< Exode 37 >
1 Et Betsaleël fit l’arche de bois de sittim: sa longueur était de deux coudées et demie, et sa largeur d’une coudée et demie, et sa hauteur d’une coudée et demie.
Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
2 Et il la plaqua d’or pur, dedans et dehors, et lui fit un couronnement d’or tout autour;
Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
3 et il fondit pour elle quatre anneaux d’or, pour ses quatre coins, deux anneaux à l’un de ses côtés, et deux anneaux à l’autre de ses côtés.
Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
4 Et il fit des barres de bois de sittim, et les plaqua d’or;
Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
5 et il fit entrer les barres dans les anneaux, aux côtés de l’arche, pour porter l’arche.
Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
6 – Et il fit un propitiatoire d’or pur: sa longueur était de deux coudées et demie, et sa largeur d’une coudée et demie.
Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
7 Et il fit deux chérubins d’or; il les fit d’or battu, aux deux bouts du propitiatoire,
Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
8 un chérubin au bout de deçà, et un chérubin au bout de delà; il fit les chérubins [tirés] du propitiatoire, à ses deux bouts.
Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
9 Et les chérubins étendaient les ailes en haut, couvrant de leurs ailes le propitiatoire; et leurs faces étaient l’une vis-à-vis de l’autre; les faces des chérubins étaient [tournées] vers le propitiatoire.
Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
10 Et il fit la table de bois de sittim: sa longueur était de deux coudées, et sa largeur d’une coudée, et sa hauteur d’une coudée et demie;
Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 et il la plaqua d’or pur, et y fit un couronnement d’or tout autour.
Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
12 Et il y fit un rebord d’une paume tout autour, et il fit un couronnement d’or à son rebord, tout autour;
Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
13 et il lui fondit quatre anneaux d’or, et il mit les anneaux aux quatre coins qui étaient à ses quatre pieds.
Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
14 Les anneaux étaient près du rebord, pour recevoir les barres, pour porter la table;
Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
15 et il fit les barres de bois de sittim, et les plaqua d’or, pour porter la table.
Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
16 Et il fit d’or pur les ustensiles qui étaient sur la table, ses plats, et ses coupes, et ses vases, et les gobelets avec lesquels on fait les libations.
Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
17 Et il fit le chandelier d’or pur; il fit le chandelier [d’or] battu; son pied, et sa tige, ses calices, ses pommes, et ses fleurs, étaient [tirés] de lui;
Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
18 et six branches sortaient de ses côtés, trois branches du chandelier d’un côté, et trois branches du chandelier de l’autre côté.
Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
19 Il y avait, sur une branche, trois calices en forme de fleur d’amandier, une pomme et une fleur, et, sur une [autre] branche, trois calices en forme de fleur d’amandier, une pomme et une fleur; ainsi pour les six branches sortant du chandelier.
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
20 Et il y avait au chandelier quatre calices en forme de fleur d’amandier, ses pommes et ses fleurs;
Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
21 et une pomme sous deux branches [sortant] de lui, et une pomme sous deux branches [sortant] de lui, et une pomme sous deux branches [sortant] de lui, pour les six branches qui sortaient de lui;
Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
22 leurs pommes et leurs branches étaient [tirées] de lui, le tout battu, d’une pièce, d’or pur.
Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
23 – Et il fit ses sept lampes, et ses mouchettes, et ses vases à cendre, d’or pur:
Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
24 il le fit, avec tous ses ustensiles, d’un talent d’or pur.
Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
25 Et il fit l’autel de l’encens, de bois de sittim: sa longueur était d’une coudée, et sa largeur d’une coudée; il était carré; et sa hauteur était de deux coudées; ses cornes étaient [tirées] de lui.
Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
26 Et il le plaqua d’or pur, le dessus et ses parois, tout autour, et ses cornes. Et il lui fit un couronnement d’or tout autour.
Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
27 Et il lui fit deux anneaux d’or au-dessous de son couronnement, sur ses deux côtés, à ses deux coins, pour recevoir les barres, pour le porter par elles.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
28 Et il fit les barres de bois de sittim, et les plaqua d’or.
Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
29 Et il fit l’huile sainte de l’onction et le pur encens des drogues odoriférantes, d’ouvrage de parfumeur.
Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.