< Job 30 >

1 Et maintenant, ceux qui sont plus jeunes que moi se moquent de moi, ceux dont j’aurais dédaigné de mettre les pères avec les chiens de mon troupeau.
Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
2 Même à quoi m’aurait servi la force de leurs mains? La vigueur a péri pour eux.
Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
3 Desséchés par la disette et la faim, ils s’enfuient dans les lieux arides, dès longtemps désolés et déserts;
Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
4 Ils cueillent le pourpier de mer parmi les broussailles, et, pour leur pain, la racine des genêts.
Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
5 Ils sont chassés du milieu [des hommes], (on crie après eux comme après un voleur, )
Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
6 Pour demeurer dans des gorges affreuses, dans les trous de la terre et des rochers;
Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
7 Ils hurlent parmi les broussailles, ils se rassemblent sous les ronces:
Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
8 Fils d’insensés, et fils de gens sans nom, ils sont chassés du pays.
Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
9 Et maintenant, je suis leur chanson et je suis le sujet de leur entretien.
Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
10 Ils m’ont en horreur, ils se tiennent loin de moi, et n’épargnent pas à ma face les crachats;
Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
11 Car Il a délié ma corde et m’a affligé: ils ont jeté loin [tout] frein devant moi.
Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
12 Cette jeune engeance se lève à ma droite; ils poussent mes pieds et préparent contre moi leur chemin pernicieux;
Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
13 Ils détruisent mon sentier, ils contribuent à ma calamité, sans que personne leur vienne en aide;
Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
14 Ils viennent comme par une large brèche, ils se précipitent au milieu du fracas.
Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
15 Des terreurs m’assaillent, elles poursuivent ma gloire comme le vent, et mon état de sûreté est passé comme une nuée.
Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
16 Et maintenant, mon âme se répand en moi: les jours d’affliction m’ont saisi.
Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
17 La nuit perce mes os [et les détache] de dessus moi, et ceux qui me rongent ne dorment pas;
Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
18 Par leur grande force ils deviennent mon vêtement; ils me serrent comme le collet de ma tunique.
Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
19 Il m’a jeté dans la boue, et je suis devenu comme la poussière et la cendre.
Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
20 Je crie à toi, et tu ne me réponds pas; je me tiens là, et tu me regardes!
Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
21 Tu t’es changé pour moi en [ennemi] cruel; tu me poursuis avec la force de ta main.
Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
22 Tu m’enlèves sur le vent, tu fais qu’il m’emporte, et tu dissous ma substance.
Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
23 Car je sais que tu m’amènes à la mort, la maison de rassemblement de tous les vivants.
Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
24 Toutefois, dans sa ruine, n’étend-il pas la main, et, dans sa calamité, ne jette-t-il pas un cri [de détresse]?
Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
25 N’ai-je pas pleuré sur celui pour qui les temps étaient durs, et mon âme n’a-t-elle pas été attristée pour le pauvre?
Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
26 Car j’attendais le bien, et le mal est arrivé; je comptais sur la lumière, et l’obscurité est venue.
Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
27 Mes entrailles bouillonnent et ne cessent pas; les jours d’affliction sont venus sur moi.
Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
28 Je marche tout noirci, mais non par le soleil; je me lève dans l’assemblée, je crie;
Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
29 Je suis devenu le frère des chacals et le compagnon des autruches.
Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
30 Ma peau devient noire [et se détache] de dessus moi, et mes os sont brûlés par la sécheresse;
Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
31 Et ma harpe est changée en deuil, et mon chalumeau est devenu la voix des pleureurs.
Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.

< Job 30 >