< Job 38 >
1 Et l’Éternel répondit à Job du milieu du tourbillon, et dit:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Qui est celui-ci qui obscurcit le conseil par des discours sans connaissance?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Ceins tes reins comme un homme, et je t’interrogerai et tu m’instruiras!
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Où étais-tu quand j’ai fondé la terre? Déclare-le-moi, si tu as de l’intelligence.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Qui lui a établi sa mesure, – si tu le sais? Ou qui a étendu le cordeau sur elle?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Sur quoi ses bases sont-elles assises, ou qui a placé sa pierre angulaire,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 Quand les étoiles du matin chantaient ensemble, et que tous les fils de Dieu éclataient de joie?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Et qui a renfermé la mer dans des portes, quand elle rompit [les bornes] et sortit de la matrice,
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 Quand je fis de la nuée son vêtement, et de l’obscurité ses langes;
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 Quand je lui découpai ses limites et lui mis des barres et des portes,
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 Et que je dis: Tu viendras jusqu’ici et tu n’iras pas plus loin, et ici s’arrêtera l’orgueil de tes flots?
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 As-tu, de ta vie, commandé au matin? As-tu montré à l’aube du jour sa place,
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 Pour qu’elle saisisse les bords de la terre, et que les méchants en soient secoués?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Elle se change comme l’argile d’un sceau, et [toutes choses] se présentent parées comme d’un vêtement;
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Et leur lumière est ôtée aux méchants, et le bras levé est cassé.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Es-tu allé aux sources de la mer, et t’es-tu promené dans les profondeurs de l’abîme?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Les portes de la mort se sont-elles découvertes à toi? Et as-tu vu les portes de l’ombre de la mort?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Ton regard a-t-il pénétré jusque dans les vastes espaces de la terre? Dis-le, si tu connais tout cela.
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Où est le chemin vers le séjour de la lumière? et les ténèbres, où est leur place?
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 Pour que tu les prennes à leur limite, et que tu connaisses les sentiers de leur maison?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Tu le sais, car tu étais né alors, et le nombre de tes jours est grand!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Es-tu allé aux trésors de la neige, et as-tu vu les trésors de la grêle,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 Que j’ai mis en réserve pour le temps de la détresse, pour le jour du combat et de la guerre?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Par quel chemin se distribue la lumière, et le vent d’orient se répand-il sur la terre?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Qui a découpé des canaux aux torrents de pluie, et un chemin à l’éclair des tonnerres,
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 Pour faire pleuvoir sur une terre où il n’y a personne, sur le désert où il n’y a pas d’hommes;
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 Pour rassasier les lieux désolés et déserts, pour faire germer les pousses de l’herbe?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 La pluie a-t-elle un père? ou qui engendre les gouttes de la rosée?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Du sein de qui sort la glace? et le frimas des cieux, qui l’enfante?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Devenues pierre, les eaux se cachent, et la surface de l’abîme se prend.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Peux-tu serrer les liens des Pléiades, ou détacher les cordes d’Orion?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Fais-tu sortir les signes du zodiaque en leurs saisons, et mènes-tu la grande Ourse avec ses filles?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Connais-tu les lois des cieux, ou établis-tu leur empire sur la terre?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Peux-tu élever ta voix vers les nuages, en sorte que des torrents d’eau te couvrent?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 As-tu lancé la foudre, en sorte qu’elle soit allée et t’ait dit: Me voici?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Qui a mis la sagesse dans les reins, ou qui donna l’intelligence à l’esprit?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Qui a compté les nuages dans [sa] sagesse? et qui verse les outres des cieux,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 Quand la poussière coule comme du métal en fusion et que les mottes se soudent entre elles?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Est-ce toi qui chasses la proie pour la lionne, et qui rassasies l’appétit des lionceaux,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 Quand ils sont couchés dans leurs tanières [et] se tiennent aux aguets dans leur fourré?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Qui prépare au corbeau sa pâture quand ses petits crient à Dieu [et] qu’ils errent sans nourriture?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?