< Job 16 >

1 Et Job répondit et dit:
Kisha Ayubu akajibu:
2 J’ai entendu bien des choses comme celles-là; vous êtes tous des consolateurs fâcheux.
“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
3 Y aura-t-il une fin à [ces] paroles de vent? Qu’est-ce qui t’irrite, que tu répondes?
Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
4 Moi aussi, je pourrais parler comme vous; si votre âme était à la place de mon âme, je pourrais entasser des paroles contre vous et secouer ma tête contre vous!
Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 [Mais] je vous fortifierais de ma bouche, et la consolation de mes lèvres allégerait [vos douleurs].
Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
6 Si je parle, ma douleur n’est pas allégée; et si je me tais, s’éloignera-t-elle de moi?
“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
7 Mais maintenant, il m’a fatigué…: tu as dévasté toute ma famille;
Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
8 Tu m’as étreint, c’est un témoignage, et ma maigreur se lève contre moi, elle dépose, à ma face, contre moi.
Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
9 Sa colère me déchire et me poursuit; il grince des dents contre moi; [comme] mon adversaire, il aiguise contre moi ses yeux.
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10 Ils ouvrent contre moi leur bouche, ils me frappent les joues avec mépris; ils s’attroupent contre moi.
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11 Dieu m’a livré à l’inique, et m’a jeté entre les mains des méchants.
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12 J’étais en paix, et il m’a brisé; il m’a saisi par la nuque et m’a broyé, et m’a dressé pour lui servir de but.
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13 Ses archers m’ont environné; il me perce les reins et ne m’épargne pas; il répand mon fiel sur la terre.
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14 Il fait brèche en moi, brèche sur brèche; il court sur moi comme un homme fort.
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
15 J’ai cousu un sac sur ma peau, et j’ai dégradé ma corne dans la poussière.
“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
16 Mon visage est enflammé à force de pleurer, et sur mes paupières est l’ombre de la mort,
Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
17 Quoiqu’il n’y ait pas de violence dans mes mains, et que ma prière soit pure.
Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
18 Ô terre, ne recouvre pas mon sang, et qu’il n’y ait pas de place pour mon cri!
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19 Maintenant aussi, voici, mon témoin est dans les cieux, et celui qui témoigne pour moi est dans les lieux élevés.
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20 Mes amis se moquent de moi… vers Dieu pleurent mes yeux.
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21 Que n’y a-t-il un arbitre pour l’homme auprès de Dieu, et pour un fils d’homme vis-à-vis de son ami!
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22 Car les années s’écoulent dont on peut compter le nombre, et je m’en vais dans le chemin [d’où] je ne reviendrai pas.
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

< Job 16 >