< Genèse 42 >

1 Et Jacob vit qu’il y avait du blé en Égypte; et Jacob dit à ses fils: Pourquoi vous regardez-vous les uns les autres?
Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
2 Et il dit: Voici, j’ai appris qu’il y a du blé en Égypte; descendez-y, et achetez-nous-en là, afin que nous vivions, et que nous ne mourions pas.
Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
3 Et dix frères de Joseph descendirent pour acheter du blé en Égypte;
Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
4 mais Jacob n’envoya pas Benjamin, le frère de Joseph, avec ses frères, car il disait: De peur qu’un accident ne lui arrive!
Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
5 Et les fils d’Israël allèrent pour acheter du blé, parmi ceux qui allaient; car la famine était dans le pays de Canaan.
Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
6 Et Joseph était gouverneur du pays; il vendait le blé à tout le peuple du pays. Et les frères de Joseph vinrent, et se prosternèrent devant lui la face contre terre.
Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
7 Et Joseph vit ses frères, et les reconnut; et il fit l’étranger vis-à-vis d’eux, et leur parla durement, et leur dit: D’où venez-vous? Et ils dirent: Du pays de Canaan, pour acheter des vivres.
Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
8 Et Joseph reconnut ses frères; et eux ne le reconnurent pas.
Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua.
9 Et Joseph se souvint des songes qu’il avait songés à leur sujet, et il leur dit: Vous êtes des espions; c’est pour voir les lieux ouverts du pays que vous êtes venus.
Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
10 Et ils lui dirent: Non, mon seigneur; mais tes serviteurs sont venus pour acheter des vivres.
Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
11 Nous sommes tous fils d’un seul homme; nous sommes d’honnêtes gens; tes serviteurs ne sont pas des espions.
Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”
12 Et il leur dit: Non; mais vous êtes venus pour voir les lieux ouverts du pays.
Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
13 Et ils dirent: Tes serviteurs étaient douze frères; nous sommes fils d’un seul homme, au pays de Canaan; et voici, le plus jeune est aujourd’hui avec notre père, et l’un n’est plus.
Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”
14 Et Joseph leur dit: C’est ce que je vous disais, en disant: Vous êtes des espions.
Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi!
15 Par ceci vous serez mis à l’épreuve: Vie du Pharaon! si vous sortez d’ici, à moins que votre jeune frère ne vienne ici!
Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa.
16 Envoyez l’un de vous, et qu’il aille chercher votre frère; et vous, vous serez liés, et vos paroles seront mises à l’épreuve, [pour voir] si la vérité est avec vous: sinon, vie du Pharaon! certainement vous êtes des espions.
Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!”
17 Et il les fit mettre ensemble sous garde pendant trois jours.
Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.
18 Et, le troisième jour, Joseph leur dit: Faites ceci, et vous vivrez; moi je crains Dieu.
Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu:
19 Si vous êtes d’honnêtes gens, l’un de vous, qui êtes frères, sera lié dans la maison où vous avez été sous garde; et vous, allez, emportez du blé pour la faim de vos maisons;
Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa.
20 et amenez-moi le plus jeune de vos frères, et vos paroles se trouveront vraies; et vous ne mourrez pas. Et ils firent ainsi.
Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.
21 Et ils se dirent l’un à l’autre: Certainement nous sommes coupables à l’égard de notre frère; car nous avons vu la détresse de son âme quand il nous demandait grâce, et nous ne l’avons pas écouté; c’est pourquoi cette détresse est venue sur nous.
Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
22 Et Ruben leur répondit, disant: Ne vous ai-je pas parlé, disant: Ne péchez pas contre l’enfant? Mais vous n’avez pas écouté; et aussi, voici, son sang est redemandé.
Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.”
23 Et ils ne savaient pas que Joseph comprenait, car il y avait entre eux un interprète.
Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.
24 Et il se détourna d’auprès d’eux, et pleura; et il revint vers eux, et leur parla, et prit d’avec eux Siméon, et le lia devant leurs yeux.
Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.
25 Et Joseph commanda de remplir de blé leurs sacs, et de leur remettre leur argent à chacun dans son sac, et de leur donner des provisions pour le chemin; et on leur fit ainsi.
Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote,
26 Et ils chargèrent leur blé sur leurs ânes, et s’en allèrent de là.
wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.
27 Et l’un [d’eux] ouvrit son sac pour donner à manger à son âne, dans le caravansérail, et il vit son argent, et voici, il était à l’ouverture de son sac.
Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake.
28 Et il dit à ses frères: Mon argent m’a été rendu; et même, le voici dans mon sac! Et le cœur leur manqua, et ils furent saisis de peur, se disant l’un à l’autre: Qu’est-ce que Dieu nous a fait?
Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.” Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”
29 Et ils vinrent vers Jacob, leur père, au pays de Canaan, et ils lui racontèrent tout ce qui leur était arrivé, disant:
Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema,
30 L’homme, le seigneur du pays, nous a parlé durement, et nous a traités comme des espions du pays;
“Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi.
31 et nous lui avons dit: Nous sommes d’honnêtes gens, nous ne sommes pas des espions.
Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi.
32 Nous étions douze frères, fils de notre père: l’un n’est plus, et le plus jeune est aujourd’hui avec notre père au pays de Canaan.
Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’
33 Et l’homme, le seigneur du pays, nous a dit: À ceci je connaîtrai que vous êtes d’honnêtes gens: Laissez auprès de moi l’un de vos frères, et prenez [du blé] pour la faim de vos maisons, et allez-vous-en.
“Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa.
34 Et amenez-moi votre plus jeune frère, et je connaîtrai que vous n’êtes pas des espions, mais que vous êtes d’honnêtes gens: je vous donnerai votre frère, et vous trafiquerez dans le pays.
Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’”
35 Et il arriva, comme ils vidaient leurs sacs, que voici, chacun avait son paquet d’argent dans son sac; et ils virent, eux et leur père, leurs paquets d’argent, et ils eurent peur.
Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa.
36 Et Jacob, leur père, leur dit: Vous m’avez privé d’enfants: Joseph n’est plus, et Siméon n’est plus, et vous voulez prendre Benjamin! Toutes ces choses sont contre moi.
Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”
37 Et Ruben parla à son père, disant: Tu feras mourir mes deux fils si je ne te le ramène; remets-le entre mes mains, et je te le ramènerai.
Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”
38 Mais il dit: Mon fils ne descendra pas avec vous; car son frère est mort, et lui seul est resté; si quelque accident lui arrivait dans le chemin où vous allez, vous feriez descendre mes cheveux blancs avec douleur au shéol. (Sheol h7585)
Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol h7585)

< Genèse 42 >