< Ézéchiel 24 >
1 Et la parole de l’Éternel vint à moi, en la neuvième année, au dixième mois, le dixième [jour] du mois, disant:
Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils d’homme, écris pour toi le nom de ce jour, de ce propre jour: le roi de Babylone s’approche contre Jérusalem, en ce jour même.
“Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
3 Et propose une parabole à la maison rebelle, et dis-leur: Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Place la marmite, place-la, et verses-y aussi de l’eau.
Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
4 Rassembles-y ses morceaux, tous les bons morceaux, la cuisse et l’épaule; remplis-la d’os choisis,
Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
5 prends du meilleur du menu bétail; et [mets] aussi dessous un tas de bois pour les os; fais-la bien bouillir, et que les os cuisent au-dedans d’elle.
chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea mpaka ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
6 C’est pourquoi, ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Malheur à la ville de sang, la marmite en laquelle est sa rouille, et dont la rouille ne se détache pas! Tires-en morceau par morceau; qu’on ne jette pas le sort sur elle;
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
7 car son sang est au milieu d’elle: elle l’a mis sur le roc nu, elle ne l’a pas versé sur la terre pour le couvrir de poussière.
“‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
8 Pour faire monter la fureur, pour exécuter la vengeance, j’ai mis son sang sur le roc nu, pour qu’il ne soit pas couvert.
Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
9 C’est pourquoi, ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Malheur à la ville de sang! Moi aussi je ferai une grande pile de bois.
“‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
10 Entasse le bois, allume le feu, fais consommer la chair, assaisonne-la bien, et que les os soient brûlés.
Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya viungo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
11 Place-la vide sur les charbons ardents, afin qu’elle s’échauffe et que son airain devienne brûlant, et que son impureté soit fondue au-dedans d’elle [et] que sa rouille soit consumée.
Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
12 Elle a lassé les efforts, et la rouille dont elle est pleine ne se détache pas: – au feu sa rouille!
Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
13 Il y a de l’infamie dans ton impureté; puisque je t’ai purifiée, et tu n’es point pure. Tu ne seras plus purifiée de ton impureté, jusqu’à ce que j’aie satisfait sur toi ma fureur.
“‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
14 Moi, l’Éternel, j’ai parlé: cela arrivera, et je le ferai; je ne reculerai point, et je n’aurai point de compassion, et je ne me repentirai pas. On te jugera selon tes voies et selon tes actions, dit le Seigneur, l’Éternel.
“‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’”
15 Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
16 Fils d’homme, voici, je vais t’ôter, par une plaie, le désir de tes yeux; et tu ne mèneras pas deuil, et tu ne pleureras pas, et tes larmes ne couleront pas.
“Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
17 Gémis en silence: tu ne feras point le deuil des morts. Enroule ton turban sur toi, et mets tes sandales à tes pieds, et ne couvre pas ta barbe, et ne mange pas le pain des hommes. –
Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”
18 Et je parlai au peuple le matin, et ma femme mourut le soir; et, le matin, je fis comme il m’avait été commandé.
Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.
19 Et le peuple me dit: Ne nous déclareras-tu pas ce que signifient pour nous ces choses que tu fais?
Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
20 Et je leur dis: La parole de l’Éternel est venue à moi, disant:
Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
21 Dis à la maison d’Israël: Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Voici, je profane mon sanctuaire, l’orgueil de votre force, le désir de vos yeux, et l’affection de votre âme; et vos fils et vos filles que vous avez laissés en arrière tomberont par l’épée.
‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
22 Et vous ferez comme j’ai fait: vous ne couvrirez point votre barbe et vous ne mangerez pas le pain des hommes;
Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
23 et vos turbans seront sur vos têtes, et vos sandales à vos pieds; vous ne mènerez pas deuil et vous ne pleurerez pas, mais vous vous consumerez dans vos iniquités, et vous gémirez l’un vis-à-vis de l’autre.
Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
24 Et Ézéchiel sera pour vous un signe: selon tout ce qu’il a fait, vous ferez. Quand cela arrivera, vous saurez que je suis le Seigneur, l’Éternel.
Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’
25 Et toi, fils d’homme, au jour où je leur ôterai ce qui a été leur confiance, la joie de leur ornement, le désir de leurs yeux, et ce que recherchent leurs âmes, leurs fils et leurs filles,
“Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile,
26 en ce jour-là celui qui sera réchappé ne viendra-t-il pas vers toi pour le faire entendre à tes oreilles?
siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
27 En ce jour-là ta bouche sera ouverte avec le réchappé, et tu parleras et tu ne seras plus muet; et tu seras pour eux un signe, et ils sauront que je suis l’Éternel.
Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”