ce pas qu’il n’y a point de secours en moi, et que toute capacité est chassée loin de moi?
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 À celui qui est défaillant est due la miséricorde de la part de son ami, sinon il abandonnera la crainte du Tout-puissant.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 Mes frères m’ont trahi comme un torrent, comme le lit des torrents qui passent,
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 Qui sont troubles à cause des glaces, dans lesquels la neige se cache;
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 Au temps où ils se resserrent ils tarissent, quand la chaleur les frappe ils disparaissent de leur lieu:
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 Ils serpentent dans les sentiers de leur cours, ils s’en vont dans le désert, et périssent.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 Les caravanes de Théma les cherchaient du regard, les voyageurs de Sheba s’attendaient à eux;
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 Ils ont été honteux de leur confiance; ils sont venus là, et ont été confondus.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 De même maintenant vous n’êtes rien; vous avez vu un objet de terreur, et vous vous êtes effrayés.
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 Ai-je dit: Donnez-moi, et de votre richesse faites-moi des présents,
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 Et délivrez-moi de la main de l’oppresseur, et rachetez-moi de la main des terribles?
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 Enseignez-moi, et je me tairai; et faites-moi comprendre en quoi je me trompe.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 Combien sont puissantes les paroles justes! Mais la censure de votre part que reprend-elle?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Songez-vous à censurer des discours? Mais les paroles d’un désespéré ne sont faites que pour le vent.
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 Certes, vous tombez sur l’orphelin, et vous creusez [une fosse] pour votre ami.
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Et maintenant, si vous voulez, regardez-moi; vous mentirais-je donc en face?
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Revenez, je vous prie; qu’il n’y ait pas d’injustice; oui, revenez encore: ma justice sera là.
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 Y a-t-il de l’iniquité en ma langue? Mon palais ne discernerait-il pas la méchanceté?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?