< Isaïe 23 >
1 L’oracle sur Tyr. Hurlez, navires de Tarsis, car elle est dévastée, de sorte qu’il n’y a pas de maisons, personne qui entre. Du pays de Kittim cela leur est révélé.
Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
2 Tenez-vous en silence, habitants de l’île! Les marchands de Sidon qui passent par la mer t’ont remplie!
Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
3 Et sur de grandes eaux la semence du Shikhor, la moisson du Nil, était son revenu; et elle était le marché des nations.
Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
4 Aie honte, Sidon, car la mer a parlé, la force de la mer, disant: Je n’ai pas été en travail d’enfant, je n’ai pas enfanté, et je n’ai pas nourri de jeunes hommes, ni élevé de vierges. –
Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
5 Quand la rumeur est arrivée en Égypte, ils ont été dans l’angoisse à [l’ouïe des] nouvelles de Tyr.
Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
6 Traversez vers Tarsis, hurlez, vous, les habitants de l’île!
Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
7 Est-ce là votre [ville] joyeuse, qui avait son origine dès les jours d’autrefois? Ses pieds la porteront pour demeurer au loin en étrangère.
Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
8 Qui a pris ce conseil à l’égard de Tyr, distributrice de couronnes, dont les négociants étaient des princes, dont les marchands étaient les nobles de la terre?
Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
9 L’Éternel des armées a pris ce conseil, pour profaner l’orgueil de toute gloire, pour réduire à néant tous les nobles de la terre.
Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
10 Répands-toi sur ton pays comme le Nil, fille de Tarsis; il n’y a plus rien qui retienne!
Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
11 Il a étendu sa main sur la mer; il a fait trembler les royaumes. L’Éternel a commandé contre Canaan, d’en détruire les forteresses,
Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
12 et il a dit: Tu ne t’égaieras plus, vierge opprimée, fille de Sidon! Lève-toi, passe à Kittim; là encore il n’y aura pas de repos pour toi.
Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
13 Vois le pays des Chaldéens: ce peuple n’existait pas; Assur l’a fondé pour les habitants des déserts: ils ont élevé leurs tours, ils ont renversé ses palais; il en a fait des ruines.
Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
14 Hurlez, navires de Tarsis, car votre forteresse est détruite.
Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
15 Et il arrivera, en ce jour-là, que Tyr sera oubliée 70 ans, selon les jours d’un roi. Au bout de 70 ans, ce sera pour Tyr comme la chanson d’une prostituée.
Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
16 Prends la harpe, fais le tour de la ville, prostituée oubliée! Touche habilement les cordes, multiplie tes chansons, afin qu’on se souvienne de toi.
“Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
17 Et il arrivera qu’au bout de 70 ans, l’Éternel visitera Tyr; et elle reviendra à ses présents et se prostituera avec tous les royaumes de la terre, sur la face du sol.
Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
18 Et ses marchandises et les présents qu’on lui fera seront saints, [consacrés] à l’Éternel; ils ne seront pas accumulés et ils ne seront pas amassés; car sa marchandise sera pour ceux qui demeurent devant l’Éternel, afin qu’ils mangent et soient rassasiés, et afin qu’ils aient des vêtements magnifiques.
Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.