< Job 12 >

1 Et Job répondit et dit:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 Vraiment vous êtes les [seuls] hommes, et avec vous mourra la sagesse!
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 Moi aussi j’ai du sens comme vous, je ne vous suis pas inférieur; et de qui de telles choses ne sont-elles pas [connues]?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 Je suis un [homme] qui est la risée de ses amis, criant à Dieu, et à qui il répondra; – le juste parfait est un objet de risée!
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 Celui qui est prêt à broncher de ses pieds est une lampe méprisée pour les pensées de celui qui est à son aise.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 Les tentes des dévastateurs prospèrent, et la confiance est pour ceux qui provoquent Dieu, pour celui dans la main duquel Dieu a fait venir [l’abondance].
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 Mais, je te prie, interroge donc les bêtes, et elles t’enseigneront, et les oiseaux des cieux, et ils te l’annonceront;
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Ou parle à la terre, et elle t’enseignera, et les poissons de la mer te le raconteront.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Qui d’entre tous ceux-ci ne sait pas que la main de l’Éternel a fait cela,
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 Lui, dans la main duquel est l’âme de tout être vivant et l’esprit de toute chair d’homme?
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 L’oreille n’éprouve-t-elle pas les discours, comme le palais goûte les aliments?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 Chez les vieillards est la sagesse, et dans beaucoup de jours l’intelligence.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 Avec lui est la sagesse et la force, à lui sont le conseil et l’intelligence.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Voici, il démolit, et on ne rebâtit pas; il enferme un homme, et on ne lui ouvre pas.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Voici, il retient les eaux, et elles tarissent; puis il les envoie, et elles bouleversent la terre.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Avec lui est la force et la parfaite connaissance; à lui sont celui qui erre et celui qui fait errer.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 Il emmène captifs les conseillers, et rend fous les juges;
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 Il rend impuissant le gouvernement des rois, et lie de chaînes leurs reins;
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 Il emmène captifs les sacrificateurs, et renverse les puissants;
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 Il ôte la parole à ceux dont la parole est sûre, et enlève le discernement aux anciens;
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 Il verse le mépris sur les nobles, et relâche la ceinture des forts;
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 Il révèle du sein des ténèbres les choses profondes, et fait sortir à la lumière l’ombre de la mort;
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 Il agrandit les nations, et les détruit; il étend les limites des nations, et les ramène.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 Il ôte le sens aux chefs du peuple de la terre, et les fait errer dans un désert où il n’y a pas de chemin;
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Ils tâtonnent dans les ténèbres où il n’y a point de lumière; il les fait errer comme un homme ivre.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >