< Ézéchiel 26 >
1 Et il arriva, la onzième année, le premier [jour] du mois, que la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils d’homme, parce que Tyr a dit touchant Jérusalem: Ha ha! elle est brisée, la porte des peuples! elle est tournée vers moi; je serai remplie; elle a été rendue déserte; …
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 à cause de cela, ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Voici, j’en veux à toi, Tyr! et je ferai monter contre toi des nations nombreuses, comme la mer fait monter ses flots.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 Et elles détruiront les murs de Tyr et renverseront ses tours; et je balaierai d’elle sa poussière, et je ferai d’elle un rocher nu.
Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 Elle sera un lieu pour étendre les filets, au milieu de la mer; car j’ai parlé, dit le Seigneur, l’Éternel; et elle deviendra la proie des nations;
Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 et ses filles qui sont dans la campagne seront tuées par l’épée; et ils sauront que je suis l’Éternel.
nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 Car ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Voici, je fais venir du nord, contre Tyr, Nebucadretsar, roi de Babylone, le roi des rois, avec des chevaux, et des chars, et des cavaliers, et un rassemblement et un peuple nombreux.
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 Tes filles qui sont dans la campagne, il les tuera par l’épée; et il établira contre toi des tours; et il élèvera contre toi des terrasses; et il lèvera le bouclier contre toi;
Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 et il placera ses machines de siège contre tes murailles, et démolira tes tours avec ses pointes de fer.
Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 À cause de la multitude de ses chevaux, leur poussière te couvrira; tes murailles trembleront au bruit de la cavalerie, et des roues et des chars, quand il entrera par tes portes comme on entre dans une ville ouverte par la brèche.
Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 Sous le sabot de ses chevaux il foulera toutes tes rues; il tuera ton peuple par l’épée, et les colonnes de ta force tomberont par terre.
“Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 Et ils feront une proie de tes richesses, et pilleront tes biens, et renverseront tes murs, et abattront tes maisons de plaisance; et ils mettront tes pierres, et ton bois, et ta poussière, au milieu des eaux.
Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 Et je ferai cesser le bruit de tes chansons, et le son de tes harpes ne sera plus entendu.
Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 Et je ferai de toi un rocher nu; tu seras un lieu pour étendre les filets; et tu ne seras plus bâtie; car moi, l’Éternel, j’ai parlé, dit le Seigneur, l’Éternel.
Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
15 Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel, à Tyr: Les îles ne trembleront-elles pas au bruit de ta chute, au gémissement de tes blessés à mort, quand le carnage se fera au milieu de toi?
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 Et tous les princes de la mer descendront de leurs trônes, et ôteront leurs robes, et dépouilleront leurs vêtements de broderie; ils se revêtiront de frayeur, ils s’assiéront sur la terre, et ils trembleront à tout moment et seront dans la stupeur à cause de toi.
Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
17 Et ils élèveront une complainte sur toi, et te diront: Comment as-tu péri, toi qui étais habitée par ceux qui venaient des mers, ville célèbre qui étais puissante sur la mer, toi et tes habitants qui répandiez votre terreur sur tous ceux qui habitent en elle?
Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Maintenant les îles tremblent au jour de ta chute, et les îles qui sont dans la mer seront troublées à cause de l’issue de ta [voie].
Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 Car ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Quand je ferai de toi une ville déserte, comme sont les villes qui ne sont pas habitées; quand je ferai monter sur toi l’abîme, et que les grandes eaux te couvriront,
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 alors je te ferai descendre avec ceux qui descendent dans la fosse, vers le peuple d’autrefois, et je te ferai habiter dans les lieux bas de la terre, dans les lieux désolés de tout temps, avec ceux qui descendent dans la fosse, afin que tu ne sois plus habitée, et que je mette la gloire dans la terre des vivants.
ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 Je ferai de toi une terreur, et tu ne seras plus; et on te cherchera, et on ne te trouvera plus, à jamais, dit le Seigneur, l’Éternel.
Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”