< Galates 5 >

1 Christ nous a placés dans la liberté en nous affranchissant; tenez-vous donc fermes, et ne soyez pas de nouveau retenus sous un joug de servitude.
Ni kwa sababu Kristo alitupa uhuru ili tuwe huru. Hivyo, simameni imara wala msinaswe tena katika kongwa la utumwa.
2 Voici, moi Paul, je vous dis que si vous êtes circoncis, Christ ne vous profitera de rien;
Tazama, Mimi Paulo, ninawaambia kwamba ikiwa mtatahiriwa, Kristo hatawafaidia kwa njia yoyote ile.
3 et je proteste de nouveau à tout homme circoncis, qu’il est tenu d’accomplir toute la loi.
Tena, namshuhudia kila mwanaume aliyetahiriwa kwamba anapaswa kuwajibika kwa sheria yote.
4 Vous vous êtes séparés de tout le bénéfice qu’il y a dans le Christ, vous tous qui vous justifiez par [la] loi; vous êtes déchus de la grâce.
Mmetengwa mbali na Kristo, wale wote “mnaohesabiwa haki” kwa sheria. Mmeanguka mbali na neema.
5 Car nous, par [l’]Esprit, sur le principe de [la] foi, nous attendons l’espérance de la justice.
Maana kwa njia ya Roho, kwa imani tunasubiri ujasiri wa haki.
6 Car, dans le christ Jésus, ni circoncision, ni incirconcision, n’ont de valeur, mais [la] foi opérante par [l’]amour.
Katika Kristo Yesu kutahiriwa au kutokutahiriwa hakuna maana yoyote. Ni imani pekee inayofanya kazi kupitia upendo ndiyo humaanisha kitu.
7 Vous couriez bien, qui est-ce qui vous a arrêtés pour que vous n’obéissiez pas à la vérité?
Mlikuwa mnapiga mbio vizuri. Nani aliwazuia kutokuitii kweli?
8 La persuasion ne vient pas de celui qui vous appelle.
Ushawishi wa kufanya hivyo hautoki kwake yeye anayewaita ninyi.
9 Un peu de levain fait lever la pâte tout entière.
Chachu kidogo huathiri donge zima.
10 J’ai confiance à votre égard par le Seigneur, que vous n’aurez point d’autre sentiment; mais celui qui vous trouble, quel qu’il soit, en portera le jugement.
Nina matumaini na ninyi katika Bwana kwamba hamtafikiri kwa njia nyingine yoyote. Yeyote yule atakayewapotosha atabeba hukumu yake yeye mwenyewe, yeyote yule.
11 Mais moi, frères, si je prêche encore la circoncision, pourquoi suis-je encore persécuté? – alors le scandale de la croix est anéanti.
Ndugu, kama naendelea kutangaza tohara, kwanini bado ninateswa? Kwa suala hilo kile ambacho ni kizuizi cha msalaba kitaweza kuharibiwa.
12 Je voudrais que ceux qui vous bouleversent se retranchent même.
Ni matakwa yangu kuwa wale wanaowaongoza vibaya watajihasi wenyewe.
13 Car vous, frères, vous avez été appelés à la liberté; seulement [n’usez] pas de la liberté comme d’une occasion pour la chair, mais, par amour, servez-vous l’un l’autre;
Mungu amewaiteni ninyi, ndugu, kwenye uhuru. Ila msiutumie uhuru wenu kama fursa kwa mwili. Badala yake kwa upendo mhudumiane ninyi kwa ninyi.
14 car toute la loi est accomplie dans une seule parole, dans celle-ci: « Tu aimeras ton prochain comme toi-même ».
Kwa kuwa sheria yote imekamilika katika amri moja; nayo ni “Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”
15 Mais si vous vous mordez et vous dévorez l’un l’autre, prenez garde que vous ne soyez consumés l’un par l’autre.
Lakini kama mkiumana na kulana, jiangalieni kwamba msijiharibu ninyi kwa ninyi.
16 Mais je dis: Marchez par l’Esprit, et vous n’accomplirez point la convoitise de la chair.
Nasema, tembeeni kwa roho, na wala hamtazitimiza tamaa za mwili.
17 Car la chair convoite contre l’Esprit, et l’Esprit contre la chair; et ces choses sont opposées l’une à l’autre, afin que vous ne pratiquiez pas les choses que vous voudriez.
Kwa kuwa mwili una tamaa kubwa dhidi ya Roho, na Roho ina tamaa kubwa dhidi ya mwili. Hizi zinapingana kila moja na nyingine. Matokeo ni kwamba hamfanyi vitu mnavyotamani kuvifanya.
18 Mais si vous êtes conduits par [l’]Esprit, vous n’êtes pas sous [la] loi.
Lakini kama Roho anawaongoza ninyi, hamko chini ya sheria.
19 Or les œuvres de la chair sont manifestes, lesquelles sont la fornication, l’impureté, l’impudicité,
Sasa matendo ya mwili yanaonekana. Nayo ni uasherati, uchafu, ufisadi,
20 l’idolâtrie, la magie, les inimitiés, les querelles, les jalousies, les colères, les intrigues, les divisions, les sectes,
ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, husuda, kuwaka hasira, ushindani, faraka, mgawanyiko wa madhehebu,
21 les envies, les meurtres, les ivrogneries, les orgies, et les choses semblables à celles-là, au sujet desquelles je vous déclare d’avance, comme aussi je l’ai déjà dit, que ceux qui commettent de telles choses n’hériteront pas du royaume de Dieu.
wivu, ulevi, ulafi na mambo mengine kama haya. Nawaonya ninyi, kama nilivyowaonya mwanzoni, kwamba wale wanaofanya mambo kama hayo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Mais le fruit de l’Esprit est l’amour, la joie, la paix, la longanimité, la bienveillance, la bonté, la fidélité,
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, ukarimu, utu wema, imani,
23 la douceur, la tempérance: contre de telles choses, il n’y a pas de loi.
upole, na kiasi. Hakuna sheria dhidi ya mambo kama hayo.
24 Or ceux qui sont du Christ ont crucifié la chair avec les passions et les convoitises.
Wale walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na shauku na tamaa zao mbaya.
25 Si nous vivons par l’Esprit, marchons aussi par l’Esprit.
Kama tukiishi kwa Roho, pia tutembee kwa Roho.
26 Ne soyons pas désireux de vaine gloire, en nous provoquant les uns les autres [et] en nous portant envie les uns aux autres.
Tusiwe wa kujivuna, tusichokozane kila mmoja na mwenzake, wala tusioneane wivu.

< Galates 5 >